Mambo vipi Kaka Michuzi?
Kwa mara nyingine tena hongera kwa kazi nzuri ya kutupa habari. Tafadhali naomba nipandishie hii kwa wadau, nauliza kama kuna Mtanzania anayeishiBrooklyn,New-York. Mimi naishi hapa na familia yangu(mtoto 1 na mme wangu)tungependa kufahamiana na familia ya watanzania kama wapo mnaoishi hapa.
unawezaukawasiliana nami kwa
Asante Kaka Michuzi
Dada Sophie

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Wewe dada Sophie unatafuta watu wanaoishi Brooklyn tu au NY city in general?

    Na pia unatafuta watanzania wa age group gani?. Unjua miaka hii na siku hizi sio kam zile enzi za 1990.Ukimwona mtanzania basi anakua kama ndugu yako. Siku hizi wabongo tuko wengi sana ila uzuri ni kuwa nchi yetu imetujalia sana tunakusanyika according to social status. Sasa ni wewe tu unataka kusocialised na watu gani?

    Kama wewe ni mtu wa kujirusha basi wanakutanaga wengi tu mahali anapopiga Mao muziki. Nadhani ni New Rochelle au Mount Vernon..Labda kuna watu watakuemail wakupe direction I am no so sure about the address.

    Kama ni watu wa kuswali kama wewe ni muisilamu basi spriengfield, MA kutakufaa. Sio mbali sana once a month it is not that bad to make a trip up there.

    Kama wewe ni wa kanisani basi wapo wabongo wengi wanakutaka according to their faiths and believes.

    Kuna wabongo wanasali pamoja Jersey City, Boston, Philadephia na pia kuna kanisa Broklyn na Manhatan wanasali kiswahili mara moja kwa mwezi Wakenya na Watanzania.

    I hope itakusaidia

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...