Home
Unlabelled
hongera
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Most read Swahili blog on earth
Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.
Niliandika kwa kejeli baada ya kuona kuwa huyu bint RICHAD HIA atakuwa miss Tanzania.Nilimpa hadi jina la Nyamambara na kumpa uraia wa majita kwikerege.hatimaye kama mzaha vile kawa.Sasa mimi wanakijiji wenzangu nahoji nini maana ya mila na desturi.Sijajua vigezo vilivyotumika na majaji hao kumchagua huyu mhindi kuwa mtanzania halisi na KUBEBA bendera ya Tanzania.Tanzania tuna makabila na yanafahamika idadi yake.JE HUYU MISS TANZANIA ANATOKA KABILA LIPI KATI YA MAKABILA YA TZ.Mimi niko huku ughaibuni natanga na njia.Na hapa nilipo kuna watoto wa kiTZ waliozaliwa huku na hawajawahi kwenda nyumbani Tanzania.Lakini wana bendera na nguo za rangi ya bendera ya tz na wanajivunia uTZ wao wawapo na marafiki zao wazungu.Hebu nisaidieni wajameniiii,nikiulizwa na mtoto mmojawapo siku ya miss dunia niwaonyeshe miss TZ,Mmmmh AIBU.Wasiwasi wangu ni pale atakapo kaa karibu na miss India na kama kawa watoto wa siku hizi wanahoji utafikiri wametumwa.Sie bwana tulishazoea kushangiia miss TZ mwenye rangi ya Tanganyika.Akinyoa unywele wake kweli ni mTZ halisi.AIBU,AIBU,AIBU. huyu si miss TZ ni miss Wahindi wa kisutu.
ReplyDeleteSasa tuseme kawawa hili halioni???
Wajameni tabu ilikuwa imelala sasa tumeiamsha.Balaaaa
Majita
1.Kila Mkoa uwe unatoa mwakilishi mmoja tu! Hakuna cha kujaza maji ya KINA-NDOONI NA ILALE n.k maana hiyo ni kuendeleza mizani ya hadaa.
ReplyDeletesawa na wamarekani hata kama wanazo kutujazia wafukuza upepo watano kwenye mbio moja unategemea kuwa kweli wakose hata medali ya mbao?(naongelea zaidi kwenye Olimpiki).
2. Michu sipendi unapoamua kusensor mawazo yangu au ya yeyote na kuyatupilia kapuni bila sababu mf. nilipouliza Mastaaz Wakongwe nafasi (hasi au chanya) ya Ushirikina katika michezo yetu Tz hususani soka.
Hongera mamaa! Kazi kwako kutuwakilisha kidunia!Tunakuombea mafanikio ili uitoe kimasomaso nchi yetu japo hata kwenye kumi bora! Vaa ujasiri utashinda tu!
ReplyDeleteHongera Richa, lakini sikutaka ashinde, jamani Tanzania sasa lazima tuamke tuwe kama nchi za wenzetu, huku niliko kuna tofauti ya raia 1. Raia mzaliwa 2.Raia alioupata kwa maombi..au wazazi au babu zake waliupata uraia kwa kuuomba(walowezi !!!lol!!!).....kwa kifupi mimi raia wa ulaya na hata niende kujaribu kushindania miss huku, SIPEWI hata nafasi ya kuyaingia mashindano..labda ningekuwa mchanganyiko (mzungu na mweusi) ndo wangeliweza kunifikiria..lakini mweusi tii no way, tena NO NO NO kwa herufi kubwa kabisa..sielewi rangi ya ngozi ya Richa inaiwakilisha vipi Tanzania..duu hongera zake lakini roho inaniuma, wabongo tunachekesha...anyway, WAOSHA VINYWA AMKENI, MTOE MALALAMIKO YENU, NA KAKA MICHU USIBANIE, HIZI NI SERA ZA UWAZI NA UKWELI.
ReplyDeleteKAKA MISUPU! NAJUA JANA LIVERPOOL WAMEMKANDAMIZA DERBY LKN MISS TZ MDOSI???? HII HAIJAKAA SAWA, SIYO ISSUE YA UBAGUZI LKN SISI WABONGO NI WACHEMKAJI KUPITA VIWANGO VYA UCHEMFU...ANYWAY LET SEE HUKO CHINA ITAKUWAJE AICHA TOKA TOKA TZ....NI MAWAZO YA KINA PATEL WANAFIKIRI AICHA ANAWEZA KUILETEA SIFA BONGO AU LAZIMA MISS TZ ATOKE DAR TENA KINONDONI?????
ReplyDeleteCongratulations dada,nakutakia kila la kheri ushinde na huko kwenye miss world,
ReplyDeleteWanaojadili rangi hawana jipya,Hii ni karne ya 21 ya sciance and technology wao bado wapo kwenye ujima,
Watanzania hatuna kabila wala rangi mambo hayo wayapeleke Kenya,Uganda, Burundi au Rwanda but bongo hayana nafasi.Nyerere akumbukwe kwa vitu kama hivi,
Congrats.
CHA CHANDU
Vipi Miss Tanzania nilini tena? maana nasikia jana ilikuwa miss India beauty peagent cant wait to see our queen this year
ReplyDeletesciance?????? haya wewe ndo maana yake nini hii?au ulikuwa na maana ya science?Ndio Nyerere alitufundisha ujamaa na kujitegemea huyu Richa na Wadosi wenzie wanayajua haya! Ebuuuu msije tu hapa kukurupuka na kumtaja bureee hayati baba wa Taifa.Watanzania tunayo makabila ila hatuna ubaguzi wa kikabila hiyo kweli .ILAAAA PIGA UA HAPA MCHEMSHOOOOOO,NEVER IN THIS WORLD MWEUSI MZAWA WA INDIA ANAWEZA AKAPEWA UMISS INDIA,UNAELEWA ATI HATA KAMA MIE NIKO KWENYE SITUATION YA AICHA INDIA ,SIJUI KAMA NITAWEZA KUTWAA TAJI LA MISS INDIA,NEVER NEVER.duuuuuuuuu.Nina hasira sanaaaaaa.Bro michu hii comment in fact tupu please ipublish.
ReplyDeleteAcheni ubaguzi !! ameshinda tusubirie atuwakilishe basi mbaya wanangalia uraia wa kuzaliwa sio kingine hapo hatuna cha kusema. Mtaosha vinywa no one will listen .Sauth africa naona wamebwabwaja wameamua kuacha maana most of the time wanakuja wazungu au wahindi tu hapo sasa na sie tz tumeshaingiliwa na nauhakika next years to come watakuja wahindi kibao kushiriki .Hii ni kwa sababu ya huyu amepewa mwanya basi wadosi wote watajichopeka just wait you will see.
ReplyDeletewabongo tunatia aibu sana, imagine watu hapa wanachonga kwanini mhindi ashinde beauty contest ya Tanzania....
ReplyDeletehivi kweli huu ushindi una impact kubwa kiasi hicho kwa maisha ya watanzania?kuliko ilivyo kwa wabunge wa kiarabu na kihindi, kumbukeni tuna mawaziri wahindi na waarabu nchini mwetu.
hayo tumeyanyamazia kwa miaka yote tangu enzi za Mwalimu Nyerere, leo hii tunapiga kelele eti BINTI WA KIHINDI KWANINI AWAPIGE BAO MABINTI WA KIBANTU....
tunaibiwa uchumi kila kukicha hatupigi kelele, hii kitu ya kudumu mwaka mmoja imekuwa kelele mtindo mmoja.no wonder jamaa pale ikulu wanamudu kuongoza nchi bila wasi wasi licha ya kuboronga.
MICHUZI LAZIMA UWE MAKINI SASA BABAKE.
ReplyDeleteWATU SASA HIVI TUNAKWENDA NA WAKATI. HAYA MAMBO YA UKABILA, UDINI, RANGI AU MTU ANATOKA MKOA FULANI LAZIMA YAKOME HUMU.
KAMA WATU WANATAKA KUTOA MAONI YA KUMKASHIFU HUYU MSHINDI, YAPIGE CHINI.
HUYU ANASTAHILI KUSHINDA, ALISTAHILI KUSHINDA TANGU NILIMWONA AMEKUWA MISS KINONDONI NA ATAWEZA KUSHINDA ZAIDI HUKO MBELE INGAWA NAFASI SI KUBWA HIVYO.
HAYA MAMBO YA KUDAI HUYU MHINDI YANATOKA WAPI. MBONA MISS ANGOLA MWAKA JANA ALIKUWA MRENO HASWA NA ALIFANYA VIZURI KWENYE MISS WORLD?
KWA NINI WATU HATUAMKI NA KUNGALIA TUNAELEKEA WAPI NA SIYO TUMETOKA WAPI? ANGALIENI TIMU YA TAIFA YA UFARANSA ILIYOJAZA WAAFRIKA KIBAO NA MATUNDA YAKE YANAONEKANA.
MAKELELE, CHIMBONDA, VIERA, CISSE, DAIRA NA WENGINE WOTE WANATOKA AFRIKA. HATA ZIDANE NAYE ANATOKA AFRIKA MNAJUA HILO?
THIERY HENRY, WILLIAM GALLAS MNAJUA ASILI YAO WAPI HAO? VISIWA VYA CARRIBEAN LAKINI NDIYO WALIOILETEA NA WANAILETEA UFARANSA SIFA.
UKEREWE WANAJIFANYA WAO WANAJUA NA MATOKEO YAKE WANAOZA KWENYE SOKA SIKU. LAKINI KWENYE KRIKETI WAMAJEFUNZA NA WANAINGIZA MAPONJOLO KIBAO. MNAKUMBUKA NAHODHA WAO HUSSEIN KAMA NI PONJOLO?
LA MSINGI HUMU NDANI NI KUMPA PONGEZI NA KUMWOMBEA KILA LA KHERI KATIKA MATAYARISHO YAKE ILI AJIANDAE VYEMA NA IKIWEZEKANA AKAFUNDWE MAPEMA ILI ASHINDE KWENYE MISS WORLD.
ACHENI HIZO. MICHUZI BORA URUHUSU MAONI YENYE MSINGI HAYA YA KUKASHIFU PIGA CHINI NA MWENYE KULALAMIKA AKAFUNGUE GLOB YAKE.
CIAO. MIMI MWEUSI KAMA MKAA.
Jamani hebu tuache tabia za ubaguzi. Ndiyo ni muhindi lakini si mtanzania. basi hiyo ya tosha. Hongera dada kwa kushinda.
ReplyDeleteHii sasa inaboa yaani hata kwenye umiss tumewekezwa inamaana wale warembo 25 wa kitz hawafai mpaka apewe mhindi ama kweli watanzania hatujui tunachofanya. Hivi Nyerere angekuwepo siangezimia kusikia muhindi anapewa bendera ya taifa kuawakilisha nchi haya bwana kama huo ndo utandawazi sina neno. ila kama vipi KIKWETE AFUTE HAYA MASHINDANO na awashauri waanzishe mashindano ya WAUZA SURA AU VIBURUDISHO! KUMBE MABADILIKO ALIYOKUA AKIYASEMA MC TAJI LIHUNDI NDO HAYA! ANYWAY WATZ AMKENI JAMANI TUNAONEKANA MAFALA HIHIVIVI! Mi naona INDIA INAWAWAKILISHI WAWILI NA TZ PATUPU! bro michu usinibanie itoe hiyo bwana! NYAAAMBAFUUUUUU!
ReplyDeleteAnnon wa 1:41,umeongea ukweli mtupu 200%,mijitu mingine imekalia ubaguzi badala ya kufikiria mambo ya maendeleo.tatizo watu weusi tunapenda kulalamika sie tukifanyiwa lakini sie tukifanya tunakuwa kimya!!!imagine kabila ingine wapiga kelele hivi si ingekuwa oooh maracist....FYI kuna maracist vilevile weusi,racist sio mweupe tuu,this is 21st century.
ReplyDeleteHAPA MI NAONA KUNA UMUHIMU WA KUBADILISHA BENDERA YETU TUONDOE RANGI NYEUSI INAYOWAKILISHA ASILI YA WATU WA TZ KWANI HAINA MAANA MBONA HATA WAHINDI,WAARABU NA HATA WAZUNGU NAO PIA NI WATANZANIA.KWANZA NAONA BENDERA IWE NYEUPE BASI KWANI HIYO RANGI YA NJANO NAYO HAINA MAANA KWASABABU HATAMALIASILI ZOTE ZIMESHA WEKEZWA SIO ZETU TENA, HAYA BLUE NAYO BAHARI SIO YETU NA HATA ZIWA VICTORIA WENYE NALO NI SUDAN NA MISRI AU HUMJUI HILO WATZ NDO HIVYO MTAJIJU! KIJANI RANGI YA CHAMA CHA MAJAMBAZI. ANYWAY NI MTAZAMO WANGU MSIKONDE SANA WATANZANIA!!!!!!! BENDERA IBADILISHWE NIKO SERIOUS KAMA NDO HIVYO! BRO MICHU HII NZURI IACHIE MTU WANGU TUNAHITAJI BENDERA IBADILISHWE!
ReplyDeleteUSA inaamini kwamba ili nchi yao iweze kuendelea mbele zaidi ilipo sasa hivi ni lazima iruhusu jamii za watu toka nchi mbalimbali kuhamia katika nchi yao yaani USA.
ReplyDeleteKila mwaka inatoa Diversity Visa zipatazo 55,000 (yaani elfu hamsini na tano).
Mbali ya hapo, mtu yeyote ambaye ana kipaji maalum (awe sehemu yeyote dunia ana nafasi kubwa ya kupewa ukazi/ uraia wa Marekani bila ya kujali rangi, jinsi, dini nk.)
Ka-nchi ketu kadogoooo, makelele meeeeeengiiiiiii.
Katika karne hii ya leo hatupaswi kuulizana wewe mhindi au msukuma? Ili mradi wote ni watanzania ni vema tukajua nini ni haki na wajibu wetu kama watanzania badala ya kuangalia mambo yasiyokuwa na tija.
Richa, kama mtanzania mwingine yeyote ana haki ya kuwania nafasi yeyote ile bila ya kujadiliwa rangi yake au dini yake au eneo analotoka nk.
Ninamsifu sana Richa kuwa dada wa mfano kwa wengine kwamba kujiamini ndiyo kutakakomtoa katika unyonge mwanamke yeyote yule,
Vilevile ameonyesha kwamba watanzania wote ni sawa hakuna rangi katika hili.
Mwisho, kutokana na vigezo vya mashindano ya urembo, sura pekee si kigezo cha ushindi, nadhani kwa wale ambao tumekuwa tukifuatia na kuweka kumbukumbu ya yanayoongelewa, ni kwamba kuna vigezo vingi huangaliwa.
Namalizia kwa kuandika kuwa washiriki wote ni washindi lakini ni LAZIMA tupate mshindi mmoja kati ya washindi wote nae ni Richa amestahili kati ya washindani wote.
Mbona hao wahindi wakiwaita jagwani muende mkale pilau hamukatai TENA MNSHANGILIA!!!!?na wavyoidhamini TAIFA STARS YETU HAMUKATAI?WABONGO TUSIWE NA KASUMBA!TUACHENI U-PRIMITIVE!KWANZA TUNAJITIA AIBU TUNAVYOONGEA PUMBA KUUSU MAMBO YA UKABILA.
ReplyDeleteMimi nina swali kama Mtanzania mzaliwa katika hospitali ya Ocean road na wazazi wote wa kimatumbi.... Kama WAHINDI wanajiita ni wazawa wa Tanzania kwa nini ni vigumu sana kukuta Muhindi kaolewa na "Mzalendo mweusi"?????!!!!!
ReplyDeleteHuku USA kulikuwa kuna zoezi la kubadili Passport nilishangaa kuona "WAHINDI" walikuwa wengi kushinda "WAZALENDO".....na katika shughuli za Kitaifa au mikutano na Misiba hawaonekani....Naomba tujiuleize sana haya mambo ndugu zangu.
Haitanishangaza kuona baadae tunakuwa na Rais wa "KIHINDI" kwa kuogopa kujivunia "UZALENDO" wetu.
Ahsanteni na muda mwema kokote pale mlipo.
GodBless.
Miss Tanzania kuwa mhindi sifagilii wala nini puuh! Huko kwao Mtanzania kuwa Miss India thubutu!! Wana ubaguzi kama nini.Tusubiri 2010 rais MHINDI.
ReplyDeleteSioni ubaguzi wa wazawa utaisha dhidi ya raia wa Tanzania wasiokuwa na ngozi nyeusi. Mimi kama Mhindi naona ni sasa na kupigana na Kaburu. lakini sina uwezo wa kupigania uhuru wangu kortini lakini napigania katika sekta ya uchumi. Na kama mnavyoona, matajiri wa Kihindi wanazidi kama wa vodacom, na maisha yetu hayajabadilika kutokana na ubaguzi wenu. Tunazidi kutajirika kwa kuwa tuna umoja. Mtasema sana hapa kwa Michuzi, lakini pia mtalipa ada yetu katika internet. Wahindi tumezaliwa na ubongo wa kibiashara, ubaguzi wenu utazidi kutupa nguvu ya kuvuna kiuchumi. Bora mtuue tu ili nchi iwe kama ya Zimbabwe, wote tukose lakini kwa sasa tuko step 10 mbele yenu. uliza TRA.
ReplyDeleteNawakilisha kana Michuzi hatabagua maoni ya Mhindi.