Elizabeth Gupta akiwa na mchumba wake Kevin Chuwang Pam
toka Abuja, Nigeria, ambaye ni mshindi wa Big Brother Africa 4 'The Revolution' ya mwaka 2009
. Huyu bwana kwa sasa ni shemeji yetu halali kwani tayari keshatoa mahari na ndoa inatarajiwa kufungwa hapa Dar wiki ijayo. Hivi tunavyoongea tayari keshawasili Dar katika maandalizi ya kumeremeta kwao...Mshindi wa Big Brother Africa mwaka 2009 Kevin Chuwang Pam akiwa na TID usiku huu katika hoteli ya Paradise City iliyomo katika jengo la Benjamin Mkapa jijini Dar. Huyu shemeji yetu ambaye wiki ijayo anatarajiwa kumeremeta na Elizabeth Gupta, mshiriki aliyeiwamkilisha Tanzania mwaka huo, ni Producer wa muziki na ana studio yake kubwa huko Abuja. TID amumualika Kevin kuwa mgeni maalumu katika uzinduzi wa albamu yake leo Jumanne katika ukumbi wa Billicanas. Kevin na Elizabeth pia wanatarajiwa kuwamo katika show mpya ya Angella Bondo Talk Show itayoshutiwa leo katika hoteli hiyo ya Paradise City ambayo hivi sasa iko chini ya mmiliki mpya.
Kevin akiwaonesha kazi zake zaa muziki TID, promota Ricky Bondo toka Italy, Chief Cameraman wa 2Eyes Production Adam Gire na Angella Bondo usiku huu wakati wa maandalizi ya harusi yake pamoja na kutokea katika Angella Bondo Talk Show itayoanza kurushwa January 2011. Ana mpango wa kuja kufunga kambi Bongo ila hayo yote amesema atayabainisha wakati wa talk show ya Angella Bondo...

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. this is crazy who is he any way to make a news ? thats is ridiculous

    ReplyDelete
  2. Kisaka, OysterbayDecember 28, 2010

    Yaani huyu jamaa anatuchukulia hivi hivi na sie watoto wa Oysterbay tuko hapa hapa???

    ReplyDelete
  3. Anony wa 10: 46: 00 kama humjui jamaa basi ni shemeji yako kama na wewe m-bongo, lakini ktk entertainment industry ya africa he is big news.... Sema jamaa yuko low profile hana makeke kama wengine... google hilo jina then utamjua ni nani.. Haters hamkosekani siku zote

    ReplyDelete
  4. We kisaka sijui kyasaka, nadhani akili zako hazina akili.

    ReplyDelete
  5. acheni maneno nyie, waombeeni heri wenzenu, NAWATAKIA KILA LA HERI LIZZY NA KEVIN, GOD WILL BLESS YOU ALL - THE - WAY!

    ReplyDelete
  6. i like this couple.post to us their wedding pics soon after their wedding plz.kwa wanaoijua vizuri show ya big brother wataipenda hii hasa kelvin.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...