jeshi la polisi linasaka watuhumiwa sita wa ujambazi ambao kamanda wa polisi wa mkoa wa kipolisi wa dar afande suleiman kova amesema mchana huu kwamba walinaswa kwenye kamera za cctv walipoingia na kupora kiasi cha shilingi milioni 50 kwenye duka la havan's limited barabara ya haile selassie oysterbay jana mchana.


amesema askari wamewatambua kwa majina wawili kati ya watuhumiwa hao sita na msako mkali unaendelea.


wakati huo huo askari wa mkoa huo umekamata kinadada 21 wanaotuhumiwa kujihusisha na biashara ya ngono maarufu kama machangudoa. hiyo ni katika kutekeleza ahadi za 'kuasfisha jiji' alizotoa mara tu alipotua dar kumrithi afande tibaiagana akitokea mbeya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 04, 2008

    hongera baba chapa kazi.
    sweet,
    Arusha.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 05, 2008

    Kwa hili la kamera nampongeza sana kamanda Kova maana itasaidia sana kuwakamata waporaji wa pesa za watu. Hizi kamera zikiwekwa kwenye mabenki,maduka makubwa,nk itapunguza sana uporaji mkubwa wa mali za umma na za binafsi. Well done kamanda Kova!

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 05, 2008

    Hongera sana Kamanda wa polisi kwa hilo. Wakati umefika wa kutumia technology kupunguza uhalifu kama ilivyo kwa nchi zilizoendelea.

    Mdau,
    Columbus Ohio.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 05, 2008

    Tupate na kamera za kunasa mafisadi sasa.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...