meneja wa taifa stars leopard tasso mukebezi (bluu) na kocha msaidizi wa stars ali bushiri wakibadilishana mawazo huku wachezaji na kocha maximo wakipumzika baada ya tizi kali jioni hii uwanja wa kumbukumbu ya karume, dar. waliokaa toka shoto ni kipa farouk na mussa hassan mgosi. anayeruka samasoti ni kipa deogratius bonaventura 'dida. usiku huu maximo atatangaza rasmi kikosi cha wachezaji 22 ambao wataondoka ijumaa alfajiri kuelekea ivory coast kwa michuano ya CHAN

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. Ni kichapo 2 na hao magolikipa feki Haki ya mung mtaona

    ReplyDelete
  2. YAP!
    HAYO NDIYO WATANZANIA WAPENDA KANDANDA TULIYOKUWA TUNAYASUBIRI KWA HAMU. BILA SHAKA JUHUDI ZA VIONGOZI WA SERIKALI KUWEKA MIKAKATI KATIKA MCHEZO WA SOKA HUKO NCHINI ZAANZA KUZAA MATUNDA, TUNA KILA SABABU YA MATUMAINI KUWA VIJANA WETU WATAANZA KUNG'ARA KISOKA KATIKA NCHI KUBWA KUBWA INSHAALLAH.
    TUMEANZA KULITANGAZA JINA LETU, MAMBO MSWANO KABISA.
    KUNA WAKATI TULIKUWA MSTARI MMOJA NA WANAIJERIA, WAGHANA NA WENGINEO WA AFRIKA MAGHARIBI, LAKINI KUTANGULIA SI KUFIKA, JK BOYS YA SASA SI MCHEZO, TUNAANZA KUTISHA!
    VIJANA NAKUTAKIENI SAFARI YA MAFANIKIO, TUTAFATILIA KWA MAKINI MASHINDANO HAYO KUTOKA HUKU TULIKO, NA TUTAPEPERUSHA BENDERA ZA TZ KILA MTAKAPOKUWA DIMBANI.
    MUNGU AWABARIKI NA KUWAPA NGUVU
    Mndengereko, Ukerewe

    ReplyDelete
  3. nakummbuka wakati tunafunga safari ya kwenda burundi na U-17 watu tulikuwa tunaita hiyo kitu albadili.kila la heri taifa starz

    ReplyDelete
  4. wadau...habari za sasa

    asa we mdau hapo juu...kukatisha tamaa watu ndo maana yake nini??kama wewe umesha give up hope kwa timu yetu tuipendayo ya taifa stars basi we kaaaa kimya...sisi wajinga wajinga ambao tunaendelea kui support wacha tui support...unatovunja morali...UNABOA

    Mdau from Obama

    ReplyDelete
  5. nilicho kuwa na maanisha kipindi kile niko u-17 yani serengeti boyz hicho kitu cha majina it waz known as albadili na sijakata tamaa na timu yetu

    ReplyDelete
  6. Michuzi,kuna kituo kimoja kinatangaza kwamba kitairusha michuano hiyo live kwenye luninga lakini hakituelezi kama kitarusha mechi zote au zile zinazohusu Tanzania na wala hakitangazi kitairusha saa ngapi.Halafu hakina hata website wananchi tukaangalia ratiba.Pili,jana kuna gazeti moja la kiswahili la michezo limeandika mchezo wa stars na senegal utachezwa saa 9 alasiri saa za TZ.Uwongo,mechi ya stars na Senegal itakuwa 1900hrs za Abijan ambayo itakuwa saa kama 4 usiku huku nadhani.Vurugu tupu.

    ReplyDelete
  7. ama kweli wakati sio kitu cha kuchezea namkumbuka ali bushiri alipokuwa tanzania one alikuwa anaidakia timu ya malindi kule zanzibar mpaka hii leo sijaona kipa kama huyu jamaa,nadhani wadau wengi mtaungana na mimi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...