mdau wa kimasai akinivisha meno ya simba kama zawadi kwa kuwatembelea ngorongoro. nami nilichangia dala kwa zawadi hiyo ya aina yake

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 18 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 08, 2008

    duh kaka we kweli bahili yaani dala wakati wenzako wanota hadi dola mia

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 08, 2008

    Muungwana mambo ya broke backMountain nini hayo; naona Yero anakucheki kwa haibaa kama anataka kukukata denda vile..au macho yangu tu.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 08, 2008

    Mie ulinistua kidogo kabla sijasoma maelezo ya picha.nikasema moyoni " mikonooooooz gani hii tena kaka michuzi analeta" kumbe unavishwa meno ya simba simchezo kumbukumbu nzuri hio.inabidi hwaimize wadau kutembelea huko sio lazima huwe mtalii kutoka nje ya nchi.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 08, 2008

    we michuzi huu mchezo umeanza lini,mbona jamaa anakutazama kimapenzi,kweli dunia imeharibika,hata wamasai wanamendea

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 08, 2008

    Misupu itabidi uaende gym maana naona kakitambi kanakunyemelea au mambo ya Sullivan? Mara hii !?

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 08, 2008

    WE MICHUZI INAELEKEA UNAPENDA MAMBO YA KISHIRIKINA KWANI JINO LA SIMBA LITAKUSAIDIA NINI??TENA UNATOKA NA NYARA ZA SEREKALI NJE YA HIFADHI!!!KWANI KUNA TOFAUTI GANI YA JINO LA NYUMBU NA SIMBA?!!WOTE NI WANYAMA WANAOKAA MWITUNI...KWANZA UNATAKIWA KULIPIA SEREKALINI HILO JINO,,UNAJUA HUNA RUHUSA KUTOKA NJE YA HIFADHI NA NYARAKA ZAKE?NI SAWA KUCHUKUA JINO LA TEMBO PIA..MDAU NORWAY

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 08, 2008

    Michuzi,
    Huyo mmasai ni Mwanaume au Mwanamama?

    Kama ni mwanamama, basi ni nusu poa.
    otherwise kama ni ME basi si poa, manake jinsi mlivyosimama na hizo konoooozzzzzz... inakua si sawa!

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 08, 2008

    Ankuvalisha meno ya simba au ndio mikonozzzz ya pambaja hehe nawewe umepatikana leo

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 08, 2008

    Kaka Misupu!?itabidi uanze joging
    hilo friji ulipunguze,we bado young
    uwezi kuwa na kitambi cha kutisha!

    ReplyDelete
  10. AnonymousJune 08, 2008

    misupu mwambie huyo jamaa aondoe huo mkono wake haraka kabla hatujakubatiza. Kule magharibi hayo mambo yameshakubalika wababa kwa wababa kuwekeana mikonozi ya kimapenziiiiiii. I hope you're not one of them baby

    ReplyDelete
  11. AnonymousJune 08, 2008

    kaka kifriji hicho noma.ingia gym kaka.usije ukaja shindwa kupata raha nyingine bureeeeeeeeeee

    ReplyDelete
  12. AnonymousJune 08, 2008

    Kama kawaida misupu naona mkutano wa suvilian umekutoa kitambi kabisa pamoja hiyo fulanazzzzzz basi raha tupu mzee wa kazi poa hao hiyo dala inawatosha sisi wengine ulivyosema dala tumeshakuelewa sio lazima usema dola hiyo unamaanisha dola sio dala big up mkuu....

    ReplyDelete
  13. AnonymousJune 09, 2008

    MICHUZI UMEKUMBATIWA KAKA

    ReplyDelete
  14. AnonymousJune 09, 2008

    Ok, sasa Mithupu,ndio mnavalishana ....wateva,ila mbona mko too close? Usitake tukubadilishie jina shauri yako.

    ReplyDelete
  15. Michuzi,

    Sina uhakika kama meno ya uliyovalishwa yalitoka kwenye Simba aliyekuwa amekufa naturally au aliyeuawa kikatili akiwa kwenye makazi yake….

    Tukiachana na hayo meno ya Simba mimi nasikitika sana juu ya eneo hili la Ngorongoro. Ngorongoro niliyoifahamu zaidi ya miaka 17 iliyopita ni tofauti sana na ya sasa. Crater kulikuwa na Wanyama wengi zaidi kuliko sasa kwa sababu mifugo ya maasai inazidi kutumia eneo kubwa zaidi kwenye Crater kadri siku zinavyokwenda. Wakati ule ng’ombe walikuwa wakiingia kunywa maji na kutoka lakini sasa huendelea kuchungiwa huko ndani na kusababisha uharibifu mkubwa kwa uoto wa asilia. Sababu ni kwamba upande wa magharibi wa Crater rim umeharibiwa sana kwa ukataji miti wa kujengea vibanda vya muda (ambavyo hutumiwa kwa makazi ya kuhama hama) na uchomaji moto na hiyo kumaliza nyasi zilizokuwa zikitumika kulishia mifugo ya Maasai. Miteremko ya Malanja ilikuwa na msitu kakini sasa miti imepunguwa sana.

    Maasai wanazidi kuzaana na kuongezeka idadi kwenye eneo hilo hilo kwa hiyo madhara kwa mazingira yanaongezeka. Mifugo pia inaongezeka na hivyo malisho zaidi yanahitajika. Kijiji cha Kimba kinaongezeka na hivyo kuongeza shughuli za kibinaadamu katika eneo hilo. Na kwa bahati mbaya sana binaadamu ni waharibifu zaidi wa mazingira kuliko viumbe vyote lakini bahati nzuri ni kwamba akielimishwa anaweza kuhifadhi mazingira. Elimu hii haipo kabisa kwa watu wanaoishi katika eneo hilo. Wao wanachofikiria ni mifugo yao ipate malisho bila kufikiri existence ya Crater hiyo.

    Katika barabara ya kutokea View Point kwenda Ngorongoro Sopa Lodge ilikuwa ni eneo ambapo Tembo na Nyati walikuwa wakionekana kwa urahisi lakini sasa kinachoonekana zaidi huko ni Ng’ombe zaidi kuliko Wanyama pori.

    Ukitembelea huko wakati wa kiangazi utashangaa kuona maeneo mengi yanayozunguka Crater hasa magharibi na kaskazini yakiwaka moto. Hata ndani ya Crater pia huwashwa moto. Moto huu wakati mwingine huwashwa na mamlaka kama ‘management tool’ lakini udhibiti wake siyo makini na kusababisha maeneo yasiyokusudiwa kuwaka pia. Kwa mawazo yangu ni Hakuna haja ya moto huu maana Wanyama wapo huko kabla sisi wote wa kizazi hiki kuwepo. Ni vyema tukaacha Nature to take its course. hasara ya moto huu ni kubwa sana kuliko faida. Ingawa mimi sioni kama kuna faida yoyote ya ziada.

    Wageni wengi (kutoka ng’ambo) wanapofika eneo hilo hutamani kama wangezaliwa huku kwa jinsi Edeni hii tuliyozawadiwa na Mungu inavyopendeza. Wao hufikiria mtazamo wetu juu ya ‘lulu’ hii ni sawa na wa kwao. Nashindwa kuelewa jinsi Crater hii ingekuwa nchi za ‘weupe’ ambavyo ingetukuzwa na kutunzwa!

    Ushauri wangu kwa wahusika ni kwamba inabidi tufanye kila njia inayofaa kuhifadhi eneo hili ili lizidi kuwa furaha kwa binaadamu kwa vizazi na vizazi. Hofu niliyonayo ni kwamba kama mambo yataachwa hivi hivi sidhani kama miaka 50 ijayo tutakuwa na Crater yenye umaarufu kama wa sasa maana hapatakuwa na Wanyama pori tena, kijani itakuwa imepotea na eneo litakuwa likifunikwa na vumbi la kutisha.

    ReplyDelete
  16. AnonymousJune 09, 2008

    Hapa Michuuuz alikuwa anaambiwa hivi,'Nikikuambia Mguu Sawaaaaz,nataka hili li shingo lako liwe Ninety Degrees (90*) kwa usawa wa Tumbo,Hapana kutikisa tikisa likiuno,sawa?'.Michuuz akajibu,'Ndiyo Afaaaaaandeeez!'.Huyo kijana wa ki Morani alikuwa akimpa darasa Michuuz kuhusu ukakamavu wa Mbugani.Si unajua tena unaweza ukastukizwa na Kifaru huna hili wala lile,aiseee,mbio zake hapo siyo za kawaida.Sasa bora ujue KungFu na Karate za Kimasai kidogo itasaidia!Kwisa ambia yeye mimi iko Ole Saibull,yeye iko ulisa ulisa ulisa saaa yote,mitu gani hii!

    ReplyDelete
  17. AnonymousJune 09, 2008

    Kuliza si ujinga hivi mbona naona na bwana kaka nae kaweka konoz kifuani kwa huyo Moran?Mm Mm haya.

    ReplyDelete
  18. AnonymousJune 10, 2008

    Mikonoooz Kaka!!! Mmhhh, una bahati mpo Bongo.....mngekuwa San Fransisco wangewauliza mmekaa wote muda gani!!?? Utamaduni unavurugika sana kaka, tunaogopa hata kwenda movie na mwanamume mwenzako.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...