Home
Unlabelled
mwenge
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Most read Swahili blog on earth
Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.
Du Kaka Misupu Hicho Kitochi Bado Kinasumbua Raia???? Mie Naona Kitupwe Tu Kimepitwa Na Wakati Au Kwa Kua Ni Mtaji Kwa Wenyeviti Na Makatibu Wa Wilaya na Vijiji?? Lol Kitambo
ReplyDeleteUCHEZEAJI WA MALI ZA WANANCHI FANYENI VITU VYA MAANA WACHENI KUTEMBEZA HIKI KIBATARI WATU WANAKUFANYA NJAA WAKATI MRADI HUU UNAKULA HELA SANA
ReplyDeleteDuuh! haya mambo bado yanaendelea tuu? Mwenge wa uhuru gani?
ReplyDeleteHivi mbio za mwenge bado zipo? Zinaeneza sana magonjwa..
ReplyDeleteHivi kuna utafiti wowote wa kisayansi ulishafanyika ili kufahamu faida na hasara za mbio za mwenge tangu zianzishwe? Nauliza ili tujue kama kuna haja ya kuendeleza hizi mbio au la.Anony hapo juu anasema zinaeneza magonjwa...kuna masuala mengine?
ReplyDeleteMadhumuni ya Mwenge wa Uhuru yalikuwa:
ReplyDelete1. Ulete amani pale pasipo amani
2. Upendo mahali palipojaa chuki
3. Na heshima ambapo pamejaa dharau
Nimeimba sana huu wimbo wa "Sisi tumekwisha kuwasha Mwenge, na kuuweka Mlima Kilimanjaro".
Ni kautamaduni ka kihistoria kukimbiza huu Mwenge lakini je ni kweli haya maudhui ya kuwashwa Mwenge bado yanafuatiliwa? Isije ikawa Mwenge umekuwa fasheni tu.
Sasa hivi inasemekana mbio za Mwenge zinachangia sana kusambaza gonjwa la Kisasa.
ReplyDeleteMafanikio mojawapo ya mwenge ni kuwa na utitiri wa shule, na taasisi nyingine zinazoitwa "Mwenge" tanzania nzima.
Haya mambo ya mwenge yameshapitwa na wakati. MWENGE MWENGE!!!
ReplyDeletekWANZA HIZO HELA ZINAZOKUSANYWA HUWA ZINAENDA WAPI?
KUPOTEZEANA MUDA TU. %%%*$£""***UUU
MWENGE UKILALA SEHEM FLANI KESHO YAKE MAELFU YA ''MAPUTO'' HUONEKANA NA WATOTO WA SEHEM HIYO HUFURAHI KUYAPULIZA.KAZI KWELI KWELI JAMANI.MAISHA YETU BWANA.HALAFU WATU HUNYANG'ANYWA SANA PESA ZAO KUCHANGIA MWENGE.MWENGE UDUMU,UDUMU ZAIDI
ReplyDeleteUKIMWI UENEE,UENEE ZAIDI
Hilo torch haliko "environmental friendly" Angalia huo moshi..kuzungusha moshi kama huo kwa miezi sijui mingapi na mafuta yanayotumika ni kupitwa na wakati..Jamani okoeni mazingira..na hao FFU wanalinda nini huo moto...wamekosa cha kufanya? Majambazi yanaiba yanamaliza nchi ninyi FFU mnalipwa kulinda Tochi...!!! Kuwamulika wenye chuki..wenye chuki ni hao wanaotuibia pesa zetu za Kodi..wakusanyeni kwenye jengo moja...muwafukize huo moshi mpaka wakione kilichomfanya kanga akose manyoya shingoni..Karigabagaho...!!
ReplyDeleteTANGU MWALIMU JULIAS K NA KIDOGO MZEE MWINYI, SERIKALI KWA UJUMLA HAIJAWEZA KUPATA MTU SHUPAVU WA KUWEZA KULETA MABADILIKO MAKUBWA KATIKA MIFUMO YETU. HASA YA KISIASA LABDA KWA SABABU WALIO WENGI BADO WANANGOJA FIKRA ZA BABA. PENGINE ATHARI YA "ZIDUMU FIKRA ZA ..." BADO HAIJATUTOKA.
ReplyDeletePOLE POLE TUNATAKIWA TUBADILIKE TUANGALIE KWA KINA KIPI KINAFAA KUENDELEA NACHO NA KIPI KINAFAA KUACHWA. KWA MFANO ATHARI ZA MBIO ZA ZINGEANGALIWA NA ZIKIDHIHIRIKA MBIO ZIFUTWE - WATU HAWA WAKAFANYE VITU VYA MAANA ZAIDI.
TAYARI NCHI INA WATU WENGI WANAOLIPWA BILA YA KUFANYA KAZI ZA MAANA. KWA MFANO BUNGE LETU NI KUBWA MNO UKILINGANISHA NA PATO LETU. WAKATI TULIONAO NJIA ZA MAWASILIANO SASA NI BORA ZAIDI. SASA KUNA HAJA GANI YA WATU MIA TATU KUKUTANA ILI KUZUNGUMZA? NDIO MAANA UNAONA HATA WANACHOKIONGEA NA WANAVYOFANYA BAADHI YA "WAHESHIMIWA" HAWA HAVIENDANI KABISA NA NYADHIFA ZAO. NINA DHANI THELUTHI MOJA YA HAO INATOSHA.
TUTAPUNGUZA VIPI MATUMIZI KAMA TUTAPENDA MIFUMO YENYE KUTAFUNA PESA ZA WANANCHI?