Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu kutoka Ofisi ya Bunge Ndugu Jane Kajiru akifungua mafunzo kwa makatibu wa waheshimiwa wabunge majimboni kwa ajili ya kujengewa uwezo wa kutekeleza majukumu yao.mafunzo hayo yametolewa na Ofisi ya Bunge chini ya mradi wa kulijengea Bunge Uwezo (LSP II) unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), kushoto kwake ni Mratibu wa Mradi wa LSP II Ndugu Mary Lasway.
Mtaalamu kutoa Chuo cha Utumishi wa Umma , Ndugu Dorah Chenyambuga akitoa mada kuhusu utunzaji wa nyaraka, uendeshaji wa ofisi, ufuatiliaji na tathimini kwa makatibu wa waheshimiwa wabunge majimboni. Mafunzo hayo yametolewa na Ofisi ya Bunge chini ya mradi wa kulijengea Bunge Uwezo (LSP II) unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).
Baadhi ya makatibu wa waheshimiwa wabunge majimboni wakipatiwa mafunzo ya kujengewa uwezo.mafunzo hayo yaliyofanyika katika Ofisi za Bunge Jijini Dodoma yametolewa na Ofisi ya Bunge chini ya mradi wa kulijengea Bunge Uwezo (LSP II) unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...