

Sista akishukuru wana TPF kwa misaada
Watanzania wenzetu,
Tujenge tabia ya kujitolea kusaidia sehemu ya jamii iliosahauliwa. Jamii iliokuwa pembezoni. Jamii isiojumuishwa kikamilifu katika mipango rasmi ya nchi.Tukijivunia maisha Bora, basi angalau sehemu hii ya jamii nao wapate kidogo ya ubora huu.
TUSHIKAMANE PAMOJA FOUNDATION ni NGO iso ya kiserikali, ni ya kujitolea. Azma kuu ya kikundi hiki ni kutafuta misaada mbali mbali kama vile:
1. nguo, viatu, shuka, vifaa vya jikoni viliotumika (sio viliochakaa) au vipya za wakubwa na watoto wakiume na wakike
2. vifaa vya kulimia bustani ndogo ndogo za mboga
3.magodoro na vyandarua
4.vifaa vya shule kama vitabu, madaftari na kalamu
Vitu vyote hivi ni kwa ajili ya kuwapa wazee wasio na uwezo na wengine wamejikuta wakilea wajukuu ambao wazazi wametangulia mbele ya haki.
Tumegundua wazee wengi wanaishi katika mazingira magumu na duni sana. wazee wengine wapo katika vituo na wengine wako majumbani bila msaada wowote.
Kwa maelezo zaidi tafadhali tuwasiliane kupitia info@tushikamane.com
au piga simu +255752 224688
"Haba na haba hujaza kibaba"
Mdau
Msaaada kwa wazee ni muhimu sanaaaaaaaaaaaaaa! huo hauna kipingamizi..lakini mimi nalia na wale watoto yatima.Hawa watoto tunawasaidia ndio, lakini huwa hawana adabu. Mtoto alishafiwa na wazazi wake anajiona yeye ndie yeye, hataki kusemwa wala kuambiwa chochote kinachoweza kumjenga. Ndio maana siku hivi vituo vinakua vingi ni kwa sabb hawa wanetu hawaleleki. Ukimwambia hiki atakujibu: unasema kwa sabb mimi yatima... n.k hili neno yatima limewapa kiburi sana na wameishana kwao ni dili. Jamani tuwasaidie lakini tuwajenge kimaadili si misaada ya mali tu.
ReplyDelete