Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Biashara ya nje inayoandaa Maonyesho ya Biashara ya SabaSaba Mh. Ramadhani Khalfan akikata utepe lango kuu katika uwanja wa mwalim J K Nyere mara baada ya kampuni ya simu ya Tigo kukabidhi maeneo ya kimvuli cha kudumu yaliyojengwa na Tigo kwa ajili ya kuwakinga jua na mvua waalikwa na wageni watakaotembea viwanjani hapo wakati wa maonyeso kuanzia Jumamosi hii. Shoto ni bosi wa Masoko wa Tigo Kelvin Twissa.



Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa maonesho ya 32 ya sabasaba Julai 1, 2008, ambapo kutakuwa na maonesho ya nchi 27, wizara 9, idara 38 na serikali, kampuni za bongo 650 pamoja na wadau wa biashara ndogondogo 60, wakiwamo machinga ambao wanashiriki kwa mara ya kwanza mwaka huu.

Daily News na HabariLeo nao watakuwepo kufanya kile walichofanya wakati wa mkutano wa Sullivan A-taun kwa maonesho ya mapicha na shughuli za gazeti hilo mama la magazeti nchini ambalo limeendeleza libeneke kwa miaka 75 sasa.

Tigo ndio kampuni rasmi ya mawasiliano katika maonesho haya na tayari imeanda shughuli kibao na zawadi kedekede kwenye banda lake

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 28, 2008

    Seems like TIGO wana spend a lot of money for PR. I wonder if return on investment ni nzuri :)

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 28, 2008

    I think its better for them to spend money for PR because TIGO seems to die few years ago, and from my own outlook Kelvin Twisa his good.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 28, 2008

    Via their promotions and PR activities they make wonders thousands of people connected to this company last two years due to publicity.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 28, 2008

    NAKUPENDA TWISA!! UNAJUA KAZI KIJANA MUNGU AKUZIDISHIE

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...