Meneja wa Huduma za Jamii wa ZainTanzania, Tunu Kavishe (katikati) akikabidhi boksi lasabuni kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dk. James Nsekela(kushoto) na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, SalumFerej waliopokea kwa niaba ya kituo cha kulelea watotoyatima cha Islamic Yatima Foundation cha Wilaya yaIlemela jijini Mwanza juzi. Zain ilitoa zawadi anuwaikwa kituo hicho.
Meneja Mauzo wa Zain Kanda ya Ziwa,Ally Maswanya (kulia) akikabidhi msaada wa mbuzi nabidhaa nyinginezo vikiwamo vyakula kwa Mkuu wa kituocha kulelea watoto yatima cha Islamic YatimaFoundation cha Wilaya ya Ilemela, Hamza Bakari jijiniMwanza juzi. Katikati ni Mkuu wa Shule ya Sekondari yaIlemela Islamic Seminary, Siraji Ahmed.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dk. James Nsekela (kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Samwel Kamote wakipakua futari wakati wa hafla ya kufuturu iliyoandaliwa na kampuni ya simu za mkononi ya Zain Tanzania kwa waandishi wa habari jijini Mwanza

Meneja Uhusiano wa Zain Tanzania, Beatrice Mallya (kushoto) na Meneja wa Huduma za Jamii wa Zain Tanzania, Tunu Kavishe (kulia) wakifuturu pamoja na wanahabari wa jijini Mwanza
Wanahabari: Baadhi ya wanahabari wa jijini Mwanza, wakipakua chakula wakati wa hafla ya kufuturu iliyoandaliwa na Kampuni ya simu za mkononi ya Zain Tanzania kwa wanahbari wa jijini humo


Zain yafuturisha wanahabari Mwanza

Na Mwandishi Wetu

ZAIN, kampuni ya simu za mkononi yenye mtandao katika nchi 22 barani Afrika na Mashariki ya Kati, imeendeleza programu yake ya kufuturisha katika mwezi mtukufu wa Ramadhani.Safari hii, Zain imewafuturisha wanahabari wa jijini Mwanza, hafla ilizofanyika juzi usiku (Jumatano) kwenye hoteli za La Kairo jijini Mwanza.


Meneja wa Uhusiano wa Zain Tanzania, Beatrice Singano alisema hatua hiyo ya kufuturisha, ni programu iliyopangwa kufanywa na Zain katika kipindi cha mfungo wa Ramadhani.


Mbali ya kuwafuturisha wanahabari, pia Zain ilitoa zawadi anuwai ya vyakula ikiwa ni pamoja na unga wa sembe, ngano, mafuta za kula, sabuni kwa watoto zatima wa kituo cha Yatima Islamic Foundation kilichopo Wilaya ya Ilemela, Mwanza.

Akizungumza baada ya kukabidhi msaada huo kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dk. James Nsekela na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Salum Ferej, Meneja wa Huduma za Jamii wa Zain Tanzania, Tunu Kavishe alisema Zain itaendelea kuwajali wasiojiweza, na pia kampuni hiyo itaendelea kusaidia miradi mbalimbali ya jamii.

Mbali ya Tunu na Beatrice, pia Zain iliwakilishwa na Meneja Mauzo wa Zain Kanda ya Ziwa, Ally Maswanya na Ofisa Biashara wa Zain Mwanza, Amani Boma.

Akizungumza katika hafla hizo, Dk. Nsekela aliyeambatana na Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Samwel Kamote, aliishukuru Zain kwa kujitolea kusaidia shughuli mblimbali ya jamii.

Naye Sheik Ferej alisema amefurahishwa na kitendo cha Zain kuendelea kujitolea kusaidia shughuli mbalimbali ya jamii, na akaiombea dua njema kwa MWenyezi Mungu ili izidi kufanikiwa katika biashara zake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...