Wizara ya Kilimo imejipanga kuhakikisha mikoa mingi kujitosheleza kwa mafuta ya kula.
Kauli
 hiyo imetolewa leo Ijumaa mjini Kigoma na Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo 
Bw. Gerald Kusaya alipoongea na waandishi wa habari kuhusu ziara ya 
Waziri Mkuu . 
" Jitihada
 za Wizara hadi sasa tumeweza kuzalisha mbegu bora za michikichi 
1,556,111 ambapo miche 49,032 ipo tayari kwa ajili ya kupandwa kwenye 
Halmashauri sita za Mkoa wa Kigoma" , alisema Kusaya.
Katibu
 Mkuu huyo amesema Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa ( Mb) kesho Jumamosi
 anatarajia kufanya ziara ya kikazi ya siku moja mkoani Kigoma kwa lengo
 la kugawa miche bora ya michikichi kwa wakulima na vikundi vya AMCOS .
Aidha,Waziri
 Mkuu Majaliwa atazindua rasmi  zoezi la upandaji miche bora ya 
michikichi katika Gereza la Kwitanga na kambi ya JKT Bulombora.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...