Ruto awasilisha ujumbe wa
Rais Kibaki kwa Kikwete

Na Mwandishi Maalum,

Kasera, Tanga
JK jana Julai 18, 2008 amepokea ujumbe maalum kutoka kwa Rais Mwai Kibaki wa Kenya.
Ujumbe huo umewasilishwa kwa JK na Waziri wa Kilimo wa Kenya, William Ruto (pichani juu), wakati walipokutana kwenye makao makuu ya Jimbo la Mkinga, mkoani Tanga, katika eneo la Kasera.
Katika mkutano huo nyumbani kwa mkuu wa wilaya hiyo, Ruto amewasilisha kwa Rais Kikwete salamu na ujumbe maalum kutoka kwa Rais Kibaki.
Waziri Ruto alifuatana na Balozi wa Kenya katika Tanzania, Mh.Boaz Mbaya.

Waziri Ruto pia amemshukuru Rais Kikwete, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU), kwa mchango mkubwa katika usuluhishi wa mgogoro mkubwa wa siasa uliolipuka kufuatia tofauti kubwa zilizotokana na uchaguzi mkuu nchini humo Desemba mwaka jana.
Ruto alimfuata Rais Kikwete mkoani Tanga ambako Rais Kikwete anaendelea na ziara ya mkoa huo.Ruto ameondoka Tanga kurejea nyumbani Kenya baada ya kuwa amewasilisha ujumbe huo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 19, 2008

    Tunataka ifike wakati na sisi tumpongeze Rais wetu kwa kusuluhisha mgogoro wa kisiasa Zanzibar! Kwanini Rais anakuwa kimbelembele na migogoro ya watu, wakati ya kwetu inatushinda!!!!!!?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...