NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limetoa elimu ya viwango vya ubora kwa Wajasiriamali wadogo waliojitikeza katika Maonesho ya Kibiashara ya Miaka 60 ya Muungano katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa maadhimisho hayo leo Aprili 25,2024, Afisa Masoko (TBS), Bw. Mussa Luhombero amesema wametoa elimu kwa Wajasiriamali hao jinsi ya kuzalisha bidhaa bora pamoja na ujuzi ambao utawawezesha kupata alama ya ubora ambayo itawafungulia wigo wa soko la ndani na la Kimataifa.

“Alama ya ubora kutoka TBS itawasaidia Wajasiriamali kuaminika sokoni na kukubalika katika masoko ya ndani na ya Kimataifa ambapo itawapatia mafanikio yenye tija kwao na Taifa kwa ujumla”. Amesema

Amesema wameshiriki katika maadhimisho hayo kwa lengo la kutoa huduma kwa wananchi hasa katika makundi mbalimbali ambayo ni wazalishaji,waagizaji,watumiaji wa bidhaa pamoja na wajasiriamali.

Aidha ametoa wito kwa waingizaji wa vipodozi nchini,kuingiza vipodozi ambavyo vimesajiliwa ambapo amesema kuwa kupitia tovuti yao kuna orodha ya vipodozi hivyo ambavyo haviruhusiwi kuingia nchini.

"Lakini pia wanaotumia vipozi wanaweza kututembelea ili tuweze kuwapa matumizi sahihi ya vipodozi na kwa wale wenye maduka ya chakula na vipodozi ambapo pia tunatoa elimu jinsi gani ya kusajiri maduka yao ya chakula au vipodozi". Amesema Bw. Luhombero

Sambamba na hayo Bw.Luhombero ametoa hamasa kwa wananchi wote kutumia bidhaa yenye alama ya ubora ya (TBS) ambapo itasaidia kuepukana na matumizi ya bidhaa zisizo na ubora ambazo zinaweza kuhatarisha afya kwa watumiaji.

Kwa Upande wake, Mfanyabiashara wa Vipodozi, Bw.Hamza Kamba ambaye ni muagizaji wa bidhaa kutoka nje ya nchi ameeleza kuwa yeye kama mdau ametembelea banda la TBS na amejifunza bidhaa ambazo ni bora na zisizobora.

TBS ili kuhakikisha inalinda usalama wa wananchi imetoa namba yake kupiga bure ili kuripoti bidhaa ambazo ziko sokoni zenye kutiliwa shaka kuhusiana na kuthibitishwa na Shirika la viwango ambayo ni 0800 110 827.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...