mwenzenu nimeshanunua tiketi ya gemu la leo...

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 15 mpaka sasa

  1. NCHI HURU KAMA TANZANIA LAZIMA NITUMIE UHURU WANGU KUHOJI.

    BRAZA MICHU NINA HOFU NA MASHAKA KWAMBA HIYO TICKET RAIS WA TFF TENGA NDIO KAKUPA BUREEEEEEEEE ILI UNINGIA UWANJANI WADAU TUPATE MASNEP KWENYE DAILI NYUZI NA KWENYE BLOG:

    ILA USIHOFU MAANA NI YAKO IWE YA KUPEWA AU YA KUNUNUA KAMA SISI KIHALALI.

    ReplyDelete
  2. Michuzi acha uhuni, hiyo ticket siyo yako. Maana kwa jinsi ninavyokufahamu, lazima utakuwa umenunua ya sh. 3,000 na siyo hiyo uliyotuonyesha.

    Mzee wa TBS

    ReplyDelete
  3. NIMEFURAHIA SANA KIINGILIO CHA MECHI YA LEO. POLENI SANA KAMATI YA MISS TANZANIA SIJUI KAMA MTARUDISHA PESA ZA GARI (USED) MNALORINGA NALO NA KUWEKA KIINGILIO UTAFIKIRI TUNAENDA BUZWAGI KUCHIMBA MADINI. POLEEEEEEEEEEEE
    LEO MAMBO YOTE NESHO STADIUM BWANA!!!

    ReplyDelete
  4. HIYO TICKET MBONA HAINA SEAT,ROW WALA SECTION NUMBER?

    ReplyDelete
  5. We Michuzi usitudanganye... nyie waandishi/wapiga picha mna pasi maalumu za kuingia uwanjani na hata kama kuna kulipa anaelipa ni mwajiri wako (na sio kutoka mfukoni kwako.

    Acha danganya toto ...
    HILO NI TANGAZO LA BIASHARA!!!!

    ReplyDelete
  6. KAKA MICHI UMEAMUA KUBAAANA WE NYUZI ZA MEDI WACHA SASA MIMI NIZIVUNJE MWENYEWE.

    KUTOKA VYANZO VYANGU VILIVYO KAMILIKA MEDI KATOLEWA JANA LUGALO HOSPITAL SIO KWAMBA KAPONA ILA KWAMBA ANENDELEA VEMA.

    MIMI SIO MSEMAJI WA FAMILI HIVYO WAOSHA VINYWA SITAKI SWALI LOLOTE.

    MKIWA NA SWALI KUMUULIZENI YULE SWAIBA WAKE MZEE KUSING MA SONGI ANAYETOKEA KULE AMBAKO MJERUMANI ALITOA KIBANO WAKAKIMBILIA KURUSHA MAJIMAJI NA KUDEDI.

    EEH MOLA MJALIE AFYA ILI apone kabisa MEDI.

    NA KAMA MZEE WA KIARABU KAAMUA KUSAMEHE YULE WA KIGAMBONI BASI NAE KWA NIABA YA WAOSHA VINYWA TUNAMSHUKURU HUO NDIO MOYO WA KIZALENDO YALE YALIPITA SI NDWELE NA NINAMPONGEZA YULE MH. KWA KUAMUA KWENDA KUOMBA MSAMAHA NAONA UMESAIDIA.


    ENE WEI TUTAFIKA TU.

    ReplyDelete
  7. DAAA!! KAKA MICHUZI WEE SANAA UNAIWEZA KWELI,YAANI UMEAMUA KUTUZUGA,ILITUVUTIKE?!

    ReplyDelete
  8. Uwanja Mpya, lakini Ticket bado zinauzwa kizamani!

    Baada ya kupata uwanja mpya ni Dhahiri TFF inabidi wabadili process za uandaaji na uuzwaji wa ticket za mechi hasa zinazochezwa ktk uwanja mpya.

    naamini huu uwanja una vifaa vya kisasa vya kupambana na ticket feki na gate crashers.
    Nadhani 'makomandoo' sasa watafute janja nyingine ya ku-survive. especially kwa mechi za neshno mupya.

    Tanzania Goo...

    ./

    ReplyDelete
  9. Mzee Michuzi inaonekana umejaa, hongera safi sana. Napenda watu wakionyesha mapenzi ya vitendo kwa taifa lao na kwenda uwanjani kwenda kuwashangilia na kuwahamasisha vijana, siyo blah blah tu.
    Jambo ambalo labda linanishangaza mimi ni kwamba hizi tiketi za uwanja mpya zimetengenezwa kwa kufuata washauri wa Kenya, Kenya kuna uwanja gani kama huu wetu. Hii ingefaa tuwafate wataalamu kutoka katika nchi zenye viwanja vingi vikubwa ambavyo vinaruhusu kukaa watu wote. Afrika nchi kama hizi ni Afrika Kusini, Tunisia, Morocco, Misri. Hata tungepata wataalamu wa kutushauri kutoka nchi kubwa kama Ujerumani,Japan, Uingereza ingefaa pia.
    Kila la kheri Stars, dua zote ziko kwenu.

    ReplyDelete
  10. Kiingilio chote hicho cha nini? Tunaenda kuona mpira au kushangaa kiwanja na kujiwekea rekodi za kijinga za kuingia kiwajani siku ya kwanza. Hili nadhani limefanyika makusudi na wakuu wa tiefuefu ili wavune hela kwa kuwa wanajua kwamba kuna limbukeni wengi wetu watakaojitokeza kwenda kutazama madudu. Si bora niende kuangalia uk soccer kweye runinga au miss tz kuliko kwenda kiwanjani.

    msijifananishe na viingilio vya ulaya. Ulaya wana pesa na pia ulaya mtu unalipa pesa kwenda kutazama soka sio butuabutua hiyo ya uwanja wa taifa. Kwa taarifa yako huko uk mechi ya kawaida tu watu wanalipa kiingilio cha takribani sh.40,000 kiasi ambacho hakitofautiani sana na hizo sh. 30,000 za tiefuefu.

    Tiefuefu kama mkiendekeza njaa mtakuja kula majani siku moja. Halafu kibaya zaidi wadosi wanajitokeza kutaka kununua mechi mnawakatalia. Nyie mnajuaje kwamba kiasi walichotaka kutoa mtakipata huko uwanja wa taifa? Kwani nyie ni wapiga ramli au mnataka kuendelea kuwafuga makomandoo wa yanga na simba? Au ndio tuseme kwamba nanyi mna hisa ktk hiyo biashara ya ukomandoo?

    Na nyie makomandoo lazima mkubali kuanza kupiga miayo. Kama mlikuwa mnakaa hapa mjini kwa ajili ya mavuno yatokanayo na ukomandoo, sharti sasa mtafute majembe mwende kijini mkalime.

    Na wale mliozoea kuzamia kama hajui kwamba kile kiwanja kina electric fence nenda mjaribu kama hamjakiona cha mtema kuni!
    Ndimi mdau tpaul(Agent)

    ReplyDelete
  11. Bro Michu

    Hongera naona tumepata wawekezaji wapya wa blogu yetu ooops wafadhili wapya wa blogu yako-Easy Finance

    ReplyDelete
  12. Wadau wa soka jamani

    Mimi nimependa sana hili swala la kuwaleta hawa nyota wa mpira wa miguu pamoja. Nimesikitishwa sana na mtoa maoni aliyesema kuwa baadhi au mmoja wao amechoka. Ukweli ni kuwa kama walikuwa wanacheza mpira mwaka 1980, mimi nimezaliwa mwaka huo (27) na ukioniona siamini kama nikifikia miaka yao nitakuwa na afya na siha njema kama wao.

    Jamani wako fiti tena sana. Wamevaa vizuri, watanashati na wamependeza. Hata kama wana matatizo huko watokako, wanaonekana wenye roho zilizotulia. Si lazima kila picha ikiwekwa kuimwagia sumu

    Mwendapole

    ReplyDelete
  13. Michuziiiiii wacha uzushi ticket umepewa tu hiyo uipigie pic, michuzi wewe ticket yako ile ya sh 3000/ kajamba nani upande ule wa ushuzi wa yusufuuuuuuuu.

    ReplyDelete
  14. Mzee Michuzi,
    Mie niko ughaibuni napata faraja sana kwa kazi unayofanya ya kutupa nyuzi za moto moto. Ila, ndio hivyo bro vumilia matusi ya washenzi, ndio fadhila ya kuwatumikia watanzania (no wonder why...). Narudia tena vumilia bro na mungu akuweke.

    ReplyDelete
  15. Ni kweli NDAKI story tumezipata na tena kwenye Televisheni chanel ten jumamosi tulisikia mahojiano kati ya Mtangazaji Frank Mtao na Mzee wa kiarabu wa Kigamboni kuhusu sakata zima la Mpakanjia. Kwa hiyo Michuzi katubania lakini habari tunazo. Asante Ndaki.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...