Msaada tutani Ankal,
Ninashukuru sana Ankal kwa kuweza kutupatia habari moto moto kutoka nyumbani TZ na kwengineko duniani kupitia blog yetu ya jamii.
Mimi ni mdau kutoka U.S na ninataka kununua gari online kutoka Japan na kulituma nyumbani nimeshaona Kampuni kama AUTOREC,LUCUS JAPAN,AGASTA lakini kutokana na utapeli ulio online siku hizi nimeona bora nitafute ushauri na mapendekezo kutoka kwako na kwa wadauz juu ya kampuni au website ambayo wanaijua vizuri na kama wameshaitumia kuagiza maagari ili niweze kufanikisha zoezi hilo bila kuingizwa mjini au mkenge kama wanavyosema watoto wa mjini.
Asante sana Ankal;
mdau kutoka US.
Qsley.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 31 mpaka sasa

  1. Unaweza kununua kutoka Trust Company website yao ni www.japanesevehicles.com kwao hao nimeshanunua magari mawilikwa muda tofauti. Vile vile unaweza kununua kutoka www.japanvehicle.com wasiliana na Kenji (ni Mjapani anaongea Kiswahili, kutoka kwake nimeshanunua pia gari moja. Magari ya Kenji ni ya bei nafuu zaidi.

    ReplyDelete
  2. Mdau wa kwanza. Japanesevehicles walishawahi kuniletea magari mabovu mara mbili (nadhanik yanakaa sana kwenye yard)wala sina hamu nao. Nilijaribu kuwalalamikia lakini wakauchuna. Naona kama unataka uhakika nunua www.autorec.co.jp hawa jamaa ni uhakika mna magari yao ni mazuri sana pia isitoshe wana tawi Tanzania pale Lehman's Building. Japanesevehicle kwa ushauri wangu wana magari machakavu pamoja na kuongea kiswahili , kukuibia hawatakibia ila gari bovu utapata.
    Mzozaji

    ReplyDelete
  3. ibcjapan.co.jp hapo ni mwisho wa matatizo, mimi nimenunua magari matatu huko, rafiki zangu wamenunua magari mawili...ni uhakika na once hela yako iki-hit kwenye account yao wanakupigia simu!! magari yao ni quality ya hali ya juu...kila kitu nimefanya online!
    Semesozi

    ReplyDelete
  4. Utashauriwa mengi sana juu ya wapi ukanunue gari nzuri na nani anaaminika zaidi kuliko wengine. Chamsingi wewe usihangaike kabisa kununua gari kwa kampuni ambayo haina ofisi Dar maana hizo ndio zinaoongoza kwa kutuma magari mikweche yaliyokaa yard miaka 3 hadi 4. Wapo hao AUTOREC,SBT nk.

    Nzagamba

    ReplyDelete
  5. mdau AUTOREC is the best, you can not regret. Ila kama unataka kubahatisha kwa kuangalia unafuu wa bei waweza chukua sehemu nyingine. Mie nakushauri utumie AUTOREC wana magari mazuri hayajachoka na huyafanyia service kabla ya kuyasafirisha kwa wateja.Ila bei zao ziko juu kidogo nafikiri umeona hilo.

    ReplyDelete
  6. Tembelea www.gariyangu.com.

    Utapat A to Z ya kulinunua na kuliingiza gari lako bongo.

    ReplyDelete
  7. kweli autorec iko powa magari yao ni safi sana..

    ReplyDelete
  8. nilishawahi kununua gari kutoka kwenye hawa jamaa wakaweka gari mbili kwenye kontena moja, halafu jamaa wa gari ingine ni mzambia ilikuwa kazi sana, just nunua gari Tanzania utaepukana na mambo mengi ya kishenzi kutoka bandarini long room na tixt.

    ReplyDelete
  9. I too would recommend www.autorec.co.jp.I've done a few flawless deals with them. Good luck!

    ReplyDelete
  10. Mdau wa US.
    Nasikia autorec wamefunga tawi lao. Kama usemavyo ni kweli siku hizi Japan kuna kampuni za kitapeli unalipa hela halafu unaingia mkenge, aidha hupati gari kabisa au unapata gari lisilofanania thamani ya hela uliyotoa. Kwakweli mimi nimesha-deal na Lucus Japan nimenunua magari mengi sana kwao(zaidi ya 10), na isitoshe kwakuwa nipo nipo mitaa ya japan nilishakwenda hata ofisini kwao,Osaka, kwahiyo nawajua personally. Ukiangalia bei zao ni reasonable ukilinganisha na wengineo uliowataja hapo maana hao ni wakubwa kwa sasa hata overheads pia nikubwa so lazima wafidie hizo. Hawa tena siku hizi wana tawi Dar pale opposite shoppers plaza. Kwakifupi kazi yao nimeikubali zaidi.

    Asante
    Mpigabox Japan.

    ReplyDelete
  11. asanteni sana wadau kwa kujitokeza kwa moyo mmoja na kunipa ushauri ndugu yenu.mawazo yenu yamenipa mwanga sana tu.
    pamoja sana,
    mdau kutoka U.S
    Qsley.

    ReplyDelete
  12. Tatizo nililolipata AUTOREC, magari yao ni bei kubwa sana kwa sisi watu wa hali ya chini.

    Hivyo nilipata kampuni ndogo ya pale Japan kwenye mtandao wa Cartred view wakaniletea gari zuri kwa bei 3/4 ya bei waliyonipa Autorec.

    Tembelea huo mtandao utafanikisha tu.

    Jacqueline (K/Nyama)

    ReplyDelete
  13. Mdau wa US, hao uliowataja Autorec,Lucus Japan,ndo wenye uhakika na magari mazuri,sasa kwa nini tena utafute kwingine.Japanesevehicles wao wana cheap cars tu,kwa hiyo tegemea kushinda garage.

    ReplyDelete
  14. Lucus ni kiwango kila gari utapata kwa bei nzuri .

    ReplyDelete
  15. nunua kwenye yard za bongo kama unaogopa online

    ReplyDelete
  16. tuwasiliane,mie nipo japan ,ntakulete gari ya bei nzuri.

    ReplyDelete
  17. autorec famfa,walishawahi kuniletea kimeo,labda ujaribu Lucus,mshikaji wangu alipata gari nzuri kutoka kwao

    ReplyDelete
  18. Bwana Qsley hao watu wa makampuni yenye majina ni wasumbufu balaa. Nimeshasubiria gari langu miezi sita mpaka sasa hakuna cha Documents wala gari.

    Mpaka nilipomuomba jamaa yangu aliyeko pale Japan afuatilie hii kampuni, hapo ndo jamaa wakaaogopa na kuanza kutoa ushirikiano. Nakushauri kama unaye ndugu yako au mtanzania aliyeko pale Japan wasiliana naye ili aweze kukusaidia upate gari ulitakalo.

    ReplyDelete
  19. ndugu mie nilinunua Autorec miaka mitano iliyopita na mpaka wa leo gari bado ipo makini! Autorec walikuwa na tawi lao Dar lakini wamelifunga kwa muda (kwa mujibu wa wanavyosema wao wenyewe)

    Matata

    ReplyDelete
  20. JARIBU NA www.vwest.jp. HAO WANAMAGARI MAZURI MNO. YA UHAKIKA. ANGALIA KWENYE WEBSITE YAO, THEN UNAJISAJILI HALAFU WANAKUTUMIA STOCKLIST YAO.

    ReplyDelete
  21. Mdau chungulia hii naona imefanana na yako

    http://issamichuzi.blogspot.com/2010/02/libeneke-la-ushuru-wa-magari.html#comments

    ReplyDelete
  22. Ninaungana na mdau aliye wapendekeza autorec, ni kweli wanaaminika, na hata sisi tumeshawatumia sana kuagizia mabasi, ila tatizo ni moja tu, walituletea gari silo na tukaenda kwa agent wao hapa dar, wakasema wao kazi yao ni kuchukua order na pesa tu, mambo ya kubadilisha gari hawawezi. Ikalala kwetu tena. (kwa lugha nyingine, likija gari silo yaani umetaka automatic likaja manual ujue imelala kwako)

    ReplyDelete
  23. AUTOREC magara magari yao ni mapya.nimeshanunua magari kwao online na yako bomba mpaka leo.

    ReplyDelete
  24. Wewe unataka gari Nzuri ya Japan wasiliana na Huyu Bwana willy tel 255713404390 ofisi yake ipo Nkruma street Dsm utaletewa Gari Nzuri na ataiotoa yeye mwenyewe bandarini huna haya ya kusumbuliwa waambie ndugu zako Bongo waende hapo hakuna utapeli unapata gari unayoitaka na inafanyiwa inspection japan kabla haijaletwa na ikifeli hailetwi mpaka ipasi inspection kuna kampuni maalumu ndo kazi yake

    ReplyDelete
  25. Yes, AUTOREC is reliable although expensive.....BUT VERY SAFE AND RELIABLE......nimeshanunua gari 2 kwa nyakati tofauti....NO COMPLAINS

    ReplyDelete
  26. Tembelea, www.vwest.jp

    wasiliana na TAKASHI OGAWA na ndie mwenye kampuni hiyo ni mwaminifu na gari anakuletea mpaka bandarini Dar.

    ReplyDelete
  27. Autorec ni wazuri but too expensive, jamani kampuni za kijapani ziko hapa tz, mfano visit Nextagecars.com, mimi nanunua magari from August last year mpaka leo sijapata longolongo (nadeal na magari).
    Wamefungua tawi lao Haidery Plaza 1st floor, Bei zao ziko poa na unapata gari nzuri, Uhakika wa gari there is JAAI inspection kabla halijaja tz,linakaguliwa kwanza.

    ReplyDelete
  28. kwa kweli mimi nina Yadi ninauza magari hapa Dar....kuna mengine ya bei rahisi(famfa- kwa wanaopenda vitu vya bei rahisi) na mengine bei ya kiukweli but reasonable...lakini ili uwe na uhakika zaidi cheki na Kenase Japan wao ndio wananiletea magari ya uhakika kwa bei nzuri...

    ReplyDelete
  29. JAMANI NISAIDIENI ILE NAMBA YA PASSWORD KWENYE AUTOREC KWA AJILI YA WATEJA WA AFRICA.....USERNAME NAJUA NI AFRICA ONE....sasa ile password sijui nimezungusha zile namba yani imenitoka kabisa.....msaada wandugu

    ReplyDelete
  30. MDAU WA MAREKANI PIGA SIMU HAPA HAPA MAREKANI 215 207 4027, Ask for Prince Tony, or princek64@yahoo.com, ondokana na mawazo yoote hapo juu ingawa wote ni wa kweli lakini kila mmoja ame risk too much and u no more gonna gamble that much.NITAKUSAIDIA WEWE NA WENGINE WOTE MNAOTAKA MTACHAGUA MAGARI KWENYE TWO JAPANES USED CAR DEALERS WATAKUPELEKEA GARI CIF DAR AU MOMBASA UTALIKAGUA KAMA NDILO LAKO SAFI UNALIPIA PALE PALE PORT.

    ReplyDelete
  31. UKITAKA MAGARI JAPAN BILA KULIPA HADI UMELIONA PORT YA DAR AU MOMBASA PIGA SIMU HII-PHILADELPHIA -USA-215 207 4027 ASK Prince Tony- AU princek64@yahoo.com
    Tunasafiri kati ya USA-JAPAN WABONGO WOTE TUNAWASAIDIA HIVYO BORA UPO KAMA UPO SERIOUS KWANI WABONGO TUNAPENDA KUPANDISHA BENDERA KABLA YA USHINDI

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...