UMEMSIKIA alichosema Shishy Baby ? Iko hivi leo bwana amemtolea uvivu msanii maarufu nchini Nasseb Abdull a.k.a Diamond kwa kumwambia ni vema akamuoa Zarinah Hassan a.k.a Boss Lady. 

Shishy amesema hayo leo kwenye viwanja vya Leaders jijini Dar es Salaam baada ya kutakiwa kusalimia wasanii na wageni waalikwa walioko viwanjani hapo. 

“Diamond naomba nikwambie hivi, binafsi natamani sana umuoe Zari…ni mwanamke anayejua kusuka mipango, ni mjasiriamali , ni mbunifu na anao uwezo mkubwa katika mambo ya ujasiriamali. 

“Wakati ule ulivyomuacha Wema na kwenda kwa Zari tukasema sio tatizo.Hivyo nitumie nafasi hiii kukuomba leo kuwa natama umuoe Zari maana huyu anakufaa sana,”amesema Shishy Baby. 

Hata hivyo Shishy Baby wakati anaeleza hayo Diamond alikuwa kimya akimsikiliza tu na baada ya kumaliza kuzungumza mshehereshaji wa shughuli hiyo alisema kuwa Shishy alikuwa anatania tu ili kufurahisha wageni waalikwa. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...