Na  Editha Edward -Tabora

Mvua Zinazoendelea Kunyesha nchini zimesababisha Mafuriko Kwa Wakazi Tabora wanaoishi katika mtaa wa Mwalitani (Freemason) Kata Ya mpera manispaa ya Tabora ambapo mvua hiyo imeanza kunyesha usiku wa kuamkia Leo ambapo imepelekea wakazi wa mtaa huo kushindwa kulala usiku kucha na nyumba zao kujaa maji

Jeshi la zima moto na uokoaji mkoa wa Tabora lilifika katika eneo hili na Kuanza kuwokoa baadhi ya watu walioshindwa kuvuka maji yaliyokuwa yamewazingira

Aidha Mkuu wa mkoa Agrrey Mwanri ambaye pia alifika katika tukio hilo usiku huo amewaomba wananchi waliopata maafa hayo wasirudi katika nyumba zao zilizojaa maji hadi pale oparesheni itakapokamilika.
PichaniJeshi la zimamoto na uokoaji wakiokoa wananchi ambao nyumba zao zimefurikwa na maji usiku wa kuamkia leo.
Nyumba zilizofikwa na mafuriko mtaa wa Mwalitani maarufu kama Freemason Kata ya mpera.
Pichani ni mtaa wa Mwalitani uliokumbwa na mafuriko
Mvua Zinazoendelea Kunyesha Nchini Zasababisha Mafuriko Kwa Wakazi Wa Tabora

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...