aghalabu magari ya aina ya benzi hupendelewa sana katika sherehe kama za harusi na kadhalika. je wadau kuna anayeweza kutueleza sababu?

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 34 mpaka sasa

  1. Mi nahisi wengi wanafanya hivyo kama ku "show off" tuu ndo nia kubwa hasa!! ili harusi yao ionekane babu kubwa na pia kwa kumbukumbu huko mbeleni, wakati wanaingia gharama bureee huku gari ni gari tuu.

    na naamini pia wengine wana tumia hiyo chance ya harusi kupanda gari nzuri kama hiyo maana wanajua huko mbele hawata weza pata nafasi kama hiyo, na hivi kwenye harusi kuna michango ndo kabisaa wanafanya full utilisation of resources.
    Ila ushamba tuu, gari ni gari

    Dada Lao

    ReplyDelete
  2. ni kwasababbu yamejulikaa since then kwamba ni excutive cars na ni kweli ni excutive kama BMW kama sisi kwazini kwetu madirectors wanatumia BMW na MECEDERCES tu yaani ndio magari ya kampuni kwa excutive staff

    ReplyDelete
  3. Ndiyo aina ya gari lenye adhi

    ReplyDelete
  4. Sababu Mabenzi yanameremetaaaaa !!

    Lakini kaka Michu mara nyengine mabenzi mengi kama hivi katika nchi masikini sana kama TZ huambatana na harufu ya UFISADI wa kupindukia. Si ajabu mabenzi yote hayo yanamilikiwa na mtu mmoja ambaye ana uhusiano wa karibu na mambo ya kununua rada, EPA, Richmond au mradi wa Kiwira au bosi wa TRA.

    ReplyDelete
  5. ni magari yanayoaminika kuwa ni ya kifahari kwa class ya wa tz na ndio maana hupendelewa kwa maharusi,maana ni siku yao maalum

    ReplyDelete
  6. Sababu ni kwamba kizuri chajiuza kibaya chajitembeza. Kama maraisi wengi na vingunge wamekuwa wakipenda benzis nani atashindana nazo. Wewe peleka corolla yako ya 1998 uone macho yatakayokutazama.

    ReplyDelete
  7. It can be pride, arrogance, show off, or just fun, but the main reason I must say it must be the later.. SHOW OFF, caused by our own inferiority COMPLEX. we may not afford our daily meals, but WE LOVE TO SHOW OFF.. and thats the subject of psychological EXPERT to address that.

    How to unlock that behaviour, I DON'T KNOW. But this is the advice to you guys, the simplest wedding will imply on many occasions, the strongest marriage.

    Thanks Michuzi for Highlighting the issue.

    By Mchangiaji

    ReplyDelete
  8. mie ndio maana naheshimu walimu manake wanakutana na wanafunzi wa kila aina. haya wewe uliyehusisha umiliki wa mabenzi na UFISADI yahusu nini kwenye harusi za watu? inaelekea una roho ya kwanini sana na mtaani kwetu hatukutaki.

    ReplyDelete
  9. Sheer luxury and comfort driving experience

    ReplyDelete
  10. benz ni prestigious car. Siku za sherehe unapenda kutoka unang'aa. Huku wanatumia Bentleys, nk. Kuna gari za kifahari na gari za kawaida. Inategemea na mtoko wako mazee. Kama wewe CEO wa sehemu flani ukitoka ofisini utapenda Rolls Royce, Bentley, BMW au Mercedes Benz ikupokee hapo nje. Basi hata kwenye harusi unataka kupendeza una-hire moja, mbili, tatu, nk.
    Nyie mlidhani ma-limousine ni ya kazi gani kama sio mtoko?
    Kama unapenda sports cars...basi kuna Porsche, Ferrari, Lamborghini...haya sijapata kuona bongo. Kama yapo mnisamehe!

    Conclusion....benz ni gari lenye hadhi fulani ndo maana linatumika katika hafla kama hizo.

    ReplyDelete
  11. kaka michuzi usishangae mimi nkakwambia huku nliko mimi ulaya hii ya uyunani benzi hizo ndo taxi!!

    ReplyDelete
  12. Ni gari la kifahari na harusi ni kati ya siku tatu spesheli za binadamu (nyingine ni siku ya kuzaliwa na ya kumaliza safari ya hapa duniani, ambazo mhusika huwa hajui kinachoendelea). Kwa hiyo ni kujiachia.
    Nimefurahi kumwona tena Mchangiaji katika ukumbi. Karibu tena. ulikuwa umekwenda ulikwenda Afghanstan?

    ReplyDelete
  13. Ni uamuzi tu. Mtu kupenda kitu chake kiwe cha kifahari kwani magari yenyewe ni ya gharama na yenye hadhi na ndio maana viongozi wengi wa nchi hupenda kuyatumia

    ReplyDelete
  14. engilishi ndugu yangu mchangiaji sasa kama umeweka list ya sababu na ya mwisho ni just fun sasa "the later" itakuwa ni show off kivipi? ah mimi najifunza tu engilishi kwa hivyo nielimishe hapo.

    uliyoyasema kidogo yana msingi. kweli wetu weni hutumia pesa nyingi kwa ajili ya harusi tukishindana na wenye kipato na kwa kutaka kujionyesha hatimae tunaanza ndoa na bonge la deni

    ReplyDelete
  15. Jamani kama una hela why not use it? am pretty sure kila mtu anapenda kitu kizuri especially kwa siku kama ya harusi kama unayaweza unajiachia! Kitu kimoja haya mambo haya hitaji ushindani, kama mshikaji aliyekuwa na hayo mabenzi siku ya harusi yake ana hela za kutosha na mtoto aliyemuoa ni bomba kwa kweli ana-deserve kufanyiwa mambo hayo. Hebu check huo ukumbi uliotolewa na kaka Michu recently - Kempinski Kili Hotel...ndio reception ilipofanyiwa.

    ReplyDelete
  16. Mimi naishi Ubelgiji, Brussels na huku bwana haya magari aina na Benzi yanadhalilishwa kweli, huku benzi zinatumiwa kama taxi, asilimia 70 ya taxi zinazoendeshwa huku ni magari aina ya benzi. Ladba kwa upande wangu ni kutokana na kuwa nchi hii ndogo ni makao makuu ya Europe na pia ni Hq ya European Union na Parliament na Nato na office nyingi sana za kimataifa. Lakini all in all wanadhalilisha dhamani ya magari aina ya Benzi kweli

    ReplyDelete
  17. Hizo ni benz S-class new shape, kama zipo kama zinavyoonekana si vipaya watu wakazitumia. pia ni siku kubwa kwa bibi na bwana harusi, nimetembea sana ubelgiji benzi taxi yes zipo lakini sio S-class new shape..kama zikiwepo basi ni chache sana(namjibu mkuu wa juu hapo)Tafadhali bwana. KAMA HIZO GARI ZIPO wacha watu wale raha ndani ya Benz S-Class...
    MBONGO UK

    ReplyDelete
  18. Naishi USA na magari niliyoyaona yanatumika sio benzi wengi wanatumia. Wengi wanapenda classic antique cars kama Rolls Royce, vanden plas, sheerline laundaulette and playmouth bei kweli kukodisha hayo kuliko hata benz

    ReplyDelete
  19. Nyie watu wa Ulaya vipi? Benz kutumika kama tax ni sababu watu wanataka class. Nina uhakika hizo tax ni zile Benz za zamani hizi mpya ni tax za bei mbaya

    ReplyDelete
  20. Sifikiri kama ni kwa ajili ya kusho off kama mdau wa kwanza livyosema huo ni ufinyu wa mawazo. A special day deserves special things... that's all I can say. Ni sawa na kusema kwa nini bibi harusi anapambwa siku ya harusi?

    ReplyDelete
  21. Kawaida yetu wabongo mwendo ni kejeli , matusi na wivu na kwa mtaji huu tutamsidikiza JK mpaka 2015 na kuondoka patupu maana wenye moyo wa kujituma ni mtu na mtu nasio kikundi , kuhusu hayo magari kuwa ya kifahari jamani si kila mtu na uwezo wake hivi hata kama una vijisenti basi usifanye harusi kwa kuogopa kuonekana ya kifahari , ahhh nipeni breki jamani dhana ya kupiga vita ufisadi sio majungu wenye nacho na aliyekitolea jasho acha atumia tuu bwana , maybe niko wrong hivi bado wabongo wanadhani ujamaa upo nini maana viongozi wanatuzeveza kuwa azimio la arusha bado hai

    ReplyDelete
  22. Sababu ni kwamba Benz ni moja ya magari ya bei mbaya kwa namna hiyo hupendelewa na watu wenye uwezo kipesa, kwa nini yanakuwa na bei mbaya, ni kwa sababu yamekuwa engineered perfectly ang beautifully, na yamechukuwa nguvu kazi kubwa/manpower na capital kubwa hadi kuliunda, ni pamoja na BMW, lakini magari ambayo watu wengi huwa hawayataki kwa kuwa yanagharama kubwa kuyatunza kwa vile service zake huchukuwa pesa nyingi, na wengi walionayo huyatumia kwa miaka mingi sana na utashangaa kuwa second hand zake bei zake ni rahisi ukulinganisha na gari zingine, kwa nini, kwa sababu nyingi ya second hand zake zimetumika sana na zimekula miaka na mileage kubwa, tofauti na magari ya bei poa watu wana-tend kuyauza baada ya miaka kidodogo tu hivyo huwabado ni mapya na bei huwa juu kidogo. Kifupi ni kwamba ya status ya walionacho ndo maana watu hupenda kuyakodi kwenye sherehe tofauti ikiwemo na harusi. Lakini kuna gari zingine zimekuwa engineered vizuri kuliko Benz na bei zake kubwa kuliko Benz, but tradionally bado watu hawajazizoea, ni kama vile Coca-cola na vinywaji vingine bado watu wanapenda Coca-cola kuliko vinywaji vingine pamoja na kwamba vyote vinakidhi haja moja. Hata hivyo Benz inaanza kupitwa na magari mengine huku Ulaya na USA, kuna magaro ya Ki-Italy ,
    Ki-Swedish, Ki-Briton, Ki-USA babu kubwa kuliko Benz na yako juu sana, haya mara nyingi hununuliwa na Celebrities aki Becky.

    ReplyDelete
  23. Anonymous 9:27PM, kupambwa na magari ya kifahari hiyo ni mada nyingine tofauti!!! acha kubadilisha topic... sio lazima kila mtu kuchangia, unaweza baki msomaji tuu kama wengine.
    Mpenda maendeleo

    ReplyDelete
  24. LABDA KWA NYUMANI NI KITU CHA KIFAHARI, NCHI YA DENAMRK TAXI ZOOOTE NI BENZI

    ReplyDelete
  25. mi-mposi, mimi nakuahidi mapema, kwenye harusi yangu ntapanda bajaj, na hayo mabenz mtapanda wadau wa blog ya jamii, au vipi?

    ReplyDelete
  26. jamani ile cku ni maalum sana maana ndio sherehe inayokukuta ukiwa na ufahamu,hivyo kupanda benz ni sawa sana kwani ni cku maalum sasa kwa nini usitumie v2 maalum kama hizo Benz na mengine mengi mnayojua ni ya thamani kubwa, sio siri jamani mm mwenyewe natamani sana hiyo cku ya harusi yangu nitataka kupanda Benz!!!!!!!!!!!!.

    ni hayo tu kwa leo.

    Majoy.

    ReplyDelete
  27. Tena huyo mpanda Bajaj ndio atakeyetia fora kuliko hao wapanda benzi.
    We fikiria yule bibie anavyomeremeta na maua yake na bwana harusi kwa pembeni, yaani mnapunga upepo kama malkia akiwasalimu watu wake vile.

    Mwisho, anayesema kwamba taxi zinazotumiwa ni za zamani ni nani? anaishi nchi gani? Benzi za kwanza huwa wengi wa watumiaji ni wateja wa taxi kwa baadhi za nchi za Ulaya.
    Sijui kwa huko UK kwenu mnakoendelea kupanda Taxi za mviringo.

    ReplyDelete
  28. watu wanaoishi nje wanapenda kujifanya wajanja...eti Denmark benz ni taxi...wewe unajua Benz au unaisikia tu? Mimi sikatai kuwa yaweza kuwa taxi...lakini kuwa taxi sio maana ya kutokuwa prestigious. Unajua Mercedes-Benz SLR McLaren inauzwa kiasi gani wewe?
    Unasema benz sio gari la kifahari?...kudadadeki
    Benzi ni luxury na prestigious at the same time.

    ReplyDelete
  29. Huo uluxury ndio unaoacha wenzetu walioendelea kuutumia ili kuwavutia wateja wao, kwahio magari Luxury ndio yanayotumiwa kama Taxi
    Si hapa bongo.

    Wewe nini wewe, nenda Berlin siku moja na ubahatike kupanda kwenye benzi ambalo ndio kwanza limetoka.
    Hata viti vina heater ili matako yasipate baridi.

    Tembea uone

    ReplyDelete
  30. anayetaka kujua taxi za wenzetu apitie hii site http://www.nancarrow-webdesk.com/warehouse/storage2/2008-w27/img.259811.html

    ReplyDelete
  31. Duh kweli hawa wajerumani wameendelea yaani magari kama haya wanayafanya Taxi.
    Na mimi nime google kupata picha hii

    http://farm2.static.flickr.com/1120/1130385682_b5fe016891.jpg?v=0

    ReplyDelete
  32. haya magari yanatumika sana hapa ujerumani kama tax kwa sababu yako durable sana. kwa hiyo mwenye kampuni ya tax ata prefer kununua benz likae miaka 10 na zaidi na likiendeshwa na madereva tofauti kuliko hilo la kijapani litakaloharibika within a short time. lakini privately ukiona mtu ana benzi ujue ana pesa au anataka kujionyesha lakini kajaa madeni. habari ndo hiyo, kazi kwenu wabongo!!

    ReplyDelete
  33. Kuhusu Benz kuwa Taxi ulaya ama/na Ujerumani si jambo la ajabu kwa kuwa zinatengenezwa Ujerumani. Hivyo ununuzi ni nafuu tofauti na gari ya kiJapan ambayo ni imeagizwa.
    Vile vile Benz zina madaraja (class) kulingana na kipato, mfano bei ya E class si sawa na S class.

    ReplyDelete
  34. Ushamba, ulimbukeni, ufisadi... Marriage is unity of 2 people, regardless, big party, small or even nothing. Where do they get all this money to spend???? "UFISADI"

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...