viongozi mbalimbali wakila kiapo cha utii wakati walipkuwa JKT enzi za mwalimu ambapo jeshi la kujenga taifa ilikuwa ni wajibu wa kila mtu jambo ambalo linasemekana lilisaidia mno kujenga nidhamu, umoja na uzalendo na kutoendekeza matabaka ya aina yoyote ile

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 17 mpaka sasa

  1. matokeo ya stars vs uganda vipi???

    ReplyDelete
  2. Kama unahisi ni vizuri watu wote kulazimishwa kuwa wanajeshi, nenda tuu kajiunge mara nyingi wanakuwa wanahitaji majeshi wa ziada....

    Huu ujamaa wa Nyerere ndio jambo ambalo limenifanya nimchukue huyu babu.Hana jema hata moja alotufanyia watanzania badala ya kutuzonga na ushabiki wake wa kijamaa...tulikuwa watanzania tunakufa njaa na utawala wa Nyerere, mumshukuru sana Mzee Rukhsa kwa kuja kubadilisha sera za nchi!

    ReplyDelete
  3. Nina wasi wasi na utimamu wa akili za we mrfrosty hapo juu........kama hauna cho ku-comment cio lazima uandike. Sawa?? Kama vipi kakojoe ukalale, tuachie nyerere wetu na sera zetu.


    k'dume

    ReplyDelete
  4. Mi niliambiwa zamani watu wenye vitambi, walikuwa hawaqualify kuajiliwa jeshini, je huyu mwenzetu wa pili vipi?

    ReplyDelete
  5. Mshukuru sana yule Babu wewe, huna lolote la kumlaumu,

    ReplyDelete
  6. yani mrfroasty umenena mie kile kidingi huwa sikifagilagi kabsaaa mzee wa tukhusa adumuu

    ReplyDelete
  7. Sina uhakika kama hii ilikuwa JKT au lilipoanzishwa JESHI LA MGAMBO.

    Nakumbuka picha hii maana ni viongozi wa enzi hizo. Huyo mwenye kitambi ni Rashidi Kawawa na wa nne toka shoto ni Nyerere mwenyewe...

    ReplyDelete
  8. Anon wa 30:02:09:00
    Usiangalie kitambi
    Angalia uso
    Wakatabahu

    ReplyDelete
  9. Huyo wa pili ni mzee wetu Rashid Mfaume Kawawa aka simba wa vita

    ReplyDelete
  10. YULE MWALIMU ANGEKUWA HAI TENA RAISI KATIKA MILENIA HII NAJIULIZA ANGEWEZAJE KUTAWALA!!
    WATU WA SASA NI KICHWA NGUMU VIBAYA MNO, HATA ULIMWENGU WENYEWE UMEBADILIKA KABISA, SI RAHISI KUMWENDESHA BINADAMU NA KUMDHALILISHA KAMA ALIVOTUDHALILISHA.
    USHAHIDI NI KUPOROMOKA KWA SIASA ZA UJAMAA ZA RUSSIA, CHINA, YUGOSLAVIA NA CHEKOSLOVAKIA.
    NA LABDA NDOO MAANA ALISHTUKA AKAONA BORA ANG'ATUKE KABLA HAYAJAMGEUKIA ZAIDI.
    SISI TULIOONJA JOTO YA JIWE KIPINDI KILE TUKIKUMBUKA NI MASIKITIKO TU.
    TENA HAWA JKT WALITUNYANYASA SANA, WALIPEWA MADARAKA KULIKO HATA FBI. WALITUPORA SABUNI ZA KUNUKIA, PESA ZETU, SUKARI HATA VIGUO VYETU.
    AH, TZ ILE ILINUKA UMASKINI. SISI TULIOYAONJA NDIO HASA TUNAOFURAHIA UTAMU WA TZ MPYA.

    ReplyDelete
  11. JKT is a waste of time and money.

    Kwenda kufundishana matumizi ya gobole wakati watu sasa wanakwenda na laser ndio nini maana yake? Kulimisha watu kwa jembe la mkono badala ya kuhamashisha kilimo cha kisasa ndio nini?

    Munaweza kutupa ushahidi unaosema kwamba JKT inejenga nidhamu na kuondoa matabaka?

    Unataka kuniambia mafisadi wa nchi hii hawakupita JKT nawasiokuwa mafisadi wamepitia JKT?

    (US Blogger)

    ReplyDelete
  12. Mtoto wa CoastDecember 01, 2009

    Eti,
    "Hana jema hata moja alotufanyia watanzania..."

    basi wewe una baya moja unalojaribu kutufanyia Watanzania nalo ni hili:-

    KUOTA, KUFIKIRI NA KUANDIKA MAWAZO YAKO KWA NIABA YA WATANZANIA WOTE HATA KAMA WENGINE (MFANO MIMI NA FAMILIA YETU) HATUKUBALIANI NAWE NA WALA HATUJAKUTUMA KUTUWAKILISHA KATIKA HIYO KAULI YAKO.

    ReplyDelete
  13. we anan wa dec 01, 01:26 sema wewe ulionja joto la jiwe enzi za baba wa Taifa! usiseme sisi! sisi nani? Mimi kama mimi nilifaidika sana na Uongozi wa Baba wa Taifa, Watanzania ni kasumba yetu kutosifu au kukubali mema ambayo binadamu mwenzetu kayafanya! MUNGU AMLAZE MAHALA PEMA PEPONI. AMENI

    ReplyDelete
  14. Mbaf Kabisa,wewe haukumbuki Tanzania ilikuwa inaongoza kwa afya Africa?na shule ulikuwa unapewa mpaka madaftari bure?sasa ivi nani anakupa. Mbaf kabisa nyinyi,Nyelele alikuwa smart kuliko Presidents wote wa sasa

    ReplyDelete
  15. Wanaofagilia ujamaa ulioletwa na Nyerere, ni wanawe tuu na viongozi wengine waliokuwa wakila nguvu za wananchi kwa njia za kifisadi!

    Lakini wananchi wote, visiwani na bara walikula kisago heavy na utawala huu...no ubwabwaz hadi upange foleni, no bread on the table hadi upange foleni....hizo ndio sera za Nyerere, lkn inasemakana yeye kwake alikuwa na Sat TV!

    Apart from than,Tanzania is still suffering from Nyerere's Legacies for instance the creepy Union and others that he left behind that needs us to fix them!

    ReplyDelete
  16. alikuwa ni dikteta tuu sijui kwa nini hakufa miaka 30 nyuma tungekwa kama south hata ufisadi ungekuwa haupo simfagill ng'oooo kwa kipi??? umee barabara au maji safi???

    ReplyDelete
  17. acha upimbi hapo chini ati nyelele hiyo oblangata imefreez au?? wengine mnamfagilia tuu hata hamjui kitu bendera fata upepo kile kidingi na sera za ujamaa bin ulanguzi zilikuwa mbovu sana ati madaftari ya bure what about mchele sukari kwa foleni?? kwani tulikuwa wakimbizi hadi tupate mahitaji nyeti kwa foleni?? kwa hapo tu alichemsha sana simfagilii kabisa na kama hospitali ulitibiwa bure kwa kupewa klorokwini na sindano za ppf hata kirefu sijui ni ushuzz gani utajiju no body is perfect mzee alitokota sana tuu kinchi kimepaukaa dhiki full dhiki

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...