nampongeza sana christian ronaldo kwa kuchaguliwa mwanasoka bora wa mwaka 2008 wa huko nanihii aliko (hawezi kuwa wa dunia, kwani sie mbona hatukushurikishwa katika kuchagua). ila tatizo huyu dogo chenga nyiiiingi na anao anao sana....
-michuzi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 20 mpaka sasa

  1. Hapo ambassador umewachokoza hao jamaa. Siku walipoifunga Chelsea uwanja wa fisi kinywaji hakikutosha.

    ReplyDelete
  2. Wacha wivu.Unaposema sisi una maana Tanzania.Tanzani ilishiriki kupitia kwa kocha Maximo na nahodha Henry Joseph.Wacha kukurupuka kwa wivu usiokuwa kuwa na maana na kutojua utratibu wa kuchagua mchezaji bora ambaye huwa nachagiliwa na makocha na manahodha wa timu za Taifa zilizo wanachama wa FIFA.Ukweli utabaki pale pale kwamba CR7 ni mchezaji bora wa Dunia 2008.Nataraji ujumbe umefika.Nawasilisha.

    ReplyDelete
  3. Mtu mzima naona unaondoa lawama!!
    Love Him OR Hate him (CR7) 4ever

    ReplyDelete
  4. Hahaha kaka umenifurahusha sana unasifia alafu unauwa kwa wakati mmoja...ila ukweli unabaki palepale yeye ndio mchezaji bora sio gerrard...lol

    ReplyDelete
  5. Ila huyu dogo mpira anaupiga siyo siri.Niliwahi kuona akipiga cross moja, aliipiga kwa kupitisha mguu wa kulia nyuma ya mguu wa kushoto na karibu na kibendera cha kona hadi golini,sikumbuki ilikuwa mechi gani ya league lakini msimu uliopita.duh.

    ReplyDelete
  6. NDIO,OKEY,TUNAKUBALI DOGO NI HATARI JAMANI.
    LIGI KUU,UEFA CHAMPION,CLUB WORLD CUP JE HAVITOSHI KUMPA DOGO SUPPORT JINSI ALIVYONG'AA? MNADHANI KAMA BONGO WATU KUKURUPUKA BILA VIGEZO!!!!!!TEHE TEHE MAN U FOREVER.MASTER P HAPA

    ReplyDelete
  7. michuzi wacha chuki hata kama ukisemaje ndio ashakuwa utajiju na wivu wako.....

    ReplyDelete
  8. Mdau naona vitu kama hivi ndio vinafanya soka la bongo lidumae
    yani mtu ameonyesha kipaji bado hamtaki
    kweli moja ni wa moja tu...
    anastaili waliokaa na kumchangua huyo sio viihiyo...
    watu na taaluma zao
    habari ndio hiyo....mdau london

    ReplyDelete
  9. We jamaa sijui uchokozi utaacha lini.Inaonekana enzi za primary school ulikuwa unasubiriwa nje ya geti la shule ili uchapwe.Alafu mbaya zaidi ushamuambukiza na Viriyala.
    Em tulia bana!

    ReplyDelete
  10. Kaka Muchuzi usimind sana, Ila ndio kama hivyo SIKIO halizidi kichwa kama ni mchezaji bora wa dunia haibadiliki!

    ni sawa na kusema mkubwa mkubwa tu hata hata kama utaota ndevu ukweli unabaki palepale amekuzidi umri. haha haha inabidi ukubali matokeo!

    Amani iwepo! hahaah ahahaha hahhahah!

    ReplyDelete
  11. Michuzi kijana anastahili kwa Tuzo zote alizopata sio hii kubwa tuu.
    Mwaka jana aliwafunika wengi ila mwaka huu iko wazi kuwa tuzo itaangukia kwa MESSI,goli 20 katika mechi 22 na bado yawezekana wakazoa makombe Spain huko.
    Vyombo vya Habari bongo ndio vinarudisha maendeleo ya soka bongo.
    Timu ikishinda yawote,ikifungwa utasikia mara ya maximo mara wasindikizaji,mara kichwa cha mwenda wazimu,sasa kweli mtu katoa jasho kwa uwezo wote halafu anarudi kukutanan na vichwa vya habari kama hivyo na Kipofu kaona mwezi,inakuwaje???
    Ni mtazamo tuuu Michuzi

    ReplyDelete
  12. The kid deserve it.

    ReplyDelete
  13. sizitaki mbichi hizo,kwani ronaldo anapata nini humo ambacho wewe kinakufanya uweweseke kaka? ingekuwa mweu yeyote yule kutoka bwawa la maini kungekuwa hapakaliki



    Mbega mweupe

    ReplyDelete
  14. Duh umenifurahisha sana unaposema, anao anao sana, unanikumbusha watangazaji wetu kipindi kile tunakusanyika kijiweni kusikiliza mpira sio kuangalia!!! Enzi za kina Jongo,Sekioni na wengine!!

    ReplyDelete
  15. Hiyo anaoanao unayoiona haifai ndio iliyomfanya achakuguliwe na hayo mashuti ya Gerald aliyopiga Mango garden na maDj ndio yaliyomkosesha hata kusogea kwenda uswizi,,je unalo ama tukuongeze?

    ReplyDelete
  16. ACHA TABIA YA USENENE MKUU!!KUWA MKWELI!!MDAU MIDLAND UK

    ReplyDelete
  17. haha, mtani wa jadi si ukubali tu bwana; hivi tukisema leo tuwape Ronaldo bwawa la maini si mtakufa kwa kiwewe!! Wote mnajua kila timu inatamani dogo angekuwa wao.

    anao, anao siku hizi kaacha; ilikuwa ni mwanzo tu alipokuja. Anapopiga chenga ni chenga za kufungua ngome na kutafuta nafasi ya kufunga au kutoa pande

    ReplyDelete
  18. mimi ninachotaka kukwambia misupu wacha usenene sio unapinga kila kitu

    ReplyDelete
  19. Wabongo kwa ushabiki bwana hamjambo huyu Jamaa ni mchezaji mzuri lakini mie sijaona maajabu yoyote aliyoyafanya ukilinganisha na wachezaji wenzake waliowai kuchukua tuzo hizo...ni mchezaji wa kawaida ukilinganisha na wachezaji kama Ronaldo ,Raul, Zidane, Berkham ,Shevu ,Ronalidino Gaucho , Luis Figo ,Alexndra Depiero ,Paul Maldin ,hao ni baadhi ya wachezaji ambao hasipokuwepo kwenye timu unaona pengo ,au kuwepo kwenye timu kunabadili mfumo mzima wa mchezo hao ndiyo lakini huyu jamaa bado mdogo alafu ameisha anza mambo ya u -bishoo mpira utamshida sasa hivi kama hamuamini after two years tukutane hapa kama huyu jamaa tutaweza kumwongerea tena.....star gani alishindwa kuonekana euro 2008 hao niliowataja juu enzi zao ingawaje wangine bado ni tishio hata leo walikuwa wachezaji (in capital letters). Mchezaji kama Raul sijuhi mtamwongereaje mtu aliyeongoza kwa ufungaji wa magoli mengi katika historia ya ligi champion tangu ianzishwe... siyo mtu kaupiga msimu miwili basi watu oooho jamaa mkali... mwache acheza misimu mitatu tuona..
    Mdau wa KAMACHUMU

    ReplyDelete
  20. This comment has been removed by the author.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...