kundi la ze nanihii ambalo linajifua kabla ya kuibuka upya hivi karibuni linaendelea kula kuku kwa mrija chini ya ufadhili mzito wa mfadhili mkuu wa yanga, yusuf manji. hapo wapo kempinski walioalikwa wikiendi hii kwenye mnuso mmoja wa nguvu sana. uchunguzi wa globu hii ya jamii umedatisha kwamba ze nanihii wanatarajiwa kuzuru london hivi karibuni kwa ziara fupi kabla ya kurejea na kuanzisha upya libeneke wakiwa na TBC1

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 15 mpaka sasa

  1. KAMUENI VIJANA NAONA ITV IMEWAPA ULAJI BILA KAZI NI FARAJA SANA ILA WATANZANIA WANAZIDI KUUGUA STRESS HANA VIBURUDISHO KISA MONOPOLISTIC(UKIRITIMBA) WA IPP

    ReplyDelete
  2. Wabongo tuache upumbavu usio na sababu. Hawa jamaa comedy yao ni ujinga mtupu. Cha kushangaza Bongo hata wale wenye akili timamu utawaona wanachekelea vituko ambavyo hata mtoto anaona ujinga. Hawa jamaa hawajui ku-act, najuwa wengi mtakasirika lakini that is the fact!

    ReplyDelete
  3. wabongo bwana yaani wewe unaona wajinga ila wakina Warner bros wanavyoact unaona wanaakili sio kwasababu ni wamarekani elewa kunatofauti ya comedy kwenye industry acting pia ni kipaji na ina flow natural kutokana na kipaji ulichopewa sio lazima sio kuiga ok I think their great

    ReplyDelete
  4. Wamenitoka kama chupi ya kuazima!Hawa jamaa siyo bure wamepigwa kipapai hawajui walitendalo!Watakapo kuja rudi sijui ni lini itakuwa sawa na kaniki ilipoteza weusi wake!Hapo simuoni hata actor mmoja anayeweza kupata ajira Hollywood!Wabakie hapahapa wakila ugali wa mhogo kwa kisamvu!Mweeee!Walokosa fadhila hawa!Kweli Baniani Mbaya Kiatu Chake Dawa,nimekubali!

    ReplyDelete
  5. Kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni, ibara ya ... kifungu cha ... Tunahitaji kufurahi baada ya stress za kila siku na pia viongozi wanapelekewa ujumbe kupitia vichekesho. Keep it up Komedy! Huyo anayewaona wajinga.. well it take one to see one!

    ReplyDelete
  6. Kuna watu wanaojaribu kuwakatisha tamaa wasanii! wa nyumbani.
    Kwa tabia hizi za kishamba zinawafanya wasanii wetu kuvunjika moyo sana!
    Cha kushangaza utaona mtu yupo tayari kumfagilia msanii wa nje lakini hayupo tayari kuwafagilia wasanii wa Tanzania...!!!!????
    Tujaribu kuwa wastarabu na wenye upendo...
    Tuache Ushamba na Ulimbukeni

    ReplyDelete
  7. Mpoki hizo pozi zako ni za kishamba mno!!!!!!!!!!!

    ReplyDelete
  8. ohhh ingilishi ingilishi huyo mwengine anasema "i think their great" ohh wiii mbavu sina

    ReplyDelete
  9. asilimia 90 ya komedi kote duniani di ujinga na vituko ndio maana ikaitwa komedi,hizo kumi ni watakalo kua wana lzungumzia watatumia vituko lakini ujumbe utafika humohumo, sasa wewe mwenye kutaka vitu vya maana ingia darasani,mdau usinijue

    ReplyDelete
  10. Nahisi watu wengine ni kama wajui kutumia akili zao kwasababu mtoto anaanza kutambaa kisha usimama mwenyewe hata hao wa hollywood hawakuanzia hapo walianzia mbali cha msingi ni kuwashauli wapi wamekosea ili waboreshe kazi yao. Lakini watanzania wenzangu tuache fikra za kihindi kumtumia mwenzio bila kwa faida kubwa bila kujali hizo pesa unazipataje?bila wao eatv hawana jipya la kuingiza pesa nyingi kama hicho kipindi sasa kwanini wasiboreshe maslai yao ili waendleee na ze comedy show.ipp wanajua walichokipata kutoka kwao ndoo maana hawataki wafanye kazi na tv nyingine,kama ni kuigiza mtu kama Seki Hajaanza leo jamani.

    ReplyDelete
  11. Hiviwabongo wenzangu, kwanini mnakuwa na akili finyu? Sasa tusifie kitu ambacho hakisifiki? Kumbukeni, kuna utu uzima na utoto...na acting ya hawa jamaa ni utoto mtupu. Ndiyo kuna tofauti kubwa sana kati ya wasanii wa Hollywood na wa nyumbani, na sisemi hivyo kwa kuwakatisha tamaa wasanii wetu lakini ukweli lazima uwekwe bayana. Hawa jamaa hawana kitu, yaani chovu kishenzi. Nilikuwa Bongo mwaka huu mwanzoni, kwa kweli nilishangazwa na jinsi wabongo wa nyumbani wanavyopapatikia ujinga. Jamaa wana-act yaani mpaka you feel sorry for them bcs they are NOT funny at all. Na vituko wanavyovifanya ni ujinga mtupu yaani mpaka najiuliza watu wanachekeshwa na nini kwa kutazama Ze comedy?

    ReplyDelete
  12. Mi nawasfu,hawa jamaa kwa kitu kimoja tu,wame weza kujitafutia soko la ndani,wamekubalika na jamii ya watz.Hilo ndo muhimu kwanza.Haya mambo mengine ya uigizaji wao sitaki niingie ndani zaidi kwani kwa kiwango chao cha elimu na ufahamu wa sanaa za maonyesho wanajitahidi,japo wanahitaji utaalamu zaidi ili waweze kufanya zaidi ya hapo,vipaji vipo wanavyo ila elimu ni muhimu na siyo ya madigirii bali kujua zaidi mambo yanayo husu taaluma ya uchekeshaji.sasa wt tusiwakatishe tamaa tuwape maelekezo yatkayo wajenga.ila wasiwasi wangu ni kuhusu hivyo vyombo wanavyo tumia kuonyeshea kazi zao TV inabidi nao waache kunyonya wasanii,waweke mabo wazi katika mkataba yao na wasnii nao wasiwe hewala bwana,wajivunie vipaji walivyo navyo,ndiomaana nasema elimu mhimuitakuwezesha kujua haki zakopia,msiogope kuwa na wanasheria wenu,msiogope kuwa na mameneja wenu ,hi ita wasaidia,

    ReplyDelete
  13. WEEE anoymous wa sept 22,2008 6:12 pm KAA NA HIYO HOLLYWOOD YAKO SIE WATZ WOOOOOOOTE TWAWAPENDA ze comedy wetu... USIJIFANYE na wala USITUNYIME RAHA WEWE UNAWIVU KAMA KIKUNDI CHAKO CHA MAAGIZO KIMEMEZWA NA HAWA JAMAA POLEEEEEEEE. USITUTISHE MWANYE AKILIFINYU WEWE UKOME KUTUKANA KWANI HUWEZI KUTOA KOMENTS MPAKA UTUKANE

    ReplyDelete
  14. WEE 12:33AM USIWE KAMA MZEE MAKAMBA ANAYEPENDA KUTUSEMEA WATANZANIA WOTE BILA KUTUMWA,AKILI ZAKO ZIKO NDANI YA MAJI VINGINEVYO USINGESEMA WATZ WOTE IKIWA PAMOJA NA HUYO UNAYEMPINGA AMBAYE PIA NI MTZ, NANI ALIKUAMBIA YEYE NI MRUNDI? KUDADADEKI!

    ReplyDelete
  15. NIMEFURAHI SANA NA KUMSHUKURU ALIYEWAALIKA WANA ZE NANII KWA FUTARI INAPENDEZA, USHAURI NDUGU ZANGU ZE NANII MNACHOTAKIWA KWA SASA HIVI NI KUJIPANGA KIAFYA, KIELIMU NA KIMAISHA NINYI BADO VIJANA WADOGO AMBAO MUNGU AMEWAPA KIPAJI CHA PEKEE NAWAOMBENI SANA MSIDANGANYIKE NA VITU AMBAVYO AMBAVYO HAVIWAJENGI KIMAISHA.SASA KIELIMU NAOMBENI VIJANA WENZANGU MUENDE SHULE MJENGE KARIA KWENYE KITU CHOCHOTE AMBACHO KITAWASAIDIA KWA MAISHA YENU YA BAADAE MSIJE KUWA NI WATU WA KUPITA PITA KWENYE MABAAA NA KUSEMA MIMI NILIKUWAGA ZE NANII HIYO IMEWAKUMBA MASUPA STAA WENGI SANA AMBAO HAWAKUWA NA CLEAR VISION YA MAISHA YAO, KIAFYA MJITAHIDI SANA KUFANYA MAZOEZI KWANI KWA SASA JAMANI NAONA VIJANA WENZANGU KIDOGO KAUZITO KANAONGEZEKA FANYENI MAZOEZI KIDOGO NA KULA VYAKULA VYA AFYA MSANII YEYOTE MJANJA ANATUMIA HELA NYINGI SANA KUJIWEKA FIT,KIMAISHA HAKUNA KITU KIZURI KAMA KUIFURAHISHA JAMII MSIDANGANYIKE NA HELA AU GOODTIME AMBAZO ZINAMFURAHISHA MTU MMOJA UKIFURAHISHA AU KUELIMISHA JAMII NI BORA ZAIDI KWANI POPOTE UPITAPO UTAJIJENGEA JINA ZURI SANA NA UTAPENDWA NA WENGI IGENI MFANO WA MKUU WA WILAYA YA NANII NA AMBASADA WA ZEIN NA BLOG YAKE SASA HIVI AKISEMA ANAKWENDA POPOTE DUNIANI ATAPOKELEWA NA ATAKULA KULALA BUREEE KWA JINSI BLOG YAKE INAVYOSAIDIA JAMII, JIPANGENI KIMAISHA MTAPATA MAFANIKIO KAMA MTU ANATAKA JINA LENU MUACHIENI KABISA NYIE HATA LEO HII MKIJIITA CHEKACHEKA, BEBA BEBA WATEJA MNAO TU.MSIDANGANYIKE KABISA VIJANA WENZANGU NA GOODTIME ZISIZO NA MALENGO.
    KIPEPEO TOURS
    WWW.KIPEPEOTOURS.COM

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...