leo nimetembelewa ofisini na dardanus mfalme a.k.a darda king aishiye houston na kutesa sana kwa muziki wake wa bongofleva ambao umemfanya awe juu kama alivyo juma necha hapa bongo. kanambia yupo hapa kwa wiki nne na atapita london kwa shoo mbili kabla ya kurejea marekani. singo zake alizonachia na video ya 'yiho' zinatisha! mtembelee www.dardaking.com uthibitishe

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 15 mpaka sasa

  1. OVYO KINOMA HAKUNA KITU HAPO

    ReplyDelete
  2. Oyaa babu wacha kukandia musicians. Jamaa ana-represent wanamuziki Wabongo huko USA kwa sababu hakuna wengine wa Bongo huko, kwa iyo tumfagilie,, aaiiight?

    ReplyDelete
  3. ovyo ni ovyo ata kama anawakilisha wabongo.kizuri kinaonekana na kibaya cha onekana pia.Ovyo tu ajui kuimba.analazimisha fani, fani ina wenyewe atuachie sisi

    ReplyDelete
  4. Wewe Anon#2 usidanganye wa2 kwamba USA hakuna musicians wa Bongo. Minnesota kuna musicians wakali sana na wenye talents Wabongo

    ReplyDelete
  5. Michuzi nimeishi/kufanya kazi hapa USA for the past 17 yrs. Simfahamu huyu bwana kabisa, I know few musicians waki-Bongo waishio Minnesota.

    ReplyDelete
  6. mchovu jamaa, hata video yake ni mbovu mno, hata kwa standard ya bongo sasa hivi kuna machizi kibao tu wanampita. U can't knock his hustle though.

    ReplyDelete
  7. Hata kama ni mchovu lakini amejaribu. Mtoto huanza kwa kutambaa kisha...

    ReplyDelete
  8. Anatesa waoi wakati no one knows this sucker? Alikuja kwenye party moja Atlanta alivyoperform hovyo nafuu tu wangetuwekea CD za mchiriku. Hana lolote kwa kweli hata kama mtoto anaanza kwa kutambaa naona mtoto huyu ni kipofu so hata njia haoni.Fani haziwi forced you either have it or you simply don't. As simple as that.

    ReplyDelete
  9. Piga astaghafiru. Upofu sio tusi la kumtukana mtu. Mtu hutukanwa kwa uchafu na ujinga na sio kilema.

    ReplyDelete
  10. fala tu huyo,what is dardaking?anajifanya gangater kumbe gaystar..

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 02, 2006

    Kwa taarifa yenu huyu ndiye Mfalme wa bongoflava, miziki yake imekubalika dunia nzima, nyie mnaosema hamumfahamu kutwa mnabeba maboksi sasa mtamfahamu vipi, miaka 17 uko us. mbona hata wewe hatukujui, ulirudi lini kwenu ukafanya jambo la maana kama analofanya Mfalme?. Ule wimbo namba 4 ni spesho kwa haters like you!! hahah!!. I love that track. sikilezine miziki ya mfalme kwanza ndio mposti uharo wenu humu

    ReplyDelete
  12. AnonymousMay 02, 2006

    Video za Darda King mpya zimetulia sana sijawahi kuona mfano wake hapa bongo track zake zina quality ya kimataifa pia. cha msingi ni kumsapoti huyu bwana ili awaonyeshe njia hawa marapa wa huko waweze kuwa na quality kama yake. Nyimbo zake sio makelele tu zinaleta sense, ni songi ambazo hata wazee tunaweza tukazisikiliza.
    Hongera Darda king. nice website too.

    ReplyDelete
  13. AnonymousMay 02, 2006

    Big up dardaking, naona mafala wasiokufahamu wanachonga sana, cha msingi ukirudi huku ufanye tour ya nguvu kuliko ya mwanzo ili hawa madomokaya wakuelewa fresh. kwenye kuhastle wewe ni namba moja.
    You're a hustle and they're costomers. it dont matter what they say. funika mzee.

    ReplyDelete
  14. AnonymousMay 02, 2006

    Congratulations Darda King, Nimesikia vitu vyake radio free africa ni noma tupu.

    ReplyDelete
  15. AnonymousMay 02, 2006

    bwana mfalme mimi nashauri ile video yako ya kwanza uiondoe kwenye website yako maana haiendani na wewe kabisa, nadhani kipindi kile ulikuwa unajikongoja lakini sasa una video kali kama fresh prince. sasa basi tuwekee hizo mpya pia sio tunaziangaliz channel 5 tu!!!.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...