Ankali habari ya kuendeleza libeneke. Jana jioni nilipita pale Ubungo  stand ya daladala na kutumia huduma ya choo cha kulipia  kilichopo pale na kupewa hiyo risiti, Nawapongeza hao TANROADS sijui sasa ni Ofisi ipi kwani hiyo risiti haina anuani,kwa kutoa risiti hii kidogo itawasaidia kudhibiti mapato, watoa huduma wengine kwenu ikoje??????


Mdau Ubungo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 16 mpaka sasa

  1. Huo ni Wizi wa Mchana saa 7 jua linawaka,,,hawa waganga njaa hapo Ubungo wakamatwe mara moja!

    ReplyDelete
  2. Huo ni Upigaji kwisha kazi,,,watu wanatolewa damu hapo hakuna TANROADS wala nini!

    ReplyDelete
  3. Kama ni hivyo Wakala wa Barabara atakuwa ameishiwa Sera, kujisaidia ni kianzo cha Mapato ya barabara?

    Kwenda haja Ndogo au Kubwa na Kuoga ni huduma ya Miundombinu?

    Bora kama ni hivyo tuvunje Mkataba Wajerumani wa Tanroads warudi kwao!

    ReplyDelete
  4. TANROADS huduma ya Choo na Bafu?
    Hii hata taahira humpati ng'o!
    Bora wangefyatua risiti za DECI !

    ReplyDelete
  5. Kwa mauzo wanayoyafanya waulizwe mashine na risiti za VAT!

    ReplyDelete
  6. Duh! hongera kwako kwa kupewa risiti. Mimi jana hiyohiyo jioni majira ya saa 12 nilitumia huduma hiyo hapohapo lakini sikupewa risiti. Labda kwakuwa sikuomba risiti. Hata watumiaji wengine pia sikuona wapewe risiti. Sikuwa nikifahamu kwamba kuna utaratibu wa risiti. Hata hivyo hilo siyo suluhisho la kudhibiti mapato. Njia pekee ni kuweka machine zinazopokea sarafu ili kumruhusu mtu kufungua mlango wa choo/bafu na siyo vijirisiti ambavyo vimekatwa nusu kama ulichokionesha hapa.

    Mdau

    ReplyDelete
  7. this is so feck, the government is feck. they are playing with us. this is BIG JOKE!

    ReplyDelete
  8. hivi zile risiti za serikali za rangi ya njano zimeishia wapi?

    au sikuhizi kila idara inatengeneza risiti zake ambazo za mafanikio ya kutunisha mfuko wa suruali?

    ReplyDelete
  9. Mdau wa Ubungo wala usiulize chochote maana huu ni WIZI wa moja kwa moja. Ukitaka kuamini jaribu kuchunguza mwanye hiyo tender.... mtoto/mke wa kigogo... Tanzania zaidi ya uijuavyo!

    ReplyDelete
  10. Tanroads kamwe haiwezi kuwa na miradi ya mkononi kama hii huduma ya choo na bafu!

    ReplyDelete
  11. ha ha ha ha ha!

    Kama TANROADS inaendesha huduma ya Vyoo na Mabafu ya kuogea na mimi lazima wanipe tenda ya kunyonya maji taka na kupakua kinyesi!

    ReplyDelete
  12. Haya ndio yale yale ya Tandale Uzuri mwaka 1993, bao limewekwa Uchochoroni likieleza ni ''Shamba la Mfano'' la 'IDARA YA MISITU YA WILAYA YA KINONDONI' kumbe pana shamba la Bangi!

    ReplyDelete
  13. WAAFRIKA BWANA HAWANA AKILI KABISA,SASA KWA MTINDO HUU HATA MIMI NITAIBA...TECHNOLOGY ZIMEGUNDULIWA KUTUMIWA..WAAFRIKA HAWAPENDI KABISA KUTUMIA TECHNOLOGY.ANGALIA KIGAMBONI PALE MASHINE ZA TICKET ZIPO ILA WATU BADO WANA AMUA KUTUMIA TICKET ZA KUANDIKA KWA MKONO...WIZI WIZI.AFRICA AMKA SASA OOOH

    ReplyDelete
  14. Ohhh Tanroads hawawezi kuwa na Risiti mbovu kama hizo!

    Risiti zimefyatuliwa kwa Wajanja Manzese, kazi inapigwa kwa Wajinga Stendi ya Mabasi Ubungo!

    Hao wapigaji wewe!

    ReplyDelete
  15. Sio rahisi Mamlaka kama Tanroads kushughulika na miradi ya 'Vinyesi',,,,

    Kama hao ni Tanroads wenyewe kwa aina hiyo ya Risiti kama tiketi za Mabasi ya Haisi kwenda Lugoba na Chalinze, uwezekano ni mkubwa kuwa mapato hayafiki kunakohusika!

    ReplyDelete
  16. Hiyo sio risita halal. Rialto zone Tanzania sass hive lazima ziti ewe na EFT (mashine za TRA). MAGUFULI uko wa wapiiiiiiiiiii?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...