Mpendwa wetu Lucas Makaya Mkandya.
Nimwaka mmoja wenye huzuni tangu ulipofariki dunia.
Masaa, siku, wiki, miezi na hatimaye leo mwaka mmoja, toka siku ile ulipotutoka tarehe 25-2-2015.
ulipotuacha kwa majonzi ya kutokuamini Kama kweli umeondoka, lakini kwetu ni kama jana tu maana Upendo na Busara zako kwetu bado upo nasi na utaendelea kuwa nasi milele kiroho.
Lucas Makaya Mkandya
unakumbukwa sana na Mke wako Mariam Mkandya, mwanao Alice Mkandya, Dada zako, wadogo zako na ndugu na jamaa wote.
Warumi 14:7-9.
Umeshinda kaka yetu! Bwana amekupa makao yaliyo bora sana! Ulipigana vita vya imani kwa amani sana! Wala hakuna siku ulipiga na kwa hila! Umemaliza mwendo! Siku zote uliwajali wanyonge! Bwana Yesu atukuke kwani wewe ni chuo kamili ktk maisha ya familia! Mauti yako ina thamani sana Mbele zake Aliyekupenda zaidi! Lala salama Baba
ReplyDelete