Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Komredi Daniel Godfrey Chongolo akisalimiana na Chifu wa Kabila la Wakonongo, mwenye utawala wa eneo la Kalovya, Chifu Michael Kayamba, leo Jumatano Oktoba 5, 2023, baada ya Ndugu Chongolo kuwasili Jimbo la Katavi, wilayani Mlele, kutembelea na kukagua mradi mkubwa wa Bwawa la Nsenkwa, linalojengwa kwa ajili ya kuwa chanzo cha maji safi na salama kwa matumizi ya wananchi wa vijiji 16 katika Halmashauri ya Mlele mkoa wa Katavi. Mradi huo utakaowahudumia takriban wakazi 68,000 utagharimu jumla ya Sh. 2.8 bilioni.

Akiwa katika eneo hilo la mradi, Katibu Mkuu Komredi Chongolo, baada ya kupokea taarifa ya maendeleo ya ujenzi wa bwawa hilo kutoka kwa Watendaji wa Wizara ya Maji, Ruwasa, Mkoa wa Katavi na Wilaya ya Mlele, waliobuni mradi huo, aliwapongeza kwa kubuni jambo litakalokuwa na matokeo makubwa na chanya kwa wananchi, kwa gharama ndogo.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...