Wizara ya Kilimo imejipanga kuhakikisha mikoa mingi kujitosheleza kwa mafuta ya kula.

Kauli hiyo imetolewa leo Ijumaa mjini Kigoma na Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bw. Gerald Kusaya alipoongea na waandishi wa habari kuhusu ziara ya Waziri Mkuu . 

" Jitihada za Wizara hadi sasa tumeweza kuzalisha mbegu bora za michikichi 1,556,111 ambapo miche 49,032 ipo tayari kwa ajili ya kupandwa kwenye Halmashauri sita za Mkoa wa Kigoma" , alisema Kusaya.

Katibu Mkuu huyo amesema Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa ( Mb) kesho Jumamosi anatarajia kufanya ziara ya kikazi ya siku moja mkoani Kigoma kwa lengo la kugawa miche bora ya michikichi kwa wakulima na vikundi vya AMCOS .

Aidha,Waziri Mkuu Majaliwa atazindua rasmi  zoezi la upandaji miche bora ya michikichi katika Gereza la Kwitanga na kambi ya JKT Bulombora.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...