Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Plc, Sitholizwe Mdlalose akizungumza na maofisa kutoka benki kuu ya Ethiopia (National Bank of Ethiopia) na kampuni ya simu za mkononi ya Safaricom Ethiopia namna huduma za kifedha kwa njia ya mtandao zinavyoleta tija kwa jamii na kuongeza pato la taifa kwa kufuata sheria na mamlaka husika za nchi. Ujumbe huo umekuja jijini Dar es salaam kwa lengo la kujifunza huduma jumuishi za kifedha kwa njia ya mtandao wa simu za mkononi.


Mkurugenzi wa Vodacom M-Pesa, Epimack Mbeteni akiwaelimisha maofisa kutoka benki kuu ya Ethiopia (National Bank of Ethiopia) na kampuni ya simu za mkononi ya Safaricom Ethiopia namna huduma za kifedha kwa njia ya mtandao zinavyoleta tija kwa jamii na kuongeza pato la taifa kwa kufuata sheria na mamlaka husika za nchi. Ujumbe huo umekuja jijini Dar es salaam kwa lengo la kujifunza huduma jumuishi za kifedha kwa njia ya mtandao wa simu za mkononi.


Meneja Uendeshaji kituo cha huduma kwa wateja Vodacom Tanzania, Deogratius Massawe akiwaelezea maofisa kutoka benki kuu ya Ethiopia (National Bank of Ethiopia) na kampuni ya simu za mkononi ya Safaricom Ethiopia namna kituo hicho kinavyofanya kazi za kuweka usalama na kutunza taarifa za wateja wao



Mkuu wa Mauzo Vodacom kanda ya Dar es Salaam na Pwani, Brigita Shirima akiwa kwenye kituo cha mafuta kwa ajili ya kuwaonesha maofisa kutoka benki kuu ya Ethiopia (National Bank of Ethiopia) na kampuni ya simu za mkononi ya Safaricom Ethiopia namna ambavyo wateja wanaweza kulipia kwa kutumia huduma ya “Lipa kwa simu” ikiwa ni sehemu ya kuwaonesha namna huduma ya kulipa kidijitali kupitia M-Pesa inavyofanya kazi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...