Kaka Michu hongera kwa kuendekeza opppsssss! sore kuendeleza libeneke!
Naomba nitumie nafasi hii kama si kuwasilisha kilio cha wengi basi kuna baadhi ambao watakuwa ni wa hanga wa hili.
Naomba nitumie nafasi hii kama si kuwasilisha kilio cha wengi basi kuna baadhi ambao watakuwa ni wa hanga wa hili.
Ni kuhusu hili suala la Polisi kutumia usafiri binafsi kwa ajili ya 'Ku-arrest' wanajamii. Swali la kujiuliza ni kwamba hizi TEKSI na BAJAJI huwa analipa nani? na hasa wakati wa usiku.
Imekuwa ni jambo la kawaida kwa polisi wa vituo vidogo kuacha lindo na kukodi ama Bajaj au Teksi na kuanza kupita katika hizi bar za mtaani na kutishia kubeba viti ama kuondoka na mwenye bar kwa kisingizio kuwa amechelewa kufunga Bar.
Hawa Polisi huja wakiwa wamevaa magwanda lakini huwa wanaficha namba zao, pia hawavai kofia, na pia huja na 'mapolisi uchwara' ambao huvalishwa yale masweta ya polisi ya baridi, na mwingine hupewa radio call ashike ili naye aonekane polisi. Kwa mfano tukio la jana kuna Polisi waliotumia Bajaj namba T391AZM ambapo baada ya kunyimwa UCHAKAVU hawa jamaa wakaiba viti na kuondoka navyo.
Baada ya purukushani za hapa na pale mwisho hawa 'wanausalama ' humwita mwenye Bar faragha na kumdai chochote. Na kama ikatokea raia akauliza swali kuwa imekuwaje wamekuja na Bajaji, utasakamwa kwa vitisho ikiwemo hata kutaka kupigwa. Meneja wa Bar alipowaomba namba zao ili ajue kama wao ni polisi kweli au 'MAGUMASHI' walikuja juu. Sasa kuna hatari ya wale walio na nguo zinazofanana na Polisi kuja kutufanyia uhalifu, kama Polisi mwenye mafunzo rasmi hataki kutoa ushirikiano unategemea nini?
Vituo vya Polisi vinavyoongoza kwa kudai 'UCHAKAVU' ni kwa Ali Maua (mwananyamala karibu na Mtogole) uchakavu wao huja kuudai Bar za kijitonyama huku wakijua kule kwa mtogole watu hawana kitu na Bar uchwara zinakesha kama kawa. Kituo kingine ni kile cha Kijitonyama Kisiwani.
sasa kwa mtindo huu kweli Polisi Jamii itafanikiwa ikiwa wananchi hao hao ndiyo wananyanyaswa. ? Ninachokiona mimi kuna siku kutatokea la kutokea kwani unapomdai mwenye Bar 100,000 wakati mtaji ni 500,000 unategemea nini kama si kumrudisha nyuma mtu anayepiga hatua.
Kwa Taarifa yao sasa tutaanza kuwaalika TAKUKURU waje kukaa nasi katika Bar wakiwa na hizo hela ambazo zinawafanya Polisi watoke vituoni na kuanza kuranda Bar. Naomba kuwasilisha.
Mwananchi
Mwananchi
kuanzia leo tukio lolote likitokea usichelewe kupiga picha kwa kutumia camera au sim yako ina kamera kwanini usitumie kupiga picha tuwaweke kwenye mablog ili wakome na waweze kuchukuliwa hatua tukiwa na ushahidi?fanyeni hivyo tutafanikiwa sana kwani sim kazi yake nini.
ReplyDeleteNa hao wenye Mabaa kwanini hawafuati sheria? Hatuwezi kuwa tunalalamika kuhusu uonezi wa polisi wakati sis wenyewe hatufuati sheria. Tulete hapa uonezi wa 'inocent people' kama hayo mambo ya fire extinguisher, wale matapeli wa parking nk. Nendeni night club kama mnataka kukesha, nasi twahitaji usingizi ati!! Kuwaleta takukuru, itabidi nao uwahonge. Halafu ulichowapa watagawana na tkkr. Kesho yake watakuja kukudai fidia...Kalaghabaho!!
ReplyDeleteHata wale wa pikipiki ndo mwisho!!!! Hawajawahi hata siku moja tukio la ujambazi, lakini kwa kushughulikia madili yenye "uchakavu" hakuna kipimo. Hayo ndo malengo waliyowekewa? Maana siamini kuwa wakuu wao hawajui haya kwa kuwa nao ni sehemu ya wananchi
ReplyDeleteHIVI HII SERIKALI NAHISI INATUONA SISI WANANCHI NI MAGARI MABOVU YA KUSUKUMA TU, HIVI WANAPOPIGA KELELE JUU YA RUSHWA WANA MAANA GANI AU WANAIMBA WIMBO AMBAO SISI TUNGEPENDA KUCHEZA, KWANI WANAJUWA HAWA MALOFA TUKIWAIMBIA WIMBO HUU BASI WATAJUWA KUWA SISI NI BONGO FLAVA BABU KUBWA, TATISA NI MKUU WA POLISI ANAWAONEA AIBU WATUMISHI WAKE KWA NINI HAWAKEI? NA HII RUSHWA IMEZIDI SANA ENZI HIZI ZA SAID MWEMA, NASHAWISHIKA KUSEMA ANAWATUMA WAPELEKE MAFUNGU KWAKE, NAYE YUPO OTHERWISE WE WANNA SEE YOU TAKING ACTIONS AGAINST THESE DESPICABLE THINGS, AND MORALLY CONTEMPTIBLE, TAFADHALI SAID MWEMA WE WANNA HEAR YOU ON THIS FOOLISH ACTS. SIKU TUTACHOKA TUTAANDAMANA BUNGENI NA KWA KIKWETE
ReplyDelete