Reginald Mengi
UVUMI ULIOZAGAA JIJINI DAR HIVI SASA KWAMBA MWENYEKITI WA IPP REGINALD ABRAHAM MENGI AMEKIMBIZWA HOSPITALI YA AGA KHAN JIJINI DAR LEO SI ZA KWELI, GLOBU YA JAMII INAWEZA KUTHIBITISHA.
RIPOTA MCHUNGUZI WA GLOBU YA JAMII AMBAYE ALIINGIA KILA KONA KUTAKA KUJUA UKWELI WA MAMBO ILI KUTHIBITISHA UVUMI HUO AMEGUNDUA KWAMBA BW. MENGI AMETOKA SAFARI YA NDANI MCHANA HUU NA AMEKUWA OFISINI MUDA WOTE.
HADI TUNAANDIKA HABARI HII GLOBU YA JAMII ILIKUWA IMEPOKEA SIMU 18 (SABA KUTOKA NJE YA NCHI) KUULIZIA KAMA MKASA HUO NI WA KWELI AU LA.
HALI ILIKUWA HIVI HIVI MIDA KAMA HII JANA WAKATI UVUMI ULISAMBAA KWAMBA MH. ROSTAM AZIZ AMEANGUKA GHAFLA NA KUKIMBIZWA AGA KHAN KWA MATIBABU. GLOBU YA JAMII ILIFUATILIA NA KUKUTA HOLLA!

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 23 mpaka sasa

  1. Kweli Rostam amedhamilia kufa na Mengi, kwani habari zilikuwa Rostam kuanguka na kukimbizwa Aga Khan.. Baadaye zikalipizwa kuwa na Mengi naye alianguka.
    Za awali zilikuwa Rostam ni Papa wa Ufisadi.. Then akazigeuza kuwa Mengi naye ni Nyangumi wa Ufisadi.
    Hii ni ile tuliyoambiwa Mwizi anakuibia kisha anakutimua wewe mwenyewe kwa mayowe ya mwizi, mwizi.. Kaaazi kweli kweli:)))

    ReplyDelete
  2. Naona kuna watu wamekosa kazi za kufanya na kuishia kuanzisha uvumi usiokuwa na msingi wala kuleta tija.
    Shukrani Mkuu kwa kurekebisha hali hiyo.
    Mdau
    Faustine
    http://drfaustine.blogspot.com/

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 06, 2009

    Ee Mungu isaidie Tanzania isiingie kwenye vurugu. Tujalie Amani na Upendo.
    Amina.

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 06, 2009

    mengi hamuwezi rostam; anaadhirika sasa;

    kumbe pesa zote za wizi ; halafu anajifanya kutoa misaada;

    hana hata senti moja madeni mimi afadhali ;

    unamfaa nini umaarufu wakati madeni mpaka pua

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 06, 2009

    Huyu Mengi lazima aekwe ndani afanyiwe upelelezi, sababu tuuma za ufsadi zinazo mkabili nikubwa, fisadi ni fisadi awe Muhindi, Mangi wote mafisadi

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 06, 2009

    hebu na wewe Michuzi tuletee mambo ya maana manake nakuona ushakuwa msela wa kijiweni sasa, kwani hata wakilazwa inatusaidia au kutuondolea nini sisi?ushaniudhi

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 06, 2009

    Mengi kidume, wadosi wote wanamhara sasa. Rostam kaishia kuongea uongo wa waziwazi. Hajawahi kutokea mswahili kama Mengi.

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 07, 2009

    Mengi kweli kidume. Mengi hajawahi kutuhumiwa kuhusu wizi wala ukwepaji kodi ila huyu Rostam ameona yeye kafichuliwa lazima nae aseme chochote ili mradi ngoma iwe droo. Hata hivyo Mengi kupitia mawakili wake kaweka nyaraka zote wazi zinazothibitisha kuwa analipa kodi. Sasa kama ni feki basi Rostam alete hizo genuine zinazoonesha kuwa Mengi halipi kodi.

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 07, 2009

    Au ni pressure? Maana naona Rostam kamchana kweli Mengi!

    Mengi achana na siasa! Endelea kula kivyako na hakuna atakae ku mind. Siasa waachie malofa.

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 07, 2009

    fatilia baaba fatilia hujua bahati yako imeangukia wapi. kama ungekuwa na kasi hii kwa wlalahoi wa mbagala, ungeambulia jike ukapata wajukuu lakini kwa mtaji huu wa EPA,hukosi kiwese baba cha kukusogeza kibaruani. akufaaye leo utamfaa kesho, m'bayone mwana wa m'bayonike

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 07, 2009

    Kama ni mashindano ya debate basi Mengi kamroast Rostam by far hands down. Kwa sababu kapangua hoja zote za Rostam isipokuwa ya ile habari ya kumuuzia kiwanja Fida Huseein ambayo wala so hoja nzito kwa sababu yeye ni mfanya biashara ambaye hana ugomvi na wahindi. If anything hoja ya Rostam kuwa Mengi hapendi wahindi imekuwa crashed hapo.

    Hoja nyingine ni kuhusu kunyanyasa wafanyakazi wake. Hiyo ndiyo hakuijibu japokuwa it is quite trivial.

    Sasa mbele ya macho ya jamii Mengi ameosha sana jina lake. Waulize walemavu, waulize watoto yatima, waulize VICOBA kule Kahama na SIngida, waulize wahanga wa Mbagala. Sasa tuje kwa Rostam kaifanyia nini jamii? Hakuna labda CCM kwa maana ya viongozi wake wachache. Labda.. Kwa hiyo kisiasa Mengi ameosha jina lake. Kama kuna anaebisha aseme.

    ReplyDelete
  12. AnonymousMay 07, 2009

    We anon wa 12.55 Rostam kamchana Mengi? Wa kwenda ICU Agakhan ni Rostam na wenzie and not Mengi my friend. Wewe vipi?

    ReplyDelete
  13. AnonymousMay 07, 2009

    mengi kidumeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee

    ReplyDelete
  14. AnonymousMay 07, 2009

    mengi tupo pamoja mkubwa

    ReplyDelete
  15. AnonymousMay 07, 2009

    Lakini nahisi kama hapo kaka Michuzi umejikoroga vile??!! Habari ulizozungumzia za Bw. Mengi kukimbizwa Aga Khan then Unatuambiwa teana MH. Rostam Aziz ameanguka..Sijaelewa...Inamaana wote walizushiwa kukimbizwa Aga Khan? Nahisi umekoroga

    ReplyDelete
  16. AnonymousMay 07, 2009

    Huyu Rostam anaweza kuwa keshamwendea Mengi kwa babu kumkorogea mavitu...Sina imani nae kbsa

    ReplyDelete
  17. AnonymousMay 07, 2009

    Michuzi
    Habari za Mengi na Rostam sasa zafika High Court na mabilioni ya fidia na 'kuombwa msamaha ktk magazeti kibao' ikiwa ktk kesi hiyo: nenda link ya www.thisday.co.tz

    ReplyDelete
  18. AnonymousMay 07, 2009

    Maskini kaka Michuzi...yani umeenda hadi Aga Khan??!! Pole sana kwa kuhangaika.....Ukicheza na wazushi wa bongo wanaweza kukuzeesha...hawana muamana...pengine hata wewe walishakuzushia hujijui tuu

    ReplyDelete
  19. AnonymousMay 07, 2009

    Hapa sasa ni ushabiki, wa `Mengi' kwa upande mmoja na Rostam kwa upande mwingine, wasiwasi wangu ni kuwa `wapiganapo mafahali ziumiazo ni nyasi'. Watu wengine wameshaanza kunyosheana vidole, kwanini unamtetea huyu, na vitu kama vile. Tuwe makini kwa hili, kwani wenzetu wana malengo yao!
    M3

    ReplyDelete
  20. AnonymousMay 07, 2009

    Kwenye hii Sakata Mengi ameibuka kidedea maanake ndivyo biashara inavyofanywa mahali popote duniani kwa kukopa. Hakuna ubaya wowote hapo. Halafu mambo yakiharibika wanakwenda na bancruptcy. So huo ni mchezo unaokubalika.
    Lakini sasa kuwa na mabilioni bila hata kumiliki kampuni yameingia tu kwenye account ndio hayo yanyofikiriwa kuwa ya Kigoda.

    ReplyDelete
  21. AnonymousMay 07, 2009

    Nyie mnaosema mengi fisadi hamna lolote!!mengi tajiri oka mtoto,familia yao wote wana hela..na kama mnavyojua achagga akili mkichwa toka wakiwa tumboni

    ReplyDelete
  22. AnonymousMay 08, 2009

    huyu nani lakini ? au anajiona ana nini ?

    ReplyDelete
  23. Mengi is guilty of not paying debts and in time everyone knows that but those Indians rostam and the like are milking the economy by their anti morals behaviours such as bribery of politicians and key figures and lack of True patriotism for the country by investing outside the country and importing counterfeit goods.You decide who is evil now!!

    Mdau
    aka USA-1

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...