Mwakilishi wa Kuteuliwa na Rais Marina Joel Thomas akila kiapo mbele ya Spika wa Baraza hilo Pandu Amer Kificho huko katika Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Mbweni nje ya Mji wa Zanzibar.
Mwakilishi wa Kuteuliwa na Rais Marina Joel Thomas wakatikati akiwa katika picha ya pamoja na Familia yake nje ya Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi baada ya kuapishwa na Spika wa Baraza hilo Pandu Ameir Kificho. PICHA NA YUSSUF SIMAI-MAELEZO ZANZIBAR.
Uamsho kaeni macho, wanatumwa hao na kueneza ajenda zao za kanisa
ReplyDeleteWe mtoa maoni wa kwanza mbona unaleta udini?? Mi nilifikiri muamsho wanapinga muungano. Au wameanza na muungano halafu wakipata kisiwa chao watawabadilikia ndugu zao wasio swali pamoja?
ReplyDeletehuyo mchangiaji wa kwanza nadhani ni wakumwacha mana ni sawa na kumfukuza chizi uchi aliyechukua nguo zako wakati unaoga,ana matatizo yake huyo.
ReplyDeleterais unatuletea watu ambao hawajisitiri ktk bunge la watu wanaojisitiri?..Allah hu Akbaru...hata kama ni mkristo angalau angejisitiri kidogo..mambo gani haya jamani,,hii dunia inaelekea wapi..mimi ni mbara lakn kuna haja ya kutenga visiwa hivi vijitenge ili vilinde hadhi ya walio wengi wao..kujisitir ni jambo zuri, nani asiejua?
ReplyDeleteAssalam Alaykum,
ReplyDeleteNi ukweli usiopingika ya kuwa:
1.Kanisa la Kwanza Afrika ya Mashariki lipo Zanzibar.
2.Lilijengwa Kabla ya Uhuru wa Tanzania Bara.
3.Lipo kabla ya Mapinduzi ya Zanzibar.
4.Lipo kabla ya Muungano.
5.Ukristo Bara uliingia ukitokea Zanzibar ambako ndio Wamisionari walifikia kwa mara ya kwanza kwa vyombo vya majini hakukuwa na Ndege enzi hizo.
6.Hivyo kama mna akili nzuri ni lazima muelewe ya kuwa Wakristo pia ni sehemu yenu Wazanzibari.
Kwa hivyo ndugu zetu wa Zanzibari msituchukulie sisi wa Bara (tukiwemo Waislamu wenzenu) kuwa Bara na watu wa Bara ndio shina la Ukristo!!!
HAPO JUU ZINGATIENI HISTORIA!!!
WASSALAAM!
wewe mchangiaji wa kwanza ni mpumbavu kabisa inabidi wakuogope kama mtu mwenye ukoma
ReplyDeleteAssalam Alaykum,
ReplyDeleteAnonympous wa kwanza Tue Jun 19, 09:42:00 PM 2012
Ni muhimu uelewe pia ya kuwa Mtume Muhammad SAW aliishi na watu wengine achilia mbali watu wa Dini zingine wakiwemo Wayahudi ktk Makkah walikuwepo Manaswara na Mapagani wasio na Dini kabisaaa !!!
Sasa kama Zanzibar inajulikana ina kama zaidi ya 99% asilimia Waislamu, hiyo idadi Kiduchu chini ya 1% ya Wakristo hapo Zanzibari isiwe kigezo kwa nini wasitendewe haki na kupewa nafasi pia,,,hata kama kwa idadi wapo watatu (3) tu!
Hiyo ndiyo Demokrasia ya Usawa wa kibinaadamu ambayo hata katika Uislamu ipo aliyoitumia Nabii wetu Muhammad SAW ni kuwa unatakiwa uwe Muislamu unayeheshimu watu wa Imani zingine pia!