mdau wa kigogo mwisho, Dar, anapenda kutoa Eid Mubarakh kwa wadau wooooooote wa globu hii. ujumbe anasema; kazi na dawa....anapenda salamu zimfikie msela wake wa loooongi alieko majuu ya wapi sijui huko aitwaye nathan chiume. anampa shavu kwa kuanzisha blogu mpya kabisa iitwayo http://tzcommoncents.wordpress.com/

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 17 mpaka sasa

  1. Hivi wewe mzima au mwehu? hii suruali si ungeivalia shingoni tukajua moja?

    ReplyDelete
  2. Huyu akijamba shuzi linatokea kifuani -sentimeta chache kutoka mdomoni, na walleti yake iliyo mfuko wa nyuma anaitolea begani...mambo hayo, New York wanavalia magotini, bongo mabegani.

    ReplyDelete
  3. mh! papaa huyu kiboko, naomba kuuliza...ikibidi masuala ya haja ndogo chapchap INAKUWAJE?...kazi kwelikweli

    ReplyDelete
  4. @ ndumba

    comment yako imenivunja mbavu. imagination zako kiboko baba'ke. aminia! hahahahaha

    ReplyDelete
  5. Hahahahahahaha!!!! ka Michu dah..
    yaani umenichekesha hadi basi.kweli kazi na dawa.
    S.

    ReplyDelete
  6. Mmmmmmmh,
    Sasa huyu sijui akienda haja ndogo anafanyaje.Naona mkanda uko kwapani kabisa.Sijui mfuko wake wa nyuma utakuwa sehemu gani.Mmmmh hii kali.Nimecheka ila inabidi sasa nishangae tu.Kinachonifurahisha ni kuwa yeye hana wasiwasi kabisa na amepozi kwa ajili ya picha.Au labda shati lake ndo fupi (Kijasti bikozi) hivyo kaamua kushona suruali ya namna hiyo.
    Kaaaazi kwelikweli

    ReplyDelete
  7. .......jamaa alosto inamsumbua,ameishakata tamaa ya maisha.

    ReplyDelete
  8. Sasa bro MIchu! Huyu Jamaa ni muuza gahawa au spea tairi? Maanake kama anatangaza genero taya???

    ReplyDelete
  9. Jamani huyu katoka BAra kaambiwa Pwani (Dar) Kuna "mamende" wanaweza mfanza kitu mbaya so ikabidi ajiwahi msimlaumu.

    ReplyDelete
  10. Hapa jamani inabidi kusaidiana kimawazo. Huyu jamaa ni muuza kahawa na sijui kama kipato chake ni kikubwa kiasi cha kutumia kitambaa cha surali mbili kushona suruali moja. Umasikini wetu unaongezeka pia kwa kutojua matumizi muafaka ya rasilimali zetu. Anyway, kazi njea muuza kahawa.

    ReplyDelete
  11. watu wengine bwana, sijui mnawazaga nini jamani, yani ndumba umenichekesha vibaya sana, sio vizuri hivyo jamani. Big up papaa
    Huyu jamaa bonge la mbunifu

    ReplyDelete
  12. ...nimecheka mbavu sina wazee ila not bad not bad at all jamaaa kapendeza na kiatu kapiga kiwi safi na shati jeupe na inaonekana alikuwa anakuwa wa mwisho darasani kama alisoma na kina Nathan,nathan mwokoe mwenzako mpe mtaji si unajua washkaji hawatupani,unajua nikishuka bongo huwa nakunywa na jaamaa zangu waliochoka na kuishia primary ingawaje nina MBA na kazi nzuri tuu unyamwezini....na Nathan big up bro na kazi nzuri ingawaje huko kwako najua wabongo wengi wavivu wa kusoma

    ReplyDelete
  13. duuuuu jamaa ananikumbusha zamani enzi za mabolingo "mikono mileki mingi,ndukidi, sekizengi , novele generation"nk uncle J.wa radio one ,joachim wa DOdoma na Mwl.Kunyanja kule ludewa mpo?

    ReplyDelete
  14. Nathan mshikaji wako wa Primary kakupa shavu I think that is that is so qute

    ReplyDelete
  15. ah! Nipo hoi katika picha ya comments zilizonivunja mbavu ni hii! Duh! Jamaa kweli mjasiriamali. kwa mtindo huu atauza chai ile mbaya. Michuzi hongera

    ReplyDelete
  16. at least ni msafi.

    Na wanaosema alikuwa wamwisho darasani mnakosea sana.

    Bongo unaweza ukawa na akili lakini uwezo mdogo. Opportunity zinakimbia ni watoto wangapi wanafauli kwenda form one nawazazi wao wanashindwa kuwalipia ada na wanaishia mitaani....

    ReplyDelete
  17. Eejama eejama, hizi comments atakufa mtu kwa kuvunjika mbavu na health insuarance siyo wote tunazo, oohooo!!! Kusema ile kweli ya kumwogopa mola, huyu jamaa ni mnyakyusa kabisaaa wa Tukuyu, kiwira-mwankenja, kaenda Dar kwa magari ya mbio za mwenge, na ana uhakika wa kurudi kiwira na magari ya kampeni ya Mbunge mwaka 2010...uwongo Kasyosyombole????

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...