FC BONGO jana kiliwazima midomo wana Tampere fc kwa idadi ya magoli 5-1 na mpira safi wa kuburudisha ndani ya jiji la Tampere Finland.

Baada ya kurejea kutoka Sweden na usongo mkubwa wa kufungwa na wana kilimanjaro wa stockholm, Fc Bongo walimalizia hasira zao bila huruma kwa watani wao wa jadi nchini Finland.


Pichani hapo wenyeji wakiwahudumia wageni wao Fc bongo vibawa viwili viwili vya kuku na vipande viwili vya viazi na kachumbari kiidoooooooooooogo.

Na picha ingine hapo inaonyesha kocha wa Tampere GEORGE (Wenger) MATOVU akiwaelekeza wachezaji wake fomesheni ya kuwafunga FC BONGO.

Magoli ya ya FC Bongo yalifungwa na BOB 1, EDO 1, na DUDU hatrick 3.

Goli la TAMPERE lilikuwa la penati waliopewa na refa iliofungwa na ELVIS.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. Vizuri mmewafunga midomo, manake kila siku wanaikandia fc bongo na kumlaumu michuzi kwa kuweka picha za fc bongo tu haweki za wapinzani wao, leo michuzi kaweka picha zao na kocha wao joji matovu akiwachuza wachezaji wake, eti fomesheni ya kuwafunga fc bongo, imenimaliza sana hiyo.

    ReplyDelete
  2. MMhm Bongo FC hamwishi kulalama na hasa linapokuja suala la menu... Well nawapa Hongera TAS kwa kuandaa menu maridadi kabisa ambayo imefunika menu iliyotolewa na Bongo FC mapema mwezi wa sita waliposhindiliwa bila huruma bao 3-1

    ReplyDelete
  3. Bongo fc hao kwa mpunga ndio wenyewe, hawakosi ndizi mifukoni kwenye hitima.

    ReplyDelete
  4. Mmh sio kwamba tunalalamika maswala ya msosi..kama ulikuwa mdogo tusiseme?lol..
    mimi na mtaka sana huyo Edwin Ndaki nione comment yake maana alivyokuwa anaongea kabla ya game si mchezo..nashangaa amekaa kimya..na bado tunawasubiri summer ijayo tutwafunga 10-0 mkome ubishi..
    Fc Bongo Oyee.........

    ReplyDelete
  5. Duh! Eddo ndio ulikuwa kipa? ebwana goli mbona nyingi?

    ReplyDelete
  6. Tatizo leno nyie fc bongo huwa mnakuja wengi ndio maana mnaambulia pilau bila nyama au vibawa vya kuku.
    Next time njooni wachache tu mtashiba.

    ReplyDelete
  7. Tangu lini soka likafundishwa/kuelekezwa kama basketball? Dar huyu kocha ana clipboard bin daftari.Hata hao kina Wenger,SAF,Mourinho etc hawatumii hivi vitu.Ebana hii sijawahi kuiona.

    ReplyDelete
  8. Edwin Ndaki kala kona, goli tano nyingi na simu kafunga, Ndaki is not richebo.

    ReplyDelete
  9. Huyo kocha wenu joji matovu hafai.
    Fomesheni gani hiyo anakupeni mkalambwa goli tano?.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...