
leo tumepata heshima kubwa sana photo point kutembelewa na familia ya bavon kapesi toka cheltenham, uingereza. nimefurahi kumuona shemeji yetu karolina na watoto bavon junia, jada na amani. na nilifurahi zaidi walipokubali kuingia studio na kupiga picha nami. pia kaka bavon na mkewe wamenitia moyo sana kwa kusema blogu yetu hii inasomwa karibu na kila mbongo alie ughaibuni. bavon na sehemeji, mkiondoka ijumaa naomba nisalimieni wabongo wote huko ughaibuni. waambie nawaheshimu, nawapenda na nitaendelea kuwatumikia kwa nguvu zangu zote. mbarikiwe nyooooote!


Picha nzuri sana ,i like the color
ReplyDeleteThat is nice, Michuzi. Tell your Bro. Bavon that I also live not far from Cheltenham. I lived in Glucester for many year. We can get in touch if that is okay for him. There is a good number of Tanzanian families in the Gloucestershire county.
ReplyDeleteusije jifanya unataka kumsalimia kisa umeona shemeji pale unataka kurukia mzigo
ReplyDeleteWe anony amekwambia yeye mlokole bwana usiwe na haraka mambo mengine hafanyi yeye ni kwa kakobe tu
ReplyDeletena kwa kifupi anataka mpa neno la bwana na amani ishuke ndani ya family yao.........ahahaha
ReplyDeleteJamani labda mimi ni wa miaka ya 47,
ReplyDeletenauliza kwani huyu Bavon yeye ni nani na anafanya nini? ni celebrity au mfanya biashara maarufu au ni vipi??
"Anonymous August 14, 2006 4:28 PM"
ReplyDeleteNafikiri Celeb wa wote hapa ni Michuzi, Kwasababu kile anfanya... hakijawahi fanyika kabla and we like it,
Kwa mfano mimi... ilikuwa nikimaliza kazi zangu by the end of the day ndio natembelea hii blog.... lakini sasa, im kind of addicted when i get in the office first is Michuzi blog and mails harafu mambo mengine.
"Anonymous August 14, 2006 4:28 PM"
ReplyDeleteKwa hiyo inamaana kama sio celebrity asiwekwe kwenye blogu? Acha mtima nyongo!
Hola Bavon, Caroline and the children. Wamependeza sana. Hawa ni marafiki zangu na watu wazuri sanaa. What a nice family!!
ReplyDelete