Mgombea Mwenza wa urais kwa tiketi ya CCM,Dk. Mohamed Gharib Bilal, akiwahutubia wananchi wa Jimbo la Mtera, wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika jana
Mgombea Mwenza wa urais kwa tiketi ya CCM,Dk. Mohamed Gharib Bilal na mkewe Zakia Bilal, wakipunga mikono kuwaaga wananchi wa Jimbo la Kibakwe Wilaya ya Mpwapwa Mkoa wa Dodoma baada ya kumaliza mkutano wa kampeni uliofanyika jana eneo la Stendi ya Mabasi na kumnadi mgombea Ubunge wa Jimbo hilo George Simba Chawene.
Wananchi wa Kijiji cha Mloa Barabarani, Jimbo la Mtera, wakiwa na mabango wakati wakimsubiri Mgombea Mwenza Dk. Mohamed Gharib Bilal, kuingia eneo hilo kwa ajili ya kufanya mkutano wa kampeni jana,ikiwa ni pamoja na kumnadi mgombea Ubunge wa Jimbo hilo, Livingstone Joseph Lusinde, ambaye ni mrithi wa Malecela.

Bro Michuzi nasikia Dr Bilali kuna mahali last week or this week alikosa watu wa kuwahutubia kwenye mkutano wake. Hivi ilikuaje? mbona hutuhabarishi kuhusu hilo? Tuna hamu ya kujua nini chanzo.Msaada tutani tafadhali
ReplyDeleteMdau Mbezi Loius
hiyo picha ya mwisho sina mbavu
ReplyDeletePicha ya mwisho hao ndio wanaotambulisha "mtanzania wa kawaida". Shida kwao ni kama ukoo, pigia kura CCM wazidi kuwa na shida. Kama kumburuza mlevi vile.
ReplyDeleteCheck walivyo simama na mbango..then mtapata nini?
ReplyDeleteNina uhakika hapo kama hawajapewa buku buku tu, basi ubwabwa wa bure tu,
RIP Tsnzania
We anym wa kwnza mbona unambeep michuzi.
ReplyDeleteMichuzi hawezi toa hizo weweeee , humjui ankal ana damu ya kijani nini!
Hivi jamani Mhe. Balali mimi naona bora tu asingingia kwenye huu uchaguzi, umri wake umeenda sana jamani....angepumzika tu. Hata hivyo namtakia kila la heri ila tu namuonea huruma umri wake umeenda sana. Hivi CCM ni chama cha Wazee tu?
ReplyDeletembona jamaa wakati wote yuko FULL TINTED !? tutapataje hisia zake!? huyu bwana bila shaka hii post kaburuzwa tu, mwenyewe alikua napo anapotaka. Ankal nistiri hii moja tu uitoe basi ! au?
ReplyDeleteMzee wa Kengeja.