Pichani  mmoja wa wakazi wa mjini Mtwara akiwa amebeba magunia ya mkaa,akipeleka kujitafutia soko kama alivyonaswa na Camera ya Globu ya Jamii jioni ya leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Ingawa ni ukumu gumu Ukuzaji wa Kiuchumi kuwafikia watu.

    Njia hizi hapa chini zinaweza kutumika kama zilivyotumika ktk jamii zingine zilizopata rasiliami kama Mtawara ilivyopata Gas.

    1.Sovereign Wealth Funds:
    Inakuwa kama Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ama Mifuko ya Akiba za Mafao ya kustaafu, lakini hii inahusika na ukusanyaji wa Mapato ya rasilimali.

    2.Energy Hedge Funds:
    Ni mifuko ya Akiba inayoweka fedha kuendeleza Sekta ya Nishati na pia Mifuko hii inaunda Sera ya kufanya Nishati kuwa sehemu ya matumizi ktk mzunguko wa maisha ya kila mtu 'energy as domestic consumption' hivyo mutliprier effect zake zinaujenga mfuko zaidi na mafao yake yanaelekezwa kwa kila mwananchi kama Bonasi.

    3.Direct Cash Transfers:
    Hii sio njia nzuri sana, kwa kuwa inatakiwa kutumika kwa dharura sana mfano wakati wa maafa kama njaa ama Majanga asilia na pia kwa Makundi maalum ktk jamii kama Wazee, Wagonjwa, watoto na akina mama wasio na kipato cha uhakika ama Familia zenye mzazi mmoja,,,Isitumike kwa kundi la vijana kwa kuwa hufanya wawe wamebweteka na Nguvu kazi kudorora na kuathiri Uchumi wa jamii.

    Muda ufike angalau mtu kama huyu baada ya Kupokea Mafao ya Mfuko wa Jamii atumie Bajaj ama Toyo kubeba magunia.

    Ifanyike liwezekanalo kuhakikisha Rasilimali na Utajiri unawafikia watu kama hawa.!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...