mtangazaji maarufu wa eatv ben kinyaiya akifurahi baada ya taifa stars kupiga bao
hata watasha wanaishabikia taifa stars
uzalendo ni wa hali ya juu siku hizi kwa wadau kuipenda taifa stars
kila aina ya mitindo ipo siku hizi kushabikia timu ya taifa

ni fahari ilioje kuvaa bendera ya taifa siku hizi
kinadada wapo bega kwa bega kushabikia timu yao ya taifa
mitaani nako mambo kama kawa
jamaa akikatiza mitaa ya ilala na bendera zake
gari la saidi muchacho ambaye ni shabiki wa bwawa la maini na pia taifa stars
siku ya mechi ya taifa stars ni neema kwa ndugu zetu hawa...





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. huyu Kinyaiya naye vipi na vipini hivyo? Kwa mila za Bongo wanaume rijali hatuweki piercings bwana

    ReplyDelete
  2. It's lovely and beautiful. This means a lot about the mentality of the Tanzanians and the country as a whole. Not many countries in the world today would its citizens be proud of their country, like in West Africa where young men die everyday trying to stowaway in ragged ferries to Spain and EU.Big Up!

    ReplyDelete
  3. Watanzania ni watu wazuri sana Duniani, kimaumbile na "wisdom" yao. Ila wana kasoro moja kubwa sanaaaa, ambayo inaboa. Nayo ni: KUIGA. Wakiiga, wanawapita hata wale walioanzisha kile kitu kiigwacho. Jamaa hapo juu, ni handsome, ila pini kwenye mdomo....ahh come on. Does he really know the reason why people/women put pins on the lower mouth?

    ReplyDelete
  4. mh nhiyooooooo angekua mtu ametoboa mdomo hivyo yuko majuu watu wangemsema kama nini....sasa huyu kulikoni?

    Siamini kijana mzuri hivi katoboa na kuweka sijui hereni chini ya mdomo wake kama thugs.

    ReplyDelete
  5. Hiyo imetulia. Mnamsema kijana wa watu bure muacheni ajirembe apendavyo. Mbona msiwaseme wanao oana wanaume kwa wanaume? Big-Up kinyaiya.

    ReplyDelete
  6. acheni kulialia ktk vitu vidogo.mambo ya kutoboa masikio/pua/mdomo vilianzia kwetu Waafrika ingawa zamani walikuwa wakitumia vijiti na kadhalika.hao wa huko Magharibi waliiga tu na pia kuporesha kwa kutumia jewels.makabira chungu mzima back in the days walikuwa na desturi za kutoboa masikio si kwa wanaume wala wanawake.again, vitu hivyo vimeanzishwa na Africans na hao wenzetu waliiga tu na kuboresha kwa kutumia gold/diamond na kadhalika...punguzeni kulialia bila msingi....

    ReplyDelete
  7. Jamani Kinyaiya ni mrembo sana! anajipenda sana, uacheni apendeze, asipopendeza sasa mnataka apendeze akishakufa? nyie lawakereketa nini? ananivutia kijana huyu!

    ReplyDelete
  8. Ni kweli jamani kijana rijali hawezi kuweka vipini kuvaa herini mnh bdo kuvaa gauni tu

    ReplyDelete
  9. we Uyoga kasome historia yako vizuri. Katika makabila ya kiafrika wanaume walikuwa hawatogi pua na midomo. Kwenye baadhi ya makabila masikio labda, ila nao ni wachache. Hata kwa wamakonde wanawake pekee ndio walikuwa wanaweka ndonya; wanaume walikuwa hawaweki.
    Na kwa yale makabila yaliyokuwa yanaruhusu wanaume kutoboa masikio, midomo, n.k. staili zao ilikuwa tofauti na hii na nia yake ilikuwa kuleta taswira ya kijasiri; ya kikakamavu an kishujaa. Kuwa na wanajeshi (warriors) ambao ukiwaona wanawatishia maadui. Sio unaweza vipini vinakufanya uonekane demu.

    Anyway, hili sio suala la Ulaya au Uafrika. kama ni suala la uafrika, unataka kuniambia katika kabila lake huyu Kinyaiya ndio wanatoga mdomo na kuvaa vipini hivi?

    Na nyie mnaosema tumwache kama alivyo. Ofcourse ni uhuru wake and there is niothing we can do even if we wanted to. Ila we r just commenting and querying, we r entitled to that, for as long as one has not outright gone to defame the other person's character.
    Ila kila jamii ina utaratibu wake, utamaduni wake na mazoea. Kwa vitu ambavyo sio mazoea ya kwetu lazima tuulize. Maana kuna jamii wanaruhusu hata cross-dressing; na transsexualism (transgenderism). Haya basi si uhuru wako, fanya hivyo Bongo uone.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...