ulinzi mkali ulikuwepo na maalim seif kalisifu sana jeshi la polisi sio tu kwa ushirikiano mkubwa bali pia hata ile kuruhus maandamano na mkutano wa hadhara hapa dar, kesho zenj na novemba 14 kule pemba kushinikiza serikali ya mseto alisema leo mkutanoni imemshangaza hata yeye

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. Nashukuru kusikia maandamano yamemalizika bila purukshani.FFU wetu hapa bongo bila kufyatua mabomu ya machozi huwa wanaona hawajafanya kazi.Kazi kwelikweli.

    ReplyDelete
  2. TUNASHUKURU KWA HILO, MUNGU IBARIKI TANZANIA

    ReplyDelete
  3. Next time wasiandamane Bara kwa masuala ya Zanzibar yasiyo ya muungano.Mimi na wenzangu tulipanga kupinga mahakamani maandamano yasifanyike sababu hayana uhusiano na Tanzania Bara.Bahati mbaya Tibaigana Akatangaza kuyaruhusu jioni wakati mahakama zimeshafunga muda wa kazi.

    Afande Mwema utangaze kuruhusu maandamano siku za kazi mapema ili wengine kama tuna uchu wa kwenda mahakamani tuwahi kabla majaji hawajaenda kulala.Safari hii umetunyima haki zetu tuliokuwa hatuyataki hayo maandamo ya kutupotezea muda watu wa bara na kuziba barabara zetu bila sababu za msingi kwa vitu vya wapemba .Hongera magazeti ya Tanzania bara kwa kutoandika habari za maandamano ya CUF yaliyofanyika Zanzibar jana.Ni sawa yaachieni magazeti ya huko zanzibar yaandike habari zao.Na ni vizuri hamkwenda nadhani na nyinyi waandishi hamjasahau kipigo cha mbwa walichowapiga wana CUF Pale BUGURUNI.Kile kipigo hamji kukisahau na vikamera vyenu.Kumbe na nyinyi waandishi waoga mkibondwa!! Nimeshajua dawa ya kukukomesha michuzi.Michuzi ukiniblog vibaya nakuahidi nitakubonda.

    ReplyDelete
  4. Tunashukuru kuwa kila upande ulishika adabu wananchi tusiohusika na maandamano mali zetu hazikuguswa.Zingeguswa polisi na CUF wote tungewaweka matatani mahakamani sababu ya hayo maandamano yanayohusu Zanzibar mliyokubaliana myafanyie kwenye ardhi isiyohusika ya Tanzania Bara ambao mnajua fika kuwa hatukumpigia kura hata moja Karume.Polisi na CUF mlikubaliana kuendesha umamuluki dhidi ya Karume Tanzania bara.Said Mwema acha siasa.Siasa za Zanzibar ziache huko huko Zanzibar.Maandamano yanayohusu Zanzibar usiya-Import Tanzania Bara.Wewe jua vizuri sheria za muungano.Usikurupuke tu kupanga vijana wako barabarani.Hawa CUF ukiwadekeza watakupambanisha na raia bila sababu.Haya maandamano ulikosea kuyaruhusu.Usirudie tena kosa la namna hiyo.Tutaomba wabunge wapunguze mshahara wako kupinga bajeti ya wizara yenu kama utaendelea.Maandamano hayo ni moja ya Kero zilizoongezeka za muungano ambazo Umeziongeza Said Mwema kwa kuruhusu uhusiano wa bara na visiwani ukae vibaya kwa kuruhusu maandamano yafanyike kumlaani kiongozi wa upande wa pili wa muungano katika ardhi ya bara wakati bara haihusiki na uchaguzi wa Raisi wa Zanzibar.

    ReplyDelete
  5. EWE, Monday, November 13, 2006 5:23:00 PM, Mtoa Maoni: Anonymous...

    WAKATI WA KUPIGANIA UHURU...kama mwanasiasa akitoa hoja mbadala yenye msimamo swafi, tulikuwa tuNaimba:

    TOBOA!

    Kwahiyo, nakupongeza kwa TOBOA!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...