Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 8 mpaka sasa

  1. Hahahahaha Kanumba kanifurahisha nimevaa Shati watu wanasema nimevaa Top TehTehTeh, KAKA KANUMBA MWENYEZIMUNGU INSHA-ALLAH ATAZIDI KUKUPA MUONGOZO TIZAMA ARNOLD NA JACKIE CHAIN WAPO WAPI? USIWASIKILIZE WABAYA ILA WAOMBEE NIMEPENDA MSG YAKO YA MWISHO, MAJID

    ReplyDelete
  2. Binafsi sio mtazamaji mzuri sana wa kazi za nyumbani na ukizingatia kwamba sasa niko US ila I would say Steven Kanumba ni TZ business icon, kwa pale sanaa ya bongo ilipofikia tu jamaa ametoa msaada mkubwa sana. Pindi kanumba yuko BBA nilikua bado bongo na nilipata kutazama, jamaa alifanya vyema sana ila cha ajabu watz hawakuthamini msaada wake na kama haitoshi wakaanza kumkandia. Jamaa kaumia i can tell that from vile kaongea na ukweli inauma ila usife moyo ndugu, siku TZ nzima itatambua mchango wako. GO FURTHER KANUMBA

    ReplyDelete
  3. Tatizo kubwa kwa Jamii ya Wabongo ni 'ENVIOUS JEALOUSY' yaani wivu usio na Tija.

    Mfano Joka la Mdimu linakaa juu ya mti wenye ndimu na kila anayetaka kuchuma linachachamaa linakuwa kaliii utafikiri lenyewe linakula hizo ndimu wakati sio chakula chake na halitaki wengine wachume na wale ndimu.

    Hii kitu inarudisha wengi nyuma, mfano angalia ktk hali ya kawaida unapopata mafanikio kidogo basi walio karibu yako wanageuka kuwa maadui!

    Pia ifahamike kuwa adui yako anapokuwa ni mtu anayekufahamu vizuri inakuwa ni vigumu kuchomoka hapo lazima atakulaza chali na akifanikiwa atafurahi sana ingawa kuanguka kwako au kuyumba kwako hakuna faida kwake bali yeye ataridhika kwa kufikia lengo lake chafu tu !

    ReplyDelete
  4. Slang ni lugha ya mtaani! sasa bwana kanumba unadhani watu walitaka uongee lugha ya mtaani ya Kiingereza kama wamarekani?
    Jamaa alijitahidi kuongea, kuna matatizo na lugha ya kiingereza kwa watanzania wengi, hata wale niliosoma nao shule ya msingi na walikua wanafanya vizuri, kwa sasa ni wahitimu wa vyuo vikuu na wapo Tanzania kiingereza chao kimeharibika, kwa jinsi ninavyokiona kwenye hizi tovuti kama facebook!

    ReplyDelete
  5. Kuongea kiingereza kwani ni lazima? hata ukiwa umesoma alimradi aweze kuelewa kilichoandikwa na kinachozungumzwa.

    Sisi kwa kujikomba kwa kiingereza! Mfano utaona latin americans ambao wamesoma kweli kweli na scientists wa kusifika akiongea kiingereza hata huelewi amekusudia nini. Na watu wanamthamini kwa mchango wake na sio lugha yake.

    Ila sisi ni lazima tujitweze.

    Kitu kimoja tu Kanumba ambacho nilinotice na ukifanyie kazi kwa maendeleo yako - utafute meneja anayejua mambo ya wardrobe (kabati na mavazi). Mdogo wangu shati la pinki aa a! pinki ni ya kike na ndiyo maana hao wakakwambia umevaa blouze.

    Ila jitihada kweli unaonyesha.

    ReplyDelete
  6. we are proud of you anyway,usijali kaka,wenye chuki wana mwisho,GODBLESS YOU,,I SUPPORT YOU

    ReplyDelete
  7. Kiengereza cha Marekani sio Kiengereza sema Pia kuna tofauti hujakatazwa kuwa na uengeaji wa Kiengereza WAJERUMANI WANAONGEA ILA KUNA UONGEAJI WAO UNAMJUWA HUYU MJERUMANI AU HUYU MFARANSA HAIKUKATAZWA TATIZO LINAKUJA UONGEAJI MBOVU WA SENTENSI KWENYE KIENGEREZA, ONGEA HATA KAMA UNAONGEA KIENGEREZA CHA NIGERIA ILA UTUMIE VIZURI, TATIZO LA WATOTO WENGI NIMETIZAMA TANZANIA WANAONGEA KIENGEREZA ILA WANATUMIA SLANG, AMBAYO NI KIENGEREZA KIBOVU KINA HARIBIKA KUTOKANA NA HAWATUMII MUDA WAO KUANDIKA AU KUONGEA INAVYOTAKIWA, WANATIZAMA SANA WAMAREKANI WA MTAANI NA MOVIE KAMA ILIVYO KISWAHILI KINAVYOHARIBIWA BILA MTU KUJALI NDIO FACEBOOK NA TWITTER KIENGEREZA WANAVYOHARIBU VIJANA. ILA KANUMBA ENDELEA KWENDA MBELE YAKO SASA HIVI MAFANIKIO WANAYAONA. MWAIPOPO

    ReplyDelete
  8. Jealousy and Envy is something that cause by terrirtory man...like my main man Biggie would've said. Jamaa kaumia sana hadi anataka kulia. Ndio, ukubwa huyo kaka kaza moyo.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...