rais joseph kabila wa congo akipokea ujumbe maalum toka kwa jk kupitia wa waziri wa nchi ofisi ya makamu wa rais anayeshughulikia mazingira profesa mark mwandosya leo ikulu ya kinshasa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. Ikulu na viti vya plasitiki utafikiri tuko bar sanawari?Hii ni soo kwa kweli

    ReplyDelete
  2. my sentiments exactly.... tena vinaangusha watu viti hivi.

    ReplyDelete
  3. Namuona Mzee Mugurusi hapo!
    Mkurugenzi wa mazingira

    ReplyDelete
  4. Waafrika tuna matatizo sana kila kitu malalamiko!! Ingekuwa ikulu ina mazulia makubwa na viti vya kifahari pia ungechonga tu wewe anony hapo juu na ungesema hoo nchi maskini lakini ikulu ya kifahari!! sasa sijui unataka nini??!! By the way,huo ni upande mmoja tu wa ikulu ya Congo.... mwambie michuzi akupe picha zaidi ili uchonge vizuri!!! shame on you!!KOKENDE LIBOZO EZAKO KOMATEE!!

    ReplyDelete
  5. kwa kweli ikulu ni ikulu viti vya plastic hapana jamani

    ReplyDelete
  6. Hii ni noma. Ikulu lazima iwe na class. viti vya plastik its not class alafu inaonekana wamenunua waliposikia ujumbe unakuja kwani kwenye kiti cha Kabila stika ya bei bado ipo.

    ReplyDelete
  7. IKULU SI VITI AU MAVAZI. NI KAZI. KABILA KASHIDWA LIPI KATIKA DRC? JIBU NI WAZI KABISA. HAKUNA ALICHOSHINDWA. ANAFANYA KILA ALIWEZALO KWA MOYO MKUNJUFU NA UZALENDO WA HALI YA JUU KUIENDELEZA NCHI YAKE. HAJAIBA KAMA MOBOTU. SASA KUNA KOSA GANI KWA IKULU YAKE KUWA VITI KAMA HIVYO? HILI LINATUONYESHA YUKO MAKINI KATIKA KUBANA MATUMIZI YA SERIKALI KWA KUISHI MAISHA YA KAWAIDA TU. HATAKI ANASA. NANI ASIYEUJUA UTAJIRI WA DRC?
    KUMBUKENI HUYU KIJANA ALIWAHI KUTAMKA KUWA ATAFUATA MWENENDO WA MAISHA NA SIASA ZA MWALIMU NYERERE. NA KWELI ANAFUATA. HOJA ZENYE HEKIMA NA BUSARA HAZIJALI UMEKAA WAPI? HATA UKIWA UMEKALIA JAMVI HOJA IKIWA NI NZITO ITASIKIKA TU. NA WATU WATAKUBALIANA NAYO.
    ACHENI KUANGALIA VITU, ANGALIENI UTU NA UCHAPA KAZI. kituo.

    ReplyDelete
  8. Nikitaka kuburudika baada ya kazi sinywi Tusker, naingia katika blog ya Michuzi niwasome watanzania walivyo mabingwa wa kuongea. Nyie wa-TZ mnapenda sana kuongea, mnajifanya mnajua kila kitu, wengine huwa nadhani wanaandika hizi comments wakiwa wamelewa chakari. Jaribuni kutumia hii blog kuwa constructive badala ya yakuifanya kama kijiwe cha kahawa. Mnajiabisha sana ndugu zangu wa-TZ.
    Sasa hivi mnaongelea masuala ya ubaguzi, lakini ninyi ndiyo mmewasaidia wa-KE na wa-UG kuona ukabila hauna maana, sasa iweje nyie mnajionyesha waziwazi katika "SHINDANO LA MREMBO WA BONGO?"
    Sasa hebu angalia hapa hata mambo ya ndani ya DRC nyie mnakuwa mabingwa wa kuisemea DRC na kumponda Mheshimiwa Rais Joseph Kabila. mimi kwa mawazo yangu vitu siyo kazi wala ufahari.
    TAMBULA MALEMBE MOKILI YA BATO

    ReplyDelete
  9. Kiusalama viti vya Plastic ni bora kuliko makochi sababu unaweza ona kila kitu tofauti na kochi ambalo mtu aweza futika bomu ukalikalia mkundu ukakutoka nje likifumka.

    Ikulu ya Kwa kabila si kama ikulu zenu za kwa Michuzi kulikojaa amani na utulivu ngedere nyie.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...