Miss Earth Tanzania 2007 Angel Kileo jana alijumuika na warembo wenzake katika kuwania taji la kipaji (Talent). Mrembo Angel alionyesha ngoma ya kipekee ambapo alicheza na moto akiwa amevalia nguo asilia ya kaniki. Angel Kileo alifundishwa ngoma hii ya kipekee na Kikundi cha sanaa cha Makumbusho na alifanya mazoezi mazito ili kuweza kumudu ngoma hii. Kutokana na utumiaji wa moto, warembo wenzake wengi pamoja na watazamaji waliogopa moto ule, hata hivyo mrembo huyu alikuwa kati ya wachache waliosifiwa kwa kuonesha vipaji tofauti zaidi ya kucheza ngoma za kiasili au kuimba pekee. Mshindi wa talent atatangazwa tarehe 11 novemba.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Go girl!Go..!Sisi tuko na wewe sambamba kukushangilia na kukupa moyo kuiwakilisha NCHI YETU!!!

    ReplyDelete
  2. Miss ka' mganga wa kienyeji. Kama maisha yamekushinda nenda kalime. Mdau

    ReplyDelete
  3. nywele mbona za kidhungu,angepiga afro hapo kiafrica.Kuiga jamani.

    ReplyDelete
  4. Bro Michuzi. Hayo yalikuwa mashindano ya wachawi au waganga wa jadi? Tufahamishe kaka.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...