hasheem akiwa na majonzi baada ya gemu 

pamoja na kufungwa hasheem alionesha mchezo baaabkubwa

hasheem baada ya gemu

Mkuu wa nanihii, pamoja na UConn kutolewa kwenye nusu fainali kwa kufungwa vikapu 82 - 73 na Michigan state University, kijana wetu mpendwa alionyesha kiwango kizuri kwa kuongoza kwenye timu yake kwa vikapu 17 na blocks 2. 
Pole mdogo wetu, usikonde ndio game.  
Kusoma story yote
Mdau Piruu

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 36 mpaka sasa

  1. Haya mtu wenu huyo keshashindwa, sasa kelele ziishe, na bado Mashaka.

    ReplyDelete
  2. poa haikuwa bahati , uskonde tunakukubali unatisha mtu wetu

    ReplyDelete
  3. Inshallah Mazuri yatakuja tumuombee mbele azidi kungara popote atapokuwa, MAMA yake Mzazi jana pia alikuwepo Sijui na Dada yake pembeni Asikate Tamaa zidi kumuomba Mola wako atazidi kukupa na kukuzidishia mazuri tupo na wewe kwenye muda kama huu. Pazi.

    ReplyDelete
  4. Anon wa kwanza, Kushindwa ni moja ya matokeo mchezoni, waswahili wanasema asiyekubali kushindwa si mshindani. sasa wewe kinakuuma nini watu wakimpa moyo Hasheem?? Mashaka anahusika nini na post hii? Kama wewe hujui unafanya nini maishani, usilaumu watu na kukandia bila mpango. Juangalie mwenyewe umefanya nini cha maana maishani mwako,Kaa chini fikiria Chuki ulizonazo kwa watu wasiokujua Zitakusaidi nini au zitakupeleka wapi? Mwisho wa siku ni wewe ndio utakae pata vidonda vya tumbo kwa mawazo na hasira, utapata mfadhaiko wa akili na matatizo chungu mzima ya kisaikolojia na uwachukiao hawajui wala hawajali unawapenda au unawachukia... Huwalishi huwavishi,na ukifa wakisikia watakuja kukuzika na kukuombea dua kwakuwa hawakujua ni jinsi gani una roho ya zaidi ya mnyama...
    Mungu Akuongoze wewe na wenye mitazamo kama yako.

    Mdau UK.

    ReplyDelete
  5. Duh Jamaa ana mguu balaaa......Mzee wa wa nanihii hiyo size ya kiatu ni namba ngapi???? Na wataalamu wa pwani husema ulefu wa kiatu ni sawa na urefu wa mjengo.....kaazi kweli kweli.

    ReplyDelete
  6. MDAU WA KWANZA SIO LAZIMA KUTU HAKIKISHIA KWAMBA WEWE NI MPUMBAVU WAKATI UNAJIJUA NI MPUMBAVU.HASHEEM NA MASHAKA WOTE WANA MAISHA YAO.KUFUNGWA KWA UCONN SIO MWISHO WA HASHEEM YEYE ATAENDELEA NA KIPAJI CHAKE POPOTE ANAPOTAKA KWENDA.SASA WEWE KAMA UNAONA KUTOFANIKIWA KWA HASHEEM NDIO FURAHA YAKO ENDELEA NAYO.
    WABONGO BWANA KAPEWA KAZI MUINDI WHITE HOUSE WAMEMRUKIA MSWAHILI WA KWANZA WHITE HOUSE SASA MWEUSI MWENZAO ANATAFUTA MAISHA NA KUWAKILISHA NCHI YAKE WANAMUONA HADUI..

    ReplyDelete
  7. Haya sasa mahater mpate la kuongea sasa... najua mtakuwa mlikuwa mnalingojea hili kwa hamu!! Anyways Hasheem BIg UP!! Do You guys know how many kids in the USA wants to play on the Final Four Game? Do you know how many Tanzanins besides Hasheem will ever get the chance to play in it? Ya people just don't how it is like to get to that point. May be one day your sons will get there and so u can know how it feels. I been here in the US for 22 and I have seen enough of basketball but never heard of the media talkin about Tanzania as much as they did these past three years just because of Thabeet. So all of ya haters i can't wait to see your son playing division one basketball. I bet Thabeet's mom got to be proud!!

    Mungu Ibariki Afrika
    Mungu Mbariki Thabeet
    Mungu Ibariki Tanzania!!

    ReplyDelete
  8. Pole sana Hasheem lakini ndio hali ya mchezo.
    Japo UConn walifungwa katika hii mechi lakini Hasheem aliipeperusha vema bendera ya Tz. Kila la heri na endelea kuwa balozi mzuri wa taifa. Utawafungulia milango na wadogo zako ukiendelea kufanya vema.

    ReplyDelete
  9. FIFA inakataza timu yoyote kutumia nembo za taifa kama bendera au wimbo wa taifa kwenye mechi ambazo si za kitaifa kama klabu kwa sababu kwenye klabu kunaweza kuwa na wachezaji ambao siyo wa nchi husika. Ningependa kujua NCCA nao wana msimamo gani? Kwa nini Hashim anaweka anavyaa bendera ya Marekani wakati yeye siyo Mmarekani au mwenzetu mambo ya makaratasi yamekaa sawa?

    ReplyDelete
  10. Hasheem alicheza vizuri sana jana. I think ilikuwa moja ya best perfomance yake kwenye hii tournament.

    Game iliwakataa sana UCONN guards AJ Price na Kemba Walker. Jamaa hata free throw na 3 points walikua wanakosa. Game zilizopita walikuwa wana make all these easy shots.

    Anyway, Hasheem ana future nzuri sana. Jamaa amecheza organized basketball kwa miaka michache na angalia alivyopandisha kiwango. Ana potential kuwa center mzuri sana NBA.

    Naona hata jana watangazaji walikuwa wanamsifikia alivyo mwepesi ku move. Wanasema soccer background imemsaidia sana. Ma center wengi NBA sio wepesi kama Hasheem.

    Sasa tusubiri next step. Kila la kheri Hasheem. Umetuwakilisha wa-Tanzania vizuri sana.

    GG

    ReplyDelete
  11. namuunga mkono huyo anony wa kwanza ndo keshashindwa sasa wapambe na vigroupie mtulizane maana ilishakua taaabu holaaaa!!!

    ReplyDelete
  12. Piruu, OmanApril 05, 2009

    Mdau Uk nakuunga mkono ndugu, huyo anon wa kwanza anaonekana ni limbukeni. Mtu anawakilisha taifa letu, hadi JK anamtambua halafu wewe unataka bifu nae, acha upuuzi kijana!
    Mungu ibariki Afrika
    Mungu ibariki Tanzania
    Mungu mbariki Hasheem Thabeet

    ReplyDelete
  13. The UConn players walked slowly off the court, looking shell-shocked that their season had ended.

    "I've got a lot of kids in there crying right now," Calhoun said. "But they had a great season. It hasn't been that easy to stay focused the past few weeks. But I give (Izzo) a great deal of credit."

    This was expected to be a battle of big men. UConn's Thabeet had been a one-man swat team, averaging a double-double and winning defensive player of the year in the burly Big East for a second straight year. Michigan State's Goran Suton led the equally gritty Big Ten in rebounding and had averaged a double-double in the NCAA tournament.

    But the matchup never developed, with neither a factor. Izzo had said all week the Spartans planned to make the game a sprint to keep Thabeet out of his comfort zone.

    "That's one thing we've been doing since Day 1: We just rebounded and we ran," Lucas said.

    And Thabeet couldn't keep up. He led the Huskies with 17 points and six rebounds, but it was the quietest 17 points anyone's ever had. The 7-foot-3 center looked gassed from the opening tipoff, leaning over, tugging on his shorts and gasping for air not even six minutes into the game.

    The most aggressive he got was at the end of the first half, getting in Marquise Gray's face after Jeff Adrien and Travis Walton got tangled up under Connecticut's basket. There was some pushing and shoving, prompting Calhoun to come all the way from the other end of the floor to calm his players. But the dust-up fizzled quickly, and no technicals were even called.

    Suton, who had the main job of corralling Thabeet, didn't score his first field goal until early in the second half and finished with four points and seven boards.

    ReplyDelete
  14. I Just Want To Know. What Is Next For The Young Man? Kuna Mchezo wa KUtafuta Mshindi wa Tatu? Baada ya Michuano hii Kisha Kunafuata nini??

    ReplyDelete
  15. Kinachofata kwa hasheem ni Draft 2009 NBA. Inshallah.

    ReplyDelete
  16. Hakuna cha mshindi wa tatu. Next step ni NBA au abaki shule. Most likely he will turn pro.Bora aende NBA akatengenezea pesa. He is ready!

    Mnaweza kusoma article bomba about Hasheem Thabeet.

    LIFE OF REILLY

    Hasheem Thabeet is a long, tall, shot-blocking machine with an NBA future. But that's not why he can't stop smiling.

    http://sports.espn.go.com/espnmag/story?id=4032725

    GG

    ReplyDelete
  17. FIFA haina uhusiano na NCAA,you should know that.
    Pia kama unafuatilia UEFA champions league,jezi za timu za Spain zina bendera ya Spain,jaribu kuangalia kwa makini Jumanne na Jumatano.
    Sasa sina uhakika umeipata wapi hiyoi nukuu yako.

    ReplyDelete
  18. oh no ....niliangalia kidogo walivyokua wametie....jamani I feel so bad...Nilikua nazania kesho ni kesho kumbe ni Michigani sijui na timu gani vile...masikini mama yake walimwonyesha katoka bongo just to watch the game......Si yuko senior mwaka kwesho tena hiyo tunakuombea Mungu tu

    ReplyDelete
  19. It is quite unacceptable to make comparison between huyu kijana (Thabeet) na Mashaka... America ina population ya around 300 million. Huyu Mashaka ana ka-first degree tu ambako hakana mpango wowote katika ulimwengu huu wa credit crunch, maana hata watu wenye PhD's ama wengine ambao wako more experienced and intelligent than Mashaka nao wanapigwa chini kila siku uko makazini. Huyu bwana mdogo Thabeet ana heshima ya mpaka kufikia kutambulishwa he's from Dar es salaam Tanzania mwanzoni mwa gemu kubwa kama lile la jana.. So, kumlinganisha yeye na Mashaka ni sawasawa na kumlinganisha Lebron James na rookie yeyote ambaye hajawahi pangwa game lolote mzimu huu wa NBA.

    Ushauri wa bure kwa kijana Thabeet: Jana nilikua naangalia game kwenye club iliokua na mtu zaidi ya 300 zikiangalia hilo game. Kila mtu alisifia kwamba kijana Thabeet ana potential kubwa ILA anapaswa ku-work on his jump-shots.. This is his major weakness. Kama anataka kufikia level ya akina Nowitzki basi anapaswa ku-spend more time at the gym ku-work on his jumpshots.. Ile jumpshot aliyoikosa kama dakika 7 zikiwa zimebakia kwa kweli ingemfanya aonekane mtu wa maana zaidi kama angeipata. Work on jumpshots bro na utakua star in the future...

    Nakumbushia tena; It is quite wrong kulinganisha maharagwe na Nyama choma. Mashaka is NOTHING na hapaswi kutafuta masifa kwa nguvu. Anapaswa ku-work harder na mambo yatamnyookea, na sio kutumia blog ya Michuzi kujitafutia umaarufu (cheap publicity)

    ReplyDelete
  20. Kinachofuatia kwa Thabeet ni ama kurudi shule kumalizia mwaka wa nne na kuchukua shahada yake au kujitosa NBA. Usajili wa NBA una sura ya kijamaa sana. Timu iliyokuwa mbovu kuliko zote katika msimu uliotangulia inapewa nafasi ya kuchagua mchezaji kwanza. Halafu kila timu inapewa nafasi ya kuchukua mchezaji hivyo hivyo mpaka wachezaji waliopo sokoni waishe. Inaaminika kwamba Thabeet ataitwa katika raundi ya kwanza (dau linakuwa juu zaidi na anapata mkataba wa muda mrefu zaidi). Kama akirudi shule na wenzie wakarudi basi wana uwezekano mkubwa wa kuchukua ubingwa wa michuano hii mwakani. Kama akijitosa NBA baada ya mwaka atakuwa na hela kama Chenge, tena za kwake mwenyewe za kihalali.
    Vyovyote atakavyoamua, kila la heri!!

    ReplyDelete
  21. Wabongo bwana!! Ili kuonyesha kuwa wanajiamini kwa kitu wanachoongea lazima waingize lugha ngeni kidogo. Ona sasa April 05, 2009 11:50 PM. Hakuna mtu aliyesama kuwa FIFA ina uhusiano na NCCA ingawa ukisoma rules nyingi za NCCA soccer zinalingana na za FIFA na hivi karibuni wamebadilisha nyingine ambazo zilizokuwa hazilingani na za FIFA.
    FIFA ulikuwa mfano wa chama ambacho kinakataza vilabu kuingiza utaifa wakati kuna wachezaji ambao siyo wa taifa hilo. Timu ya taifa ya SPAIN haikatazwi na FIFA kuvaa nembo ya bendera ya timu ya taifa kama mataifa mengi yanavyofanya.
    Pamoja na utafiti wangu wote, tofauti na NBA, NCAA wanavaa nembo ya bendera ya marekani upande wa kushoto hiyo inamaanisha nini hata kama siyo raia wa Marekani? Hilo ndilo swali langu la msingi. Je, NCAA inawalazimsha au ni aina mojawapo wa mtindo. Kama hujui ni heri ukae kimya.

    ReplyDelete
  22. Duh!!! Anonymous wa kwanza kikorosho kweli kweli. Kumbuka kwamba washindanapo wawili moja lazima ashindwe. Ndio siri ya michezo.

    ReplyDelete
  23. wanapokwaruzana wawili lazima mmoja ashinde... jana haikuwa zamu yao Thabeet na Uconn.....

    ReplyDelete
  24. One more year of College basketball, then maybe he will be ready for the NBA! Pole zake.

    ReplyDelete
  25. We annony wakwanza unamanisha nini kwamba mtu wenu huyo, ni mtanzania mwenzetu ndio na inafurahisha kumuona badala ya kuona mataifa mengine tu ndio yenye kutoa wachezaji wazuri....."Yes we can".
    Subiri NBA draft then aje kwenye state yako yenye timu ovyo..

    ReplyDelete
  26. kweli hashimee kama anavyo jiita amevuka sen'genge kwa rasilimali yake ya urefu lakini nasisi waswahili tumezidi kwa domo kijana mbona wa kawaida sana jana niliiona hiyo mechi kuna vija wa green walikuwa mwimba sana ukianangalia uwezo wa mchezaji mmoja mmoja kiwanjani dogo wetu amepinga hatuwa sikatai ila si kwa kiwanga kama tunavomnadi kabla ya ya jana ohh ataiongongoza unncon, tegemeo la unncon na zogo jiingi kwa kweli ni bahati lakini ukimlinganisha na dulla huyu tunayemfahamu aliyetesa sana kill dula mwarabu basi dullah kwa kiwango angestahili kuchezea green anafanana nao sana tu

    ReplyDelete
  27. HASHEEM INGIA KWENYE DRAFT NA I'M SURE UNAINGIA KWENYE DRAFT. LEVEL ULIYOIWAKILISHA TANZANIA NA AFRIKA KWENYE COLLEGE BASKETBALL HAINA MFANO KWA MIAKA MITATU ILIYOPITA.AGAIN DECLARE YOURSELF WEWE NI TOP 5 PICK MOST LIKELY UTAKUWA NI SECOND PICK OVERALL NA UNAJUA HICHO,UTAPATA MILIONI ZAKO NA UKITAKA KURUDI SHULE UTAJILIPIA MWENYEWE.

    ReplyDelete
  28. sikutegemea kama kuna mtanzania yeyote atakuja na negative coments hapa i personal i proud of this boy manake mke hapa nilipo watu wananiuliza wewe nchini kweni ni spoti ya aina gani mnacheza manake sija ona hapa mbongo mmoja ktk spoti na wewe yani mimi ninapenda sana kuangalia spoti lakini siku hii ktk local pub yangu nikawaomba waweke espn mambo yakawa hivi ktk kutajwa majina ya wachezaji nakumbuka alikuepo janki mmoja toka kwa wapopo watu wakasema eeeh kuna muafrika pale punde si punde likaja jina la thabeet from Dar es salaam Tanzania lol kila mtu ananiangalia mimi sasa mambo kama haya ndugu zangu amnaolete uchawi wakusema mtu wenu keshatolewa we shoga au vp kabla huja kunya hatharani fikiria kwanza kijana huyu dogo mie simfagilii lakini na mpe 5 kwa achivimenti aliofikia tunapenda socer tunasapoti club za ulaya hata siku moja hujasikia mbongo anacheza timu mojawapo maarufu huyu dogo katuweka ktk ramani ya ulimwengu na mungu atamsaidia Dogo big up achana na maneno ya mashoga we keep focus

    ReplyDelete
  29. kama watanzaniamgekuwa mnamuombea dua kwa wingi basi ingesaidia hata kwa mungu lakini nyinyi kila siku ilikuwa ni kumsifia tu sifa kem kem hilo kama tunavyoelewa majisivu na majivuna yakiwa mengi hutokea mitihani fulani sasakijana amepata mtihani any way mimi binafsi namuombea mchezo ufuatao awe ndio nyota peke yake nitamsifu atakapo nyakuwa ushindi sio sasa kwa sasa namuombea ushindi

    ReplyDelete
  30. ...The BIG difference here ni kuwa DULLA bado anasota mechi za mchangani na Kijana wetu yuko US of A na watu wanakubali kazi zake na ndio maana yupo hapo alipo. Hiyo kwamba kwenye mechi ya jana sijui juzi kwamba ulimuona ni wa kawaida tu, hayo ni maoni yako. Hata akina Larry Bird, Dikembe Mutombo na wengineo nao kulikuwa na siku wanaamka wapo wapo tu! Tupende Chetu, Mkuu.

    ReplyDelete
  31. Mtanzania mwenzetu jamani, tubadilike - tupende vyetu! Kila la kheri Hasheem Thabeet...!

    ReplyDelete
  32. ...wewe hater wa 7:52 AM seems ni wivu tuu au kutoelewa game,hivi wataalam wote wa kikapu waliompa Hasheem thabeet Big East player of the year na defensive player of the year bila kusahau ni all first American team (wako watano tuu marekani) yaani achievemnet zote hizo huzioni? au unataka kusema kapendelewa mpaka ukafikia hatua ya kumlinganisha na Dulla mtu ambaye bado anasota kwenye gemu za vumbi maana waswahili hamkawii kusema hivyo...kwa taarifa yako thabeet ataingia NBA, na ni projected top five na haitaji support yako.wewe endelea na kutoa maneno yako ya uzushi tuu lakini watu wanasonga mbele,yaani roho mbaya tena kwa mbongo mwenzenu sijui zitawafikisha wapi?hasheem ni one of the best B/baller kwa sasa katika NCAA ndio maana pia alikuwa ni finalist wa NAISMITH award iliyochukuliwa na Blake Griffin juzi,subiri mwenzako by Nov atakuwa NBA na millions of contracts huku wewe na wivu na roho mbaya na uzushi wako sijui utakuwa wapi unaliwa na mbu au kupigwa baridi Alaska!

    ReplyDelete
  33. weweee bababesi unaelewa lakini huoni ndio tukasema ni bahati tu lakini kwa uchezaji hasa katika mechi ya juzi dogo alikuwa ni wakawaida mmno haku na zile sifa tulizikuwa tukimnadi kabla maana tulivokuwa tukimnadi ni kama copy ya kina jordan

    ReplyDelete
  34. Mdau kuhusu vilabu na bendera za mataifa,(FIFA,NCAA)nimekuelewa vizuri.
    Sikutumia kiingereza kuonyesha uhakiki wa point yangu,ni kama vile ninavyoongea kiswahili nikaingiza neno la kisukuma.Naamini ningefanya hivyo wala usingelalama.
    Niliposema timu za Spain,nilimaanisha vilabu.Jaribu ku-google real madrid vs liverpool uone picha au angalia link hii
    http://www.zimbio.com/Live+Sport+TV+Links/articles/9566/live+Liverpool+vs+Real+Madrid+online+streaming
    Kuhusu nchi nyingene sijawahi ona na sijui msimamo wa NCAA.
    Sam.

    ReplyDelete
  35. D YA MEAN HE ONLY MANAGES TWO BLOCKS WHILE HE PLAYS IN CENTRAL POSITION? WELL THAT'S POOR PERFOMANCE FROM HIM!

    ReplyDelete
  36. Misifa tu, jamaa kaona bado hana bog hits kwa Balozi, sasa anatuletea na kademu ili tumfagilie zaidi wakati tunajua paper ni muhimu nchi za watu. Awadanganye wajinga wajinga, sisi tumesoma huko huku na tumetulia, hatudanganyiki na uchawi.
    Subiri tu, utaambiwa jamaa anaoa ili wasimnyonge immigration ya Marekani.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...