



MKOMBOZI MKOMBOZI! NDIZO SAUTI ZILIZOSIKIKAWAKATI Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige alipotembelea jamii ya wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu katika jimbo la uchaguzi la Msalala, ambalo yeye ni mbunge.
Waziri alitembelea eneo hilo kufuatia malalamiko ya wachimbaji hao wa Mwazimba, kudai hivi karibuni kuvamiwa na Askari Polisi na Maafisa wa BARRIC waliokuwa na silaha za moto na mabomu wakidai kwenda kuitekeleza opererasheni ya kufukia mashimo ya wachimbaji licha ya kuwepo kwa agizo la Mhe. Waziri wa Nishati na Madini, MHe. William Ngereja kutaka wachimbaji hao wasisumbuliwe katika eneo hilo.
aakihutubia wananchi hao jana, Maige alisema kuwa kuna watu wamefanya ndivyo sivyo kutokana na nguvu ya fedha ya kampuni ya BARRIC kuipoka haki ya wachimbaji wa Mwazimba na kumtaka Mhe. Ngereja kuchunguza watu wake.
Akihutubia wananchi hao Maige alisema, “Katika sakata hili sitegemei lugha tofauti, nitahakikisha kwa gharama yoyote nasema kwa uwazi hata kama utanigharimu, BARRIC hawaitakii mema serikali kwakuhangaisha wananchi wake wenye njaa, nami sitakata tama kupambana nao kwa gharama zozote, eneo hili ni halali yenu haki itendeke,” alisema Mhe. Maige.
tunahitaji viongozi kama hawa wanaosimama upande wa wananchi katika masuala ya msingi. kama eneo ni la wachimbaji wadodo wadogo iweje hawa barrick wanaingilia. endelea bwana mh maige umasikini hauji kwa kuwasikiliza wazungu ila kwa kufanya kazi kwa upendo wa taifa letu
ReplyDelete