WaziriMkuu, Mizengo Pinda akitoa maelezo kuhusu kifaa maalum kinachotumika kukamuwa asali kutoka kwenye masega wakati Wakuu wa Mikoa na Wilya pamoja na Makatibu Tawala wa Mikoa walipotembelea mradi wake wa ufugaji nyuki,eneola Zuzu Dodoma, May 29,2012.
Wakuu wa Mikoa na Wilaya pamoja na Makatibu Tawala wa Mikoa wakitembelea mradi wa ufugaji nyuki katika Shamba la Waziri Mkuu, Mizengo Pinda lililopo eneo la Zuzu Dodoma May 29,2012. Viongozi hao wako Dodoma kwa semina. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


mkulima wa tanzania huwezi kulima au kufuga alafu unaishi mkoa mwingine danganya toto hiyo na king`ora juu hicho siyo kilimo adivataiz
ReplyDeleteWastaafu hii ndio kazi sasa!
ReplyDeleteWala msikate tamaa ya maisha wala kufikiria Utajiri kwa njia ya Ufisadi!!!
Mmeitambua mbinu ya ya kuyakabili maisha baada ya kustaafu na kupata ushindi?
Ni ufugaji wa nyuki!!!!
waswahili hatuna dogo,akiiba na kununua nyumba ya usd 700 kwa cash,mnalalamika,akifuga nyuki mnasema danganya toto.mambo mengine ni ya kupongeza,si kila jambo kusemea vibaya.
ReplyDeletekufuga nyuki ni profession sawa na hizo nyengine. Vile vile kilimo na kufuga.
ReplyDeleteNi sahihi kabisa huwezi kufuga au kulima na huku una kazi nyengine hiyo ni danganya toto kama alivyosema huyo hapo juu.
Hakuna sustainability hapo tusidanganyane.
Viongozi hawa ndio wa kuigwa, wanaelewa kuwa maisha ya binadamu sio milele hapa duniani, hivyo kujilimbikizia mali kwa ajili ya yeye, vijukuu na vilembwe na kuacha wananchi wengine wakiteseka sio sahihi. Kazi zipo kama hizi za kujipatia kipato kihalali na maisha bado yanaenda vema. Unaweza ukawa mkulima hata USA na unaishi TZ maana kilimo sio lazima ufanye kila kitu mwenyewe unatoa ujira kwa wenzio nao wanafaidika.Big up Pinda and likes of you
ReplyDeleteMtoa maoni wa kwanza unashangaza sana.kwani kuwa mbali na maeneo yako ya kilimo ndo kuwa si mkulima?kazi nzima inaonekana shida yako nini?Kama angeonyesha majumba ya kifahari kuwa ni yake mngesema katuibia fisadi.Yaani watu hawana jema jamani du! Pongezeni jamani huo ni mfano wa kuigwa kwa watumishi wote.Hapo Pinda atakuwa ameajiri watu wengine ambao wanalisha na kusomesha watoto wao kwa mshahara waupatao hapo.
ReplyDelete