Afisa kanda wa PPF Temeke, Lindi na Mtwara Bi. Linda Njoolay akigawa sehemu ya msaaada kwa wagonjwa wa hospitali ya temeke. Kulia Dk. Asha Mahita, Mganga mkuu hospitali ya Temeke.
Meneja wa PPF kanda ya Temeke,Lindi na Mtwara Bi.Lulu Mengele (wa pili kulia)akikabidhi stakabadhi ya malipo ya mantanki ya maji kwa mganga mkuu wa wilaya ya Temeke Dk. Asha Mahita. Matanki hayo yatasaidia kutatua tatizo la maji hospitalini hapo hasa katika wodi ya kinamama na chumba cha upasuaji.Pembeni kulia ni Meneja wa mahusiano wa PPF Bi.Sarah Kibonde Msika. PPF imefungua kanda mpya wilayani Temeke ili kusogeza huduma karibu na wanachama wake
Wafanyakazi wa PPF wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa hospitali ya wilaya ya Temeke, baada ya kukabidhi msaada. Toka kulia ni Afisa wa Kanda ya Temeke, Lindi na Mtwara wa PPF Bi. Linda Njoolay, Meneja Uhusiano wa PPF Bi. Sarah Kibonde Msika, Meneja wa kanda ya Temeke, Lindi na Mtwara Bi.Lulu Mengele, Mganga .Mkuu wa wilaya ya Temeke Dk. Asha Mahita, Bi. Mary Msofe(watatu kushoto) Afisa uhusiano wa PPF na wafanyakazi wa hospitali ya wilaya



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. kweli PPF mmefanikiwa kuamka toka usingizini kazi kweli kweli, mfuko wenu ni mkongwe lakini haubadiliki ivi sasa suala la mafao litakuwa ushindani sana,huduma bora,mafao bora ndio yatakayo weza kuwapatia wanachama si siasa zisizo na tija,ujio wa SOCIAL SECURITY REGULATORY AUTHORITY kunamo NOVEMBER 2010 kutaleta changamoto kwenye mifuko ya pensheni apa nchini kwetu TANZANIA hasa hasa kwa PPF na wasiwasi kama mtaweza himili ushindani kwani mfumo wenu wa kukotoa mafao ni duni mkijiringanisha na mifuko mingine kama LAPF,PSPF na NSSF wanajitahidi kidogo nyie mnamnyonya mwanachama kwani haiwekani nyie mkalipa asilimia (30%)kama mafao ya mkupuo pindi mtu anapo staafu kisha asilimia (70%)ikalipwa taratibu mpaka mtu atakapofariki hii sio haki ndio maana serikali ya rais kikwete ikasikiliza kilio cha wananchi na kumleta regulator aje kuboresha upuuzi mnaoufanya, kwani investment mnazo na nyie ni wakongwe hela zetu mnazotukata mmepeleka wapi?????? au hamkuwa makini na kufanya investment bora mmejikuta mna watu wengi mnapashwa kuwalipa mafao ya kila mwezi na mzigo unazidi kuongezeka wakati wanachama wanaukuimbia mfuko wenu mbona NSSF ni mfuko wazamani na unajitahidi kulipa mafao vizuri pia LAPF ni wa zamani kwani ulianza mwaka 1944 kama PROVIDENT FUND na kisha kuwa PENSHION FUND mnamo mwako 2000 na unatoa mafao bora wenyewe na PSPF ulioanza mnamo miaka ya 90, mimi ni mstaafu wa CHUO KIKUU CHA SOKOINE (SUA) haiingii akilini kulipwa shilingi 17,000,000/= kama mafao ya mkupuo baada ya kuchangia mfuko wenu kwa takribani miaka 30, na mkanidanganya na PENSHENI ya kila mwezi ya shilingi laki tatu 300,000 kila mwezi wakati hapa nilipo na maradhi ya kisukari kutokana na umri wangu sitegemei kuishi miaka zaidi ya kumi kutokana na ukweli harisi wa nchi zetu masikini, kwanza nilikataa kuchukua hiyo hela kwani mngeweza kuniua kwa stroke ,statement ya michango nilioitoa hapo kwenu inasema jumla mpaka nastaafu kama PROFESA NIMECHANGIA SI CHINI YA MILIONI 5O,OOO,OOO/= nyie mnanipa milioni 17 hizi zingine mnapeleka wapi??????????????????? wizi mtupu serikali itupie macho kwenye hili kwani sisi mliokwisha tunyonga tumekubali yaishe lakini vijana wetu tunawashauri wajiunge na lAPF na PSPF ili pindi wanapostaafu mambo yao yawe mazuri kwani tayari bunge limeshapitisha sheria ya mwaka 2008,watu wako huru kuchangia mifuko mingine na si lazima kuchangia mfuko unaoharibu maisha ya mwanachama pindi anapostaafu badala ya kuyaboresha kwani kufanya ivyo ni sawa sawa na kumuua mwanachama..

    PROOF. MUKYANUZI
    CONSULTANT
    PKF (NAIROBI, KENYA)

    ReplyDelete
  2. Wasipotoa taabu, wakitoa taabu. Jamani sasa jema ni lipi? Huyo anayejiita professor ana jazba na tumshauri tu akachukue hiyo hela mil 17,000,000 yake aliyozira kuchukua. Ppf endeleeni kusaidia hospitali ziboreshe huduma kwa wagonjwa msikatishwe tamaa na hawa waliosoma enzi za nyerere.

    ReplyDelete
  3. WANADAMU HAMNA JEMA NYIE.WEWE MBANE MWAJIRI WAKO AKUONGEZE MSHAHARA ILI MICHANGO IWE MIKUBWA (Utavuna unacho panda),WEWE PROF WA TZ HUO MSAHARA WAKO WA LAKI 7 KILA MWEZI UNATAKA UKIJA KUSTAAFU ULIPWE MILIONI MIA 7 WAPI NA WAPI?
    NENENDI MKACHANGIE DECI.BORA UBAYA WA ULIYE MZOEA KULIKO UZURI WA UNAE MZANIA NENDENI HUKO DECI NINI LAPF

    ReplyDelete
  4. alafu wanadam kazi sana ,wanachama wanapofatwa kujiunga na hii mifuko wanakuwaga wabishi sana tafrani pale anapoacha/staafu anaifatilia hela kwenye mfuko utafikiri sio yule uliye kuwa unambembeleze kujiunga.sasa una shangaa /unajiuluiza hawa siwanakuwaga wabishi kujiunga leo anaifatilia kama sio yule aliyekuwa anabembelezwa kujiunga.HII NI AKIBA JAMANI ISHU NI KUWA NYIE MAPROFESA MLIPOKUWA VIJANA HAMKUANDAA MAISHA PPF/NSSF/LAPF N.K NI SEHEMU TU YA MAISHA CHANGA KARATA UKIWA KIJANA VINGINEVYO MTAINGILIA NDOA ZA WATOTO WENU OOO TOKA UMEOA HUSAIDII HOME

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...