waweza kutaja tofauti tano zilizo katika picha hizi? mshindi kama kawaida anapata zawadi ya picha aitakayo na atatangazwa ijumaa. wadau walioshinda shindano lililopita na ambao tayari wametaja picha za zawadi wala msikonde. nazifanyia kazi. aidha, kuanzia sasa kila jumapili kutakuwa na chemsha bongo namna hiyo ama shindano. hili la leo wadau mlio ndani na nje ya bongo ruksa!

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 18 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 01, 2007

    Tumechoka na ahadi zako hewa, kama JK vilee. Kwanini usiwe za washindi wa zamani kwanza kabla hujakurupuka ni Chemshabong mpya?

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 01, 2007

    Tofauti iliyopo ni kwamba picha ya chini ina goli la mpira wa kikapu wakati ya juu haina. kama nimeshinda nitajuaje?

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 01, 2007

    michuuuu, naona matangazo ya bishara yameanza sasa! Aminiaaaa!

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 01, 2007

    child abuse! huyo mtoto asitumiwe hapo

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 01, 2007

    (1) Fimbo iliyo mbele ya mchezaji wa kike kwa kwanza

    (2) kiatu cha mguu wa kulia cha mchezaji wa kike wa pili

    (3) blauzi ya mchezaji wa kike wa tano (nyuma ya yule asiyekuwa na uniform)

    (4) Mlingoti wa taa kule waliko watazamaji

    (5)Nadhani vidole vya mkono wa kushoto wa huyu msichana asiyekuwa na uniform.

    Zawadi yangu: Nataka picha ya yule jamaa aliyepiga wimbo wa marashi ya pemba. Ninataka picha iliyopigwa miaka ya themanini wakati angali OSS.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 02, 2007

    Tofauti ni mstari huo wa mbele.Picha moja mstari uko nusu na nyingine mstari uko kamili.

    RB

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 02, 2007

    Ngoja nijaribu bahati yangu:
    1.Picha ya juu, mbele ya dada wa kwanza kabisa naona mstari sakafuni.Mstari huu ni nusu tu wakati katika picha ya chini mstari huu umeanzia mwanzo wa picha hadi mwisho wa picha.
    2.Picha ya juu,dada wa kwanza nyuma ya mtoto wa katikati amevaa blauzi ambayo haina weupe wowote karibia na mabega wakati dada huyohuyo picha ya chini blauzi yake ina weupe karibia na mabega,yaani kamba za mabega zimeunganishwa na viunganishi vyeupe.
    3.Picha ya juu,dada wa pili raba yake katika mguu wa kulia pana mstari au mchirizi mmoja mweupe,wakati dada huyohuyo picha ya chini, katika raba ya mguu uleule kuna michirizi au mistari miwili myeupe na siyo mmoja kama ilivyo katika picha ya juu.
    4.Picha ya juu,nyuma kabisa ya wachezaji wote(karibia na walipoketi watazamaji)sioni mlingoti wa goli kama ninavyouona mlingoti huo mahali palepale ila katika picha ya chini,badala yake naona kama taa za kuongozea magari(trafic light).(Mlingoti huu unaonekana vema usawa wa kichwa cha dada wa pili kutoka mwisho).
    5.Picha ya juu, karibia na kiwiko cha mkono wa kushoto cha mtoto wa katikati sioni kitu kujitokeza kwa nyuma kama nionavyo katika picha ya chini mahali palepale karibia na kiwiko cha mtoto kuna kitu kimejitokeza kwa nyuma,huenda ni mkandaa wa suruali au ni kitu chini ya sakafu kikajitokeza kama kiko karibia na kiwiko.
    Ndugu yangu kama nimeshinda basi naomba zawadi ya picha ya LING'OMA Haswaa siyo artificial. Weka kwenye Blog.Ugonege!

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 02, 2007

    chuma laonekana kwa picha ya pili ya kwanza lina halionekani vizuri,sakafu ya pili mstari umeenda mpaka mwisho wa picha ya kwanza umekatika,miti ya picha ya pili inaonekana na mwanga zaidi kidogo kuliko ya kwanza,kwa ujumla picha ya pili ina mwanga zaidi ya kwanza umepungua kidogo kuna kaugiza,picha ya kwanza umeichukua ukiwa kwa juu kidogo ya pili ukiwa usawa mmoja.

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 02, 2007

    TOFAUTI NI HIZI HAPA:

    1.Mstari uliopo mbele kwa aisha madinda uko nusu kwa picha ya kwanza na uko full kwa picha ya pili.

    2.Chuma ya Basketball goal imeondolewa kwa picha ya kwanza na ipo kwa picha ya pili.

    3.Dada wa pili kwa aisha madinda kiatu chake cha kulia kina mstari mmoja tu mweupe (white line) kwa picha ya kwanza ila kuna mistari miwili (white lines) kwa picha ya pili.

    4. Mtoto wa kike wa nne toka aisha madinda,,kidole chake kidogo cha mkono wa kushoto kimeondolewa kwa picha ya kwanza ila kipo kwa picha ya pili.

    5. Dada wa tano kwa aisha madinda,mkanda wa blauzi yake upande wa kushoto,,umefutwa kichuma kinachounganisha mkanda huo,,ila kipo kwa picha ya pili,,hicho kichuma ni cheupe....

    6. PICHA YA KWANZA NDIYO ILIYO-EDITIWA,,,,*EDITED*,,,,NA PICHA YA PILI NDIYO ORIGINAL...

    SALIM SALIM, göteborg swdn.

    ReplyDelete
  10. Issa cheki majibu yako hapa:
    http://mshindiwaleo.blogspot.com/2007/07/chemsha-bongo-ya-july-01-ya-issa.html

    UKINIBANIA USHINDI WANGU NITAKUSHUSHA MSHIPA !!

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 02, 2007

    Anko michuzi salamu.
    Tofautizzz

    1. Mstari wa uwanja uko nusu katika picha ya kwanza wakati katika picha ya pili uko fulu.

    2. Dada wa kwanza rangi ya nguo yake imefifia katika picha ya kwanza kulinganisha na ile ya pili.

    3. Dada wa pili kiatu chake, mstari mmoja mweupe umekula kona (auko)

    4. Dada wa nne (baada ya mtoto) katika kitopu chake mistari miwili imekula kona (imepotea)

    5. Goli la netball kunamwananchi kaliiba katika picha ya kwanza (haliko)
    Anko michuzzzz nikifanikiwa kushinda naomba full picha ya jengo la BoT likionesha mapacha na kale ka kati kati, nataka kuprint katika t-shirt. au kama hiyo ngumu sana. basi snepu moja tamu ya ile askari monumenti yetu.
    Asante! mdau kutoka mashariki ya mbali

    ReplyDelete
  12. AnonymousJuly 02, 2007

    Issa Michuzi nimeipitia picha hiyo na kubaini tofauti zifuatazo,
    1.Mstari wa mbele kwenye picha ya juu haukukamilika
    2.Dada wa pili kiatu chake cha mguu wakulia kwenye picha ya juu,hakina ufito mmoja.
    3.Dada wa tano kutoka mbele,(nyuma ya binti mdogo)blouse yake haina Kifungo,marembo chini kwenye bega kwenye picha ya juu
    4.Picha ya juu haina mlingoti kwa nyuma,nadhani ni wa taa ama goli la b/ball.
    5.mti kwa nyuma

    Mbwambo UK

    ReplyDelete
  13. AnonymousJuly 02, 2007

    watu mna macho macho ka paka!mi mbona sioni tofauti hata moja. Issa eh,zote ziko sawa bwana.

    ReplyDelete
  14. AnonymousJuly 02, 2007

    toafuti 5 za picha,
    1,mstari uliopita mbele ya madinda uko nusu.
    2,hakuna goli la netball.
    3,mcheza show 2 kiatu chake cha mguu wa kulia kina mstari mmoja wa adidas.
    4,mcheza show namba 4 nyuma ya mtoto singland aliyovaa haina mistari meupe juu kati ya maziwa na mabega.
    5.mtoto anaesheza show amekatwa kidole kidogo cha mwisho mkono wa kushoto.

    picha halisi ni ya chini

    ReplyDelete
  15. AnonymousJuly 03, 2007

    TOFAUTI NI HIZI HAPA:

    1.Mstari uliopo mbele kwa aisha madinda uko nusu kwa picha ya kwanza na uko full kwa picha ya pili.

    2.Chuma ya Basketball goal imeondolewa kwa picha ya kwanza na ipo kwa picha ya pili.

    3.Dada wa pili kwa aisha madinda kiatu chake cha kulia kina mstari mmoja tu mweupe (white line) kwa picha ya kwanza ila kuna mistari miwili (white lines) kwa picha ya pili.

    4. Mtoto wa kike wa nne toka aisha madinda,,kidole chake kidogo cha mkono wa kushoto kimeondolewa kwa picha ya kwanza ila kipo kwa picha ya pili.

    5. Dada wa tano kwa aisha madinda,mkanda wa blauzi yake upande wa kushoto,,umefutwa kichuma kinachounganisha mkanda huo,,ila kipo kwa picha ya pili,,hicho kichuma ni cheupe....

    6. PICHA YA KWANZA NDIYO ILIYO-EDITIWA,,,,*EDITED*,,,,NA PICHA YA PILI NDIYO ORIGINAL...

    Kichwabuta Mwendantwala

    ReplyDelete
  16. AnonymousJuly 03, 2007

    michuzi sidhani kama kuangalizia kunaruhusiwa..

    ReplyDelete
  17. AnonymousJuly 04, 2007

    Wengine wamepiga chabo kwa waliotangulia hapo.
    Michuzi kazi unayo ya kutoa mshindi hapo.

    ReplyDelete
  18. AnonymousJuly 05, 2007

    Bro Michuzi,
    Leo nimeona ni vyema na mimi nishiriki in one way
    or
    onather katika blog yako ambayo ni mdau mzuri
    sana.

    Nimeweza kupata tofauti tano katika picha ambazo
    umeposti weekend hii.

    > > Tofauti nilizoziona ni kama ifuatavyo:
    > >
    > > 1. Mbele ya dada wa kwanza katika picha kuna
    > mstari
    > > ambao katika pich ya kwanza mstari huo unaishia
    > sehumu
    > > fulani na katika picha ya chini mstari huo
    > unaendelea
    > > moja kwa moja.
    > >
    > > 2. Kuna nguzo ya taa ambayo inaonekana katika
    > picha
    > > moja na katika picha ya pili nguzo hiyo ambayo
    > > ninaimani ni ya taa haionekani katika upande wa
    > kulia
    > > wa picha.
    > >
    > > 3. Dada aliye nyuma ya mtoto tanktop yake
    > inaoyesha
    > > alama nyeupe katika eneo la shingo katika picha
    > moja
    > > na alama hizo hazionekani katika picha ya juu.
    > >
    > > 4. Dada wa pili katika picha kiatu chake cha kulia
    > > katika picha moja kinaonyesha kuwa na strip moja
    > na
    > > katika picha nyingine kiatu kina strip mbili.
    > >
    > > 5. Mwisho ni picha ya mtoto, mkono wake wa kushoto
    > > unaonekana kama umeingia mfukoni katika picha moja
    > na
    > > katika picha ya pili mkono huo unaonekana wazi
    > wazi
    > > kuwa haupo mfukoni na kidole chake kidogo cha
    > mkono
    > > huo kinaonekana dhahiri.
    > >
    > > Ninamatumaini nitakuwa nimetimiza masharti ya
    > chemsha
    > > bongo yako na i am looking forward to be declared
    > as
    > > winner in this puzzle.
    > >
    > > Looking forward to hear from you.
    > >
    > > Yours.
    > >
    > > Katty.
    > > Mdau wa New York.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...