Mama wa kwanza Salma Kikwete akiwahimiza wananchi wa kijiji cha Hoyoyo wilayani Mkuranga kuzingatia mafunzo ya kuboresha kilimo yaliyoendeshwa na Bwana Moses William Temi ambaye ni Mkuu wa chuo cha mafunzo ya kilimo Mkindo, Turinani Morogoro.Mafunzo hayo yalifanyika katika katika kijiji cha Hoyoyo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. Ukiwakuta wenyeji wako wanakula Mbwa basi nawe kula(ingawa kwa kawaida huwa huli) Huyu mama wa kwanza kweli anajua kuvaa kutokana na mazingira anamojikuta.Hongera mama kikwete kwa kujishusha na kufanana na hao mama zetu wa kijijini.Hayo ndiyo maadili, heshima na utu vyote vinajidhihirisha hapo.Karibu nntaleta posa huko Ikulu.

    ReplyDelete
  2. Huyo ndio mwalimu.

    Nakumbuka mafunzo niliyoyapata chuo cha Korogwe, TULIKUWA TUNAAMBIWA MWALIMU KWA MFANO. sio unakwenda na suti sehemu KAMA HAPO KWA HAO WAMAMA KIJIJINI, unatakiwa uvae kulingana na mahali na jamii inayokuzunguka kwa wakati huo.

    Sasa Mama kikwete nadhani unaudumisha ualimu!!

    WAWA SALMA KIKWETE, MWALIMU KWA MFANO

    ReplyDelete
  3. Naomba Kueleweshwa hapa,Mbona Ziara hizi za Kuhimiza Maendeleo anazozifanya Mama wa Kwanza zipo Mkoa wa Pwani tuuuu??
    Mama tunaomba utembelee na hiyo Mikoa mingine zaidi ya 30 iliyobaki!!
    Well,they say charity always begins at home.

    ReplyDelete
  4. Kweli Mama Salma ni Mwalimu uliyeenda darasa lla waalimu. Hongera Mama yetu wa kwanza. Msalimie Mzee Rashid hope he is doing fine at there.
    Big up

    ReplyDelete
  5. HIZO ZIARA ZA MKOA WA PWANI TU UMEZIONA NGAPI , KUANZIA LINI??????
    MPE MUDA PSE, YAWEZEKANA ANA RATIBA .

    ReplyDelete
  6. Sisemi vibaya ila jamani huyu mama anachapa kazi kuliko wabunge. JK kama anaweza ampe mama Salma haki yake acha kuona kuwa watu watasema mbona Spika Sitta yuko na mama bungeni, Pls JK mpe mama hata ubunge wa viti maalum maana anafanya kazi kupita mfano halafu wala haringi. Adumu mama wa kwanza.

    ReplyDelete
  7. Mikoa ya Kusini na mikoa ya Pwani iko nyuma sana kimaendelea ukilinganisha na sehemu nyingine. Hata hivyo mikoa mingine ziko NGOs nyingi zinafanya kazi ya kuhimiza maendelea na hata kusapoti hayo maendeleo.

    Mama Salma endelea huko huko Pwani na Kusini kuliko kwenda mahala kudublicate kazi na tena hata mafanikio hatutayaona, lakini pwani ukiweka efforts zitaonekana mafanikio yake. Hata hivyo charity begins at home kwa sababu siku mkiondoka Ikulu watu watawacheka hamkufanya lolote kwenu. Hao hao wasawahili wanaolalamika sasa ndio watakaowacheka baadae.

    ReplyDelete
  8. kuna anon ameuliza swali la kishamba kweli!!eti kwanini semina ni maeneo ya pwani tuu!!kwa mtanzania halisi aliyeishi tanzania anauwezo wa kujua kwamba maeneo y pwani ndio sehemu amabyo watu wanataka maendeleo zaidi..mimi nimeishi rufiji na ninajua maisha ya kule,serekali inatakiwa kwa kweli ielekeze nguvu nyingi kule maana ni maeneno ya mesaulika kwa muda mrefu,kwa kweli nampongeza mama kikwete kwa jitaada zake za kusaidia wanawake wa pwani..mungu akubariki mama..nampongeza huyo jamaa hapo juu kwamba kikwete akupe hata uwaziri

    ReplyDelete
  9. Ni kweli mama ni mchapa kazi.Hata mimi naona apewe nafasi ya juu zaidi ubunge au uwaziri anafaa, anajituma hana ufahari ni mzuri saana.endelea mama salma iko siku utapanda cheo.Ninakufagilia wawawaaa.

    ReplyDelete
  10. Mama wa Kwanza alipoenda huko Rufiji alikuta watu wameliua nyama ume(simba dume),kisha wamegawana nyama yake. Michu vipi lile joka lilikuwa majuzi ktk glob mbona halipo tena? Au nalo limeshafanywa kitoweo? Manake tuliambiwa ile bara bara ni ya kwenda Mkuranga,hiko huko alipokwenda mama wa Kwanza.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...