
enzi za msanii david kyungu wa katuni za kalikenya unazikumbuka? huyu bwana baada ya kuishi ugahaibuni kwa takriban miongo miwili sasa yuko nyumbani akiendeleza libeneke na kampuni yake iitwayo matatizo productions na anashughulika na kuprodyuzi filamu na video. yeye ndiye anayewatengenezea hakielimu filamu zao


BW. Dav Kyungu! uko wapi mshikaji wangu ???? nakumbuka miaka ya 70's wakati nikiwa Sekondari nilikuwa napenda sana katuni zako baadaye nikasikia umeenda kusoma Ujerumani na mara nakuona leo hii Bw. misupu kakutundika hapo kwenye BLOG yake nikashangaa !!!! Uongo mbaya nilikuwa napenda sana KATUNI zako ambazo ulikuwa unazitoa katika gazeti la KIONGOZI (Gazeti la Kanisa Katoliki enzi hizo na sijui sasa kama bado lipo !. Sasa pamoja na hizo shughuli ulizonazo siku hizi unaweza kuendelea kuposti hizo katuni zako kwenye hii BLOG ili nasi tulio nje ya nchi tuweze kufaidika na UJUZI wako Bw. David Kyungu ??? Bw. Michuzi, tunaomba utufikishie OMBI letu ili kwani huyu Bw. alikkuwa anafurahisha sana kwa katuni zake ambazo pia zilikuwa na mafunzo mazuri kwa jamii !! Ciao.
ReplyDelete