Na Leandra Gabriel, Blogu ya jami
PASIPOTI ya kieletroniki imezinduliwa leo na Idara ya uhamiaji Mkoa wa Dar es Salaam mara
baada ya kuzinduliwa na Rais mapema Januari mwaka huu.
Akizungumza katika uzinduzi huo kaimu Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam na Mkuu wa mkoa
wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo ameeleza pasipoti hiyo ina manufaa makubwa hasa
katika teknolojia, kukidhi viwango vya kimataifa na kufafanua ukiwa nayo unakuwa na
nakala ya pasipoti kwenye simu mara baada ya kupakuwa applicationi hiyo.
Mhandisi Ndikilo ameeleza gharama za kupata pasipoti hiyo ni Sh.150,000 na kueleza kuwa
pasipoti za kawaida zitaendelea kutumika hadi Januari 2020.
Aidha ametoa rai kwa wananchi hasa katika utunzaji wa pasipoti hizo ili zisiangukie kwa
wahalifu na gharama kwa pasipoti iliyopotea mara ya kwanza ni shilingi laki 5 na ikipotea
kwa mara ya pili italipiwa shilingi laki 7 na nusu.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema amewaomba wakazi wa mkoa wa Dar es
Salaam wachangamkie fursa hiyo, pia ametoa wito wa kada mbalimbali hasa
wafanyabiashara wadogo kupata pasipoti hizo ili kuweza kufanya biashara kwa uhuru na
kuvuka mipaka hii itawasaidia kutangaza biashara zao.
Ofisa Uhamiaji Mkoa wa Dar es Salaam Chrispin Ngonyani amehaidi kusimamia kazi hiyo
kwa uadilifu mkubwa na amewaomba wananchi kueleza changamoto wanazokumbana
nazo ili ziweze kutatuliwa mara moja.
Pia, Kamishina wa Uhamiaji, uraia na pasipoti Gerald Kahiga ameeleza kuwa pasipoti hizo
zinatolewa kwa raia wa Tanzania pekee na zikitolewa wazitunze kwa usalama wa hali ya juu
na wamejipanga na harufu yoyote ya rushwa katika utoaji wa pasipoti hizo na ametoa rai
kwa wananchi kutotumia mawakala kama daraja la kupata pasipoti hizo.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam Cathy Kamba amefurahishwa na uzinduzi huo
kwani hata katika ilani ya uchaguzi walisisitiza suala la ulinzi na usalama na amemshukuru
Rais kwa kuendelea kuboresha maisha ya watanzania.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...