shirika la utangazaji la uingereza - bbc - lilipomtuma mtangazaji wake noel mwakugu kuja bongo kutafuta na kupasha habari halikumaanisha jamaa apitilize na kutafuta vya ziada. lakini huyu bwana akapitiliza na kuopoa jiko liitwalo kissah mwangopola. hapa mwandishi habari mwandamizi agnes kabigi na mumewe wanamsuta noel kwa kupitiliza wakati wa sendiofu ya kissa ilofanyika kambi ya polisi barabara aya kilwa dar. na ili nimtunzie siri noel amenialika kwao nairobi siku ya april 22 (jumamosi hii) kwenye ndoa rasmi itayofungwa kanisa la all saints na kisha kujichana pale sailing club lang'ata. bahati mbaya sintoenda kwani jumamosi nina tenda ya arusi hapa dar

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...