Leo hii timu kamambe ya Fc Bongo ya helsinki imeweza kuwabamiza timu ya Congo goli 1-0 na kujiongezea matumaini ya kuingia katika nusu fainali za michuano ya PREVENTION CUP HELSINKI.

Kesho Jumanne vijana hawa wa FC BONGO watachuana na Nigeria ambao leo hii wamewabamiza Greece goli 3-0 na kuwa sawa kwa pointi 6 kwa 6 na FC BONGO.

Goli la FC BONGO lilifungwa na sentahafu Ubaldino baada kuachia kigongo cha mita 30 kuelekea golini.. Wakongo walijitahidi kurudisha goli hilo lakini ukuta wa FC BONGO ulikua ngangari kinoma.

KILIMANJARO STOCKHOLM MPOOOOO?

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 21, 2008

    Hili chama nimelikubali, yaani washikaji wamekaa kama wachezaji wa kikweli-kweli.

    Good on you boys

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 21, 2008

    kilimanjaro fc wanatisha ulaya yote ndio wenye timu nzuri,soma squad 1 kablau, bandari mtwara,machupa simba sc,william john simba sc,ahmed dadi yanga african,kally ongara yanga african,jameel jabir moro utd,abui moro utd,zak dadi kumbukumbu,

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 21, 2008

    Hongera fc bongo, hivyo ndivyo tunavyotaka, wafungeni huko angalau watu waitambue Tanzania yetu kwamba kitale kipo ila basi tu mafisadi wengi wanaturudisha nyuma.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 21, 2008

    Keep it rollin Bongo F.C.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 22, 2008

    Wee anony wa july 21, 2008 1:41 PM,
    Hao wachezaji wako wa yanga na simba watacheua tarehe 16 august fc bongo wakitia nanga huko stockholm. Tutaigeuza fc kilimanjaro kuwa fc Meru. Fc Bongo ni noma, vijana wadogo wamekulia kwenye maacademy huku wanacheza kitale kwa vipimo sio hao jamaa zako chenga twawala.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 23, 2008

    Haya vijana wetu na wakubwa FC Bongo uzi ule ule. Nakuona Morinyo.... Huyo AK hapo anshtua...

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...